Mtoto wa kambo

Mtoto wa kambo

Mhh ntasoma tu hapa nijifunze from wakubwa zangu...all in all bikira mzee,hongera sana kwa kuwa considerate kwa mtoto asie wako,Mungu atakubariki,maamuzi mengine utakayofanya yawe kwa interest na well being ya mtoto
 
Last edited by a moderator:
Pole mamy,kwa kweli ni mtihani.
Mama wa mtoto anamtia ujinga mwanae na kwa sababu ni mdogo anayapokea kama yalivyo.
Mumeo anapaswa awe makini hasa,aongee na mzazi mwenzie kuhusu madhara ya anayom feed mtoto katika suala zima la ukuaji wa mtoto,akielewa fine ila akijifanya haelewi basi mtoto asiruhusiwe kwenda kwa mama.
Baba wa mtoto ndio awe muongeaji mkubwa akimueleza mwanawe madhara ya tabia zake,jinsi mnavyompenda na kumthamini na mnavyotamani kumuona anabadilika na kuwa mtoto mwema. Epukeni kumuongelea vibaya mama yake mbele yake. Wewe vitendo vyako ndio viongee zaidi juu ya upendo wako kwake na thamani yake kwako.
Usimlazimishe kukukubali kwa haraka kama mama acha matendo yako yamshawishi.
"Sumu aliyolishwa " haitaisha haraka ila itapungua with time. Anaweza asitamke ila moyoni atautambua mchango wako tu na atakushukuru in the long run.
 
mwanaume mwenye mtoto nje huwa namuangalia kwa jicho la tatu. jitahidi tu kumtreat kama mtoto wako, mtoto akinyea kiganja huwezi kukikata.
Yaani am glad umeweka neno "jitahidi" maanake
... Hawa watoto wanaweza kuwa wabaya ukaichukia na ndoa! Unakuwa fair, pengine unam treat vizuri zaidi ya mwanao wa kumzaa ili asijisikie vibaya. Bado haitoshi na haitatosha. Tenda wema uende zako, akisikia sawa, hasikii atakuja funzwa na ulimwengu!
 
Yaan akupigie simu ya ninii,lea huyo mtoto mpende kama unavyompenda baba yake usihitaji malipo kutoka kwa mama yakee
 
Uzuri ulee akiwaa mdogo umkuzee akuzoee piaa lakin ukiletewaa mkubwaaa kazi ipooo,
 
umejitoa ubazazini?

mleta mada..usichoke...wewe na mumeo wote inabidi mshirikiane..miaka saba bado mdogo...kama akienda kwa mama yake anarudi na tabia mbaya kuliko mwanzo,acheni kumpeleka....muda wa kumkunja samaki huyu ni sasa
Nilijitoa kabla ya Mentor mbona....!!
 
Last edited by a moderator:
mwanaume mwenye mtoto nje huwa namuangalia kwa jicho la tatu. jitahidi tu kumtreat kama mtoto wako, mtoto akinyea kiganja huwezi kukikata.

Duh..mie nnao wawili, halafu nawapendaje wanangu! Mpaka huwa nafikiria sitakuja kuoa tena, wanangu wasije teseka bure. Ila usituchukie hivyo single parents wa kiume, we really are good people, best you can ever have!
 
inabidi baba awe na maamuzi na ujasiri wa kuyasema hayo kwa mama wa mtoto. Km yy aliweza kuzuiwa asimuone mwanae basi ni wkt wake nae mtoto apunguze kwenda kwa mamake ikiwezekana mara moja kwa mwaka na kwa siku chache sana mpaka afikie umri wa kujitambua ili mpate wasaa mzuri wa kumlea kwa maadili ya famila yenu..
Hamna kinachoshindikana ktk upendo hasa mtoto mdogo. Hamfahamu baba ni nani na mama ni nani ila huwatofautisha kwa upendo wao kwake.
 
huyo mme wako niaje anaruhusu vipi mtoto wake kulelewa hovyo alafu achukui hatua zozote hapo yeye ndo inabidi awe mkali kwa mtalaka wake juu ya malezi ya mtoto la hasha hawezi amchukue mtoto amlee pamoja na wewe.
 
Pole sana.

Dada yangu wa damu aliolewa na mtu(shemeji) mwenye mtoto kama wewe na mume wako. Waliishi vizuri sana na yule mtoto mpaka walipopata mtoto wakamuita jina linalofanana nae ili asijisikie kama yuko kwa mama wa kambo.

Walikuwa wanalipia gharama zote(tangu hajahamia hapo nyumbani na kuisha nao-alikuwa kwa mama yake)

Tatizo likaja kwa yule mama(aliyezaa na shemeji). Akaanza matusi, maneno kupiga piga simu.

Mtoto akienda kusalimia anarudi amebadilika, tabia etc.

Wakamuonya yule mama na kuna kipindi kesi ilifika mpaka kwa wazazi wa yule mama.

Mwisho wa siku(nilishuhudia kwa macho yangu) yule mtoto alitoka kwa mama yake na SUMU kaambiwa aweke kwenye chai amuue baba na mama yake wa kambo(dada yangu)

Kesi ilifikishwa polisi na ustawi wa jamii(pia shemeji na dada) wakaamua kumrudisha huyo mtoto na asikanyage tena pale.

Mara kadhaa hawa wamama wanaspoil watoto wao hata kama wanaishi kwa mama wa kambo kwa wivu au ujinga wao.

Muombe Mungu, nenda nae pole pole ILA kuwa makini. Kama inawezekana mpelekeni boarding ambayo hata huyo mama haijui. Itamsadia. Atakayekuja kumuharibia ni mama yake mwenyewe
 
Duh..mie nnao wawili, halafu nawapendaje wanangu! Mpaka huwa nafikiria sitakuja kuoa tena, wanangu wasije teseka bure. Ila usituchukie hivyo single parents wa kiume, we really are good people, best you can ever have!

mie siwachukii ila tu inabdi mwanamke awe makini anapotaka kuingia kwenye mahusiano na mwanaume mwenye mtoto nje. kuna changamoto nyingi.
 
Mtoto akishafikisha miaka saba kisheria ana haki ya kuchukuliwa na baba yake?
 
pole sana ila huyo mwanamke aliyezaa nae anakuonea wivu sana na ndio maana anamjaza mtoto upumbavu ili aivuruge ndoa yenu, jitahidi kuongea na mzee wako kuhusu kuwa mtoto asiende ende sana kwa mama kwani wewe upo au kuwe na uangalizi wa kina anapoenda huko ili kuepusha kumjaza mambo yasiyofaa, hata hivyo Mungu awe mbele kwani anaweza hata kukuloga ili uachike

Ushauri wangu ni kuw hao yote yanaezekana kwa kuwa huyo motto yupo hapa Dar na mama mtoto naye yupo hapa hapa.Mpeleke kijjini kwa wazazi wa Mume wako aomeshwe sule huko huko.Mumeo amweleze mzazi mwenzake kusdio hilo na kama akipinga mumeo ni kichwa cha familia atoe maamuzi,au aende ustawi wa jamii adai mtoto kisheria.
 
Maana yangu ni kuwa akienda boarding angalau huyu dada atapumzika kiasi fulani. Kukaana mtoto wa aina hiyo 24:7 inachochosha, na inapoteza malovre ndani ya nyumba. Kule shule atajichanganya na wenzake, kwanza atakua kiakili. Ilishanitokea mimi na ikafanya kazi. Pia msimamo wa baba ndio unaweza kujenga au kubomoa nyumba
Ni kweli mdau nilikuelewa ila mie niliangalia mwisho wa siku itakuaje maana kuna familia jitu lina miaka 25 lakini bado ni fujo tu mama wa kambo, hata kama atakwenda boarding lakini juhudi zifanyike kuhakikisha anarudi kwenye mstari maana ni mtoto mdogo na akiendelea hivyo ukubwani ndio itakuwa shida zaidi (tatizo mama yake mzazi uwezo wa kumtunza hana maana alipokuwa anakaa nae alikuwa anamtumia kama SACCOS ya hela ya matunzo ikitumwa na yeye anaipiga panga lakini na wakati huo huo pamoja na kwamba amemwachia kwenda kwa baba yake bado anataka mtoto awe anamkumbuka na ndio chanzo cha yote anahisi kama akikaa kwa upendo huko kwa babae atasahaulika si unajua malezi ya upande mmoja yalivyo)

All in all malezi ya boarding yanatakiwa kwa watoto wa ujana ila kuhakikisha wakati wa likizo anakuwa anapita kwa mama anakaa siku mbili tatu alafu anapita na kwa mdingi anamalizia likizo anasepa ili ku-avoid mtoto kuegemea upande mmoja (kwa familia zingine huwa hakuna shida kwa kuwa hata kama watu wamepigana chini lakini malengo siku zote ni kuwaweka watoto kwenye mstari kiasi kwamba mtoto anajiuliza ilikuaje mpaka wazazi wakaachana maana kila mmoja ana play part yake pamoja na kwamba kila mtu ana maisha yake)

Pia na mwanamume kumpa ukweli huyo mzazi mwenzke na hata huyo mtoto pamoja na udogo wake kuna namna ya kuongea kumweka sawa unless kama nae atakuwa mpole mpaka amepitiliza
 
najua unavyojiskia,sio kwakuyaona kwa watu and i think we have the same sorrow,unachokiongea nakiona kwangu kwa asilimia 100,chakukushauri ni jua lengo lako katika hiyo ndoa jua kusudi la kumsaidia huyo mtoto,huwezi kupinga kama anadamu yenu,Mungu ni mwaminifu sana usijali watu wanasema nini,hakuna mtu atakufundisha juu yakulea mtu wa ndani ya nyumba yako atakaye ona hastahili kupewa adhabu wala kukemewa anapokosea amchukue nyumbani kwake,mwenzio nashukuru Mungu nimejifunza kua some times negligence is the best answer usisikilize kelele za uyo mama yake yeye yalimshinda ndo mana hakuolewa hapo achana naye.jitahidi usimuendekeze mtoto sisi mama wa kambo*(according to jamii) tumekua tunaonekana wanyanyasaji ukijaribu kumrekebisha mtoto asiye wako mara nyingi watoto hawa hugeuka kitu cha ajabu kwani akikua ataaga analala huku leo na kesho kule mwisho wa siku hayupo kwa baba wala hakufika kwa mama yake usi intertain ujinga utaambiwa kaharibikia mikononi mwako na cha msingi usifanye hila,mlee kama wako..karibu kwenye experience hii ngumu na lazima
 
Back
Top Bottom