mtoto wa miezi nane na nusu hataki kula

Iyokopokomayoko

JF-Expert Member
Sep 15, 2011
1,785
441
mwanangu wa kike ana miezi nane na nusu, tatizo lake kubwa ni kuwa hataki kula kabisa, inaweza kupita hata siku 2 kila tukimpa uji au chakula kingine analia sana kiasi tunaamua kumwacha lakini maziwa ya mama yake ananyonya bila matatizo. Naombeni ushauri wenu madaktari na wengine kwa uzoefu wenu tufanye nini kumuongezea apetite mtoto wetu. tunashukuru kwa ushauri wenumtakaotupatia
 
Hapendi vyakula mnavyompa. Maana tatizo lingekua mtoto hata maziwa ya mama yake angesusa.

Jaribuni recipe tofauti, muone itakuwaje.
Mnaweza mkajaribu kumpondea viazi, uji wa mchele, au hata mkapunguza vikorombwezo kwenye hivyo mnavyompa sasa hivi.

Watoto nao ni wajanja, binafsi nimeshapitia.Alikua vya makopo akipewa analia au anatemelea mbali, ila kinachopikwa vizuri nyumbani anakula kwa raha zote.
 
change your menu and recipe, make it funny, muimbie, muweke karibu na tv while eating
 
Hapendi vyakula mnavyompa. Maana tatizo lingekua mtoto hata maziwa ya mama yake angesusa.

Jaribuni recipe tofauti, muone itakuwaje.
Mnaweza mkajaribu kumpondea viazi, uji wa mchele, au hata mkapunguza vikorombwezo kwenye hivyo mnavyompa sasa hivi.

Watoto nao ni wajanja, binafsi nimeshapitia.Alikua vya makopo akipewa analia au anatemelea mbali, ila kinachopikwa vizuri nyumbani anakula kwa raha zote.
Nashukuru mkuu, ila vyakula tunamubadilishia mara nyingi, tunamuandalia wenyewe uji wa lishe, tunampikia na kumsagia ndizi, viazi, karoti na hata juice za matunda kama embe, nanasi nk lakini bado anasumbua kula. Akiwa na miezi 5 hivi ilikuwa ukimpa tuuji alikuwa anazuga anasinzia lakini ukiacha tu kumlisha anafumbua macho na kuanza kucheza, kuna baadhi za siku anaweza akaamua kula mpaka mkashangaa lakini akianza tena kukataa inaweza chukua wiki hataki.

tangu jana asubuhi ameanza akinyonya au kunywa vijiko 2 au 3 vya uji (kwa kumkaba), akimaliza anatapika, pia leo anaharisha kama maji hivi, bado anachezacheza lakini nachanganyikiwa nini nifanye kum-speed-up apetite yake, tafadhali wakuu tusaidiane
 
soseji nayo kakataa? basi nenda mkamuone doctor. inawezekana ana homa. Poleni sana Mkuu. watoto wadogo wanasumbua sana, mtoto unakuta analia wala haemi analilia nini. Mungu awasaidie. Mia
 
jaribu kumwekea pilipili kwenye uji na umpe ugali wa dona mboga matembele alafu uone kama atalia,akilia mpige makwenzi kwenye utosi
 
Jitahidini kumpa mara kwa mara hata kama atakula vijiko viwili itatosha. Kamwe msimlazimishe, kwani inaweza ikasababisha atapike. Na zaidi ya hapo mjaribu kumbadilishia vyakula tofauti tofauti. Siyo vibaya hata wkt mama anakula naye kumwonjesha hata kidogo. Pia jitahidi anapopewa chakula mama asiwepo karibu ili aweze kula. Changamoto ni kwamba kuna uwezekano atakuja kula zaidi kipindi akiachishwa.
tahadhari: kamwe usijaribu kumpa mtoto wako dawa za kumpa hamu ya kula; nyingi kati ya hizo dawa zimeleta madhara ya kiakili kwa watoto baadaye. Hivyo, ni bora kuendelea naye hivyo hivyo na kunyonya maziwa ya mama kuliko kumpa dawa hizo.
 
Nashukuru mkuu, ila vyakula tunamubadilishia mara nyingi, tunamuandalia wenyewe uji wa lishe, tunampikia na kumsagia ndizi, viazi, karoti na hata juice za matunda kama embe, nanasi nk lakini bado anasumbua kula. Akiwa na miezi 5 hivi ilikuwa ukimpa tuuji alikuwa anazuga anasinzia lakini ukiacha tu kumlisha anafumbua macho na kuanza kucheza, kuna baadhi za siku anaweza akaamua kula mpaka mkashangaa lakini akianza tena kukataa inaweza chukua wiki hataki.

tangu jana asubuhi ameanza akinyonya au kunywa vijiko 2 au 3 vya uji (kwa kumkaba), akimaliza anatapika, pia leo anaharisha kama maji hivi, bado anachezacheza lakini nachanganyikiwa nini nifanye kum-speed-up apetite yake, tafadhali wakuu tusaidiane

Yani miezi 5 tayar mmeanza kumpa mtoto vyakula? Na si ajabu mlianza muda mrefu. Mamake ana matatizo gani na matenite leave maanake nini? Ana haki ya kukataa vyakula muda wake bado.
 
Jitahidini kumpa mara kwa mara hata kama atakula vijiko viwili itatosha. Kamwe msimlazimishe, kwani inaweza ikasababisha atapike. Na zaidi ya hapo mjaribu kumbadilishia vyakula tofauti tofauti. Siyo vibaya hata wkt mama anakula naye kumwonjesha hata kidogo. Pia jitahidi anapopewa chakula mama asiwepo karibu ili aweze kula. Changamoto ni kwamba kuna uwezekano atakuja kula zaidi kipindi akiachishwa.
tahadhari: kamwe usijaribu kumpa mtoto wako dawa za kumpa hamu ya kula; nyingi kati ya hizo dawa zimeleta madhara ya kiakili kwa watoto baadaye. Hivyo, ni bora kuendelea naye hivyo hivyo na kunyonya maziwa ya mama kuliko kumpa dawa hizo.
ubarikiwe mkuu, ukipata wazo jingine usisite kunijulisha, kwa hakika naogopa sana kumzoesha mwanangu madawa ya hospitali.
 
vipi hata supu ya pweza kagoma? Mwambie mama ake amnyonyshe bana. acheni mchezo. kama vipi kamuoneni doctor. Mia
 
Yani miezi 5 tayar mmeanza kumpa mtoto vyakula? Na si ajabu mlianza muda mrefu. Mamake ana matatizo gani na matenite leave maanake nini? Ana haki ya kukataa vyakula muda wake bado.
mkuu hapo miezi 5 tulikuwa ndo tunamtest kumpa japo vijiko 2 kwani tulikuwa tunajuwa atakapofikisha miezi ndo tungeanza rasmi kumpa chakula, nashukuru hata hivyo kwa ushauri wako.
 
vipi hata supu ya pweza kagoma? Mwambie mama ake amnyonyshe bana. acheni mchezo. kama vipi kamuoneni doctor. Mia
usinikumbushe pweza mkuu, nimemiss supu yake usiseme, kuna dr mmoja nimeambiwa yupo k/koo mzuri sana kwa watoto, nacheki cku mbili tatu nitampeleka akamchunguze
 
Nashukuru mkuu, ila vyakula tunamubadilishia mara nyingi, tunamuandalia wenyewe uji wa lishe, tunampikia na kumsagia ndizi, viazi, karoti na hata juice za matunda kama embe, nanasi nk lakini bado anasumbua kula. Akiwa na miezi 5 hivi ilikuwa ukimpa tuuji alikuwa anazuga anasinzia lakini ukiacha tu kumlisha anafumbua macho na kuanza kucheza, kuna baadhi za siku anaweza akaamua kula mpaka mkashangaa lakini akianza tena kukataa inaweza chukua wiki hataki.

tangu jana asubuhi ameanza akinyonya au kunywa vijiko 2 au 3 vya uji (kwa kumkaba), akimaliza anatapika, pia leo anaharisha kama maji hivi, bado anachezacheza lakini nachanganyikiwa nini nifanye kum-speed-up apetite yake, tafadhali wakuu tusaidiane

Kitendo cha yeye kutapika baada ya kumlazimisha kula ni dhahiri kwamba tatizo lipo kwenye chakula.Yani hapendi, inawezekana ni namna mnayotengeneza. Jaribuni kumtengenezea chakula ambacho hata nyie mkionjeshwa hamtokunja nyuso. Make it fun. . . . pia ni vizuri ikifika muda wa kula mkawa mnaanza na chakula kabla ya maziwa ya mama yake maana inawezekana hua mnachanganya sana kwahiyo anapokua ameshaonja maziwa (matamu kwake) alafu mkampa chakula ambacho pengine hakina ladha anagundua tofauti right away.Na pia matunda jaribuni moja moja, hawezi kupenda yote kwahiyo jaribuni moja moja mpaka mtakapopata lile atakalokua anafurahia.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom