kilichokufanya usimalizie ni nini?
kama ulikuwepo akilini kwangu maana niliifungua kwa bashasha...dah.Nafikir hii habari ungepata wasaa wa kuiandika pemben kwanza kwenye simu au kompyuta ndo uweze kuiweka jamvin ikiwa imekamilika kuliko ulivyoileta robo. Kwa sasa huwez kupata mchango wowote kwa watu inakuwa kama zile hadithi za kwenye magazeti pendwa yanayotoa stori wiki baada ya wiki ili watu waendelee kununua sio hapa jamii forums jamani. Iweke ikiwa imekamilika tafadhali vinginevyo tunachoshana jamani
Hii ni story ya kweli imenitokea mimi mwenyewe.
Nimetapeliwa na mtoto wa mheshimiwa waziri wa serikali ya Tanzania, kijana huyu ambae alikuwa akinitafuta kwa kila njia mpaka kufika nyumbani kwangu, ambapo alinikosa na kuacha ujumbe wenye jina lake na no ya simu ya Assistant wake au Engineer wake. Kwasababu hili jina lilikua si geni kwangu nikaamua kumpigia kujua anachonitafutia ni nini.
Tulionana mlimani city siku iliyofuata nikiwa na mume wangu, Kijana alijieleza sana kwamba alikuwa anasoma chuo kikuu nje ya nchi, wiki mbili zilizopita ndio amerudi, akaamua kunitafuta. Anaamini naweza kumsaidia. Anataka niwe partner kwenye kampuni yake maana alieko nae amekosa kuwa mwaminifu. Kwamba huyu partner wake amekuwa anatumia vibaya pesa ambazo alikua anamtumia kwa ajili ya office wakati akiwa Masomoni.
Kwamba baada ya kutoka Masomoni amemuomba baba yake ampe nyumba, ambayo iliachwa na marehemu mama yake, huwa inakodishiwa kwa dola 3000$ ili awe anapata pesa za matumizi, lakini baba yake akakataa, Na kwa sababu hana jinsi yoyote ya kupata pesa ndio maana anataka niwe patner katika kampuni yake maana anaamini naweza kumsaidia kampuni yake iweze kupata pesa.
Nikamwambia siwezi kukujibu haraka maana mimi tayari nina kampuni yangu na bado ni changa na inafanya biashara tofauti kabisa na ambayo anafanya yeye. Nitaona kama naweza kukuunganisha na mtu yeyote ambae ataweza kukusaidia.
ITAENDELEA KESHO NITAWEKA PICHA NA MAJINA YAKE KAMILI SEHEMU YA MWISHO YA STORY
Haah lipa pesa zangu, maana kama ulipi kudhalilishwa ndio njia pekee, ili kila mmoja akujue. Si unaona story itaendelea kesho, bado una muda wa kulipa.
Wewe ni mwanamke ulieolewa kama sijakosea sasa ilikuwaje huyu kijana akufuate wewe uwe partner wake kwenye kampuni yake na asiende kwa mtu mwingine? We mama una lako jambo!!
Wewe ni mwanamke ulieolewa kama sijakosea sasa ilikuwaje huyu kijana akufuate wewe uwe partner wake kwenye kampuni yake na asiende kwa mtu mwingine? We mama una lako jambo!!
Kwa hiyo mke wako hawezi kufanya biashara na wanaume ni wanawake wenzake tu? Hii ni Kampuni na sisi wote ni wakurugenzi. Mtu yeyote anaweza kuongea na mmoja wetu. Mke ni nyumbani jioni.