PostGE2025 Mtoto wa Ally Kibao atuma ujumbe mzito kwa Rais Samia na PM Mwigulu Nchemba. Sihamasishi maandamano. Sihamasishi vurugu

PostGE2025 Mtoto wa Ally Kibao atuma ujumbe mzito kwa Rais Samia na PM Mwigulu Nchemba. Sihamasishi maandamano. Sihamasishi vurugu

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

Uzima Tele

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2023
Posts
1,532
Reaction score
3,537
Anasema:

1. Ni mwaka mmoja sasa, hakuna ripoti yoyote juu mauaji ya kikatili ya baba yao yaliyofanywa na Polisi Wasiojulikana, waliomshusha kwenye bus wakaenda kumtesa na kisha kumuua kikatili na kuutupa mwili wake kama wa mbwa ktk pori la Ununio

2. Wanashangaa sana kwa sababu wanaona wazi kuwa, kumbe katika nchi hii sasa Kuna sheria za aina mbili; zinazowahusu tabaka la watawala na matajiri na zile zinazowahusu kina sisi tabaka masikini la watawaliwa


3. Hii inathibitishwa na uchunguzi wa mauaji hayo yaliyotokea zaidi ya mwaka sasa toka kwa JESHI LA POLICE kutokukamilika hadi sasa na hakuna taarifa nyingine wanayopata kama familia toka TanPol

4. Haya mambo yabaumiza. Tuliowapa madaraka ya utawala wanadhani wananchi ni wajinga, hawaoni au hawasikii. Matukio ya namna yalianza kidogo kidogo kwa Tundu Lissu kupigwa risasi mwaka 2017 na baadaye wengine wengi kutekwa na kuuwawa na hitimisho ni mauaji ya HALAIKI yaliyotokea 29/10 na siku 3 au 4 baadaye

5. Ametoa ushauri kwa serikali na wenye madaraka (japo katia shaka kama wataelewa na kuuzingatia) kuwa, HAKI ndio mzizi na dawa ya kuepuka mabalaa. Aidha ametaka kila aliyehusika kuua na kuteka awajibike au awajibishwe kisiasa na ksheria

#Kwa taarifa kamili, mrazame na msikilize mwenyewe kwenye video hiyo
==============
Salaam... Nina ujumbe mfupi kwenda kwa Rais na Waziri Mkuu. Naomba msaada wako kusogeza uwafikie. Link za kupakua zipo hapo chini.

Asante.Kwa zaidi ya mwaka mmoja, hatujasikia chochote kutoka kwa mamlaka yoyote.Video hii ni ujumbe wangu kwa Rais na Waziri Mkuu.Sihamasishi maandamano. Sihamasishi vurugu. Huko nyuma, niliwapigania viongozi hawa - nikawaita wapinzani "wapumbavu."

Leo, napoteza imani. Si kwa sababu wanaharakati walinishawishi - bali kwa sababu mfumo unatuangusha.Uongozi unaokubalika unapiganiwa na watu wenyewe. Hakuna haja ya kuwahamasisha. Lakini kama kikundi kidogo kinaweza kuleta "taharuki" nchi nzima - tujue kuna tatizo kubwa zaidi.Lazima turudi nyuma kidogo.

Lazima tukiri. Hakuna taifa lililoweza kuponya majeraha yake bila kukiri makosa yake. Rwanda. Sierra Leone. Afrika Kusini. Historia inatufundisha.Amani si ukimya. Amani ni haki.
 
Poleni sana familia ya Kibao. Natumaini kuwa uponyaji upo njiani
 
Naam naam naona Wana mwagilia petrol katika moto mkali paleeee

Wamesukuma kete Yao vyema kabisa katika kipindi hiki 😁
Sio wao tu, hata UN , na Balozi kadhaa za nchi za Ulaya na Marekani wamekuja na matamko katika kipindi hiki cha kuelekea December 9.
 
Watulie tuli.
Serikali kama hauna madhara haiwezi kukudhuru.
Umesikiliza na kusoma summary, lakini masikini wewe hujaelewa chochote ktk ujumbe wa ndugu huyu!!!

Ujumbe ni kuwa: Is not about usalama wao tu, bali wanatuma ujumbe kwa Samia na serikali yake dhalimu, kwamba, katika mazingira ya namna hii ya watu kutekwa, kuuwawa na vyombo vya dola (japo wanasema ni wasiojulikana) halafu kunakuwa hakuna taarifa zozote za uchunguzi wa kipolisi na kuhakikisha wahalifu wanajamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria, utazuiaje watu kulalamika na kuandamana kutaka yeye Rais na serikali yote kuwajibika na kuachia ngazi kwa kuwa imeshindwa kulinda watu na yenyewe imegeuka kuwa muuaji wa raia wake?

Lakini wewe kwa akili zako ndogo umeishia kufikiri pafupi kwa namna hiihii ulivyoandika hapa. Think twice rafiki. This is a well calculated message which is issued at the right time kuelekea #D9
 
Pole mkuu ila ingekua wakusikiliza,wangeshasikiliza zamani now it's confirmed untreatability..

People in power will never understand people’s misery

Rais wa Madagascar months ago alisema hajui chochote kilichokua kinaendelea nchini kwake wala kufikiri watu wake Wana matatizo..
 
Back
Top Bottom