Mto Zigi na janga la uchimbaji dhahabu

Galena

Member
Jan 4, 2016
9
15
Mto Zigi ni moja ya mito mashuhuri katika bonde la Pangani. Umuhimu wa mto huu pamoja na huduma ya kimazingira mto huu ndio chanzo pekee cha maji kwa Jiji la Tanga na vitongoji vyake.
Kwa sasa mto huu umeathirika kwa kiasi kikubwa sana. Kutokana na shughuli za kibinaadamu mto huu upo katika hali mbaya inayotishia uwepo wake. Uchimbaji haramu wa madini umetamalaki tena kwenye maeneo muhimu ya vyanzo vyake.
Ukienda kwa mfano Sakale, Nelusanga na hata Kihara mkuu unaweza kutoa machozi kwa kile utakacho kishuhudia. Kiufupi licha ya juhudi kubwa zinazofanywa na mhifadhi wa msitu wa asili Amani bado uharibifu umetamalaki.
IMG_20170213_171834.jpg
IMG_20170213_170013.jpg
IMG_20170213_165720.jpg
 
Uzi mzuri sana huu.
Na huu ndio uzembe unaotuleteaga laana na majanga sisi waafrika, hivi hiyo dhahabu ina manufaa gani ya kiuchumi kulinganisha na uoto wa asili unaosababisha water catchement ya asili ambayo ndio vyanzo vya mto Zigi uliotegemezi kwa maji kwa wakazi wa Tanga?. Binafsi naona mamlaka zote husika zanafanya uzembe wa mauti kwani kwa umuhumu wa uhifadhi wa mto Zigi hao wasaka dhahabu ni janga la Taifa na walipaswa kutolewa huko hata kwa nguvu za kijeshi.
 
Dhahabu inaleta pesa,mto hauleti pesa...acha wachimbe wapate wanachokitaka...tuache kasumba ya kuthamini misitu kuliko watu...eti kuanzia leo huruhusiwi kuchota maji haya sababu tembo watakosa maji...kwahiyo mtu afe apone tembo ?

Kwahiyo mtanzania aendelee kua fukara wakati madini yamemzunguka kisa mto? Tanzania tuna maji mengi kukosa maji siyo leo wala kesho...endeleeni kuchimba vijana wangu
 
Dah uzi mzuri sana huu.Mazingira na vyanzo vya maji ni kitu muhimu sana.Pamoja na athari kuharibu chanzo cha Maji,hao wachimbaji madini (wengi wao hawana leseni) na kwa mujibu wa Mining Act,2010 hawa ni illegal miners.Hutumia Mercury wakati wa "kukamata"dhahabu.Hii Mercury ndiyo balaa kwa watumiaji wa mto huo.Galena fuatilia na matumizi ya Mercury kwenye mto huo.Hiyo mercury inatembea kwenye mto huo na italeta madhara makubwa kwa binadamu kila mto unakopita.
 
Dhahabu inaleta pesa,mto hauleti pesa...acha wachimbe wapate wanachokitaka...tuache kasumba ya kuthamini misitu kuliko watu...eti kuanzia leo huruhusiwi kuchota maji haya sababu tembo watakosa maji...kwahiyo mtu afe apone tembo ?

Kwahiyo mtanzania aendelee kua fukara wakati madini yamemzunguka kisa mto? Tanzania tuna maji mengi kukosa maji siyo leo wala kesho...endeleeni kuchimba vijana wangu
ushauri wa kilevi kutoka kwa mlevi kwenda kwa mlevi mwenzie
 
Dah uzi mzuri sana huu.Mazingira na vyanzo vya maji ni kitu muhimu sana.Pamoja na athari kuharibu chanzo cha Maji,hao wachimbaji madini (wengi wao hawana leseni) na kwa mujibu wa Mining Act,2010 hawa ni illegal miners.Hutumia Mercury wakati wa "kukamata"dhahabu.Hii Mercury ndiyo balaa kwa watumiaji wa mto huo.Galena fuatilia na matumizi ya Mercury kwenye mto huo.Hiyo mercury inatembea kwenye mto huo na italeta madhara makubwa kwa binadamu kila mto unakopita.

Kuna hatari ya kupima watu uzito hapo, ukawakuta na kg400 maana mercury bwana si mchezo..
 
Back
Top Bottom