Nyleptha
Member
- Jun 19, 2012
- 69
- 47
Habari madaktari wa JF?
Naomba msaada wenu, nina mtoto wa kiume ana miezi 7 sasa, tatizo tangu amezaliwa anashtuka sana na mara kwa mara, yaani mshtuko wa mtu anayeogopa kitu ukidondosha hata kijiko tu anashtuka sana hadi anatafuta sehemu ya kujishikilia, kama umembeba anakudaka nguo haraka, akiwa amelala anadaka shuka mradi kutafuta salama yake!
Tumemzoesha katika mazingira ya kutokuwa kimya sana, redio, tv tunawasha kama kawa na analala vizuri, pia tunaangusha vitu vyenye kelele ili azoee lakini wapi.
Akiwa macho ndio kasheshe, ikipigwa honi atashtuka karibu adondoke huku macho yamemtoka kwa hofu. Sijui ni tatizo gani na tiba yake ni nini?
Naomba msaada wenu, nina mtoto wa kiume ana miezi 7 sasa, tatizo tangu amezaliwa anashtuka sana na mara kwa mara, yaani mshtuko wa mtu anayeogopa kitu ukidondosha hata kijiko tu anashtuka sana hadi anatafuta sehemu ya kujishikilia, kama umembeba anakudaka nguo haraka, akiwa amelala anadaka shuka mradi kutafuta salama yake!
Tumemzoesha katika mazingira ya kutokuwa kimya sana, redio, tv tunawasha kama kawa na analala vizuri, pia tunaangusha vitu vyenye kelele ili azoee lakini wapi.
Akiwa macho ndio kasheshe, ikipigwa honi atashtuka karibu adondoke huku macho yamemtoka kwa hofu. Sijui ni tatizo gani na tiba yake ni nini?