Mtikila: Nitaenda mahakama ya kimataifa kwa ajili ya kufungua kesi kuhusu Rasimu ya Katiba

Huyu jamaa watu wengi ambao sio makini wanamchukulia kama mtu ambaye hayupo sawa hususani kwa
jinsi anavyoongazo kanisa lake, jinsi anvyofanya siasa zake, na hata maisha yake binafsi kwa ujumla.
Hata serikali inamchukulia kama mtu mkorofi na ambaye anapenda sana kesi.
Mchungaji huyu alishawahi kufungwa jela mwaka mmoja kwa kumkashifu baba wa taifa.
Napenda kumpongeza mchungaji mtilkila kwa ujasiri wake na uwazi wake, mchungaji mtikila alikuwa anaipigania Serikali ya Tanganyika kwa muda mrefu sana, Tumemshuhudia mara nyingi kwenye maazimisho ya uhuru wa Tanzani dec 9 kila mwaka jinsi anavyokorofishana na watu wa usalama pale alipokuwa anataka kuingia uwanja wa Taifa na bendera ya Tanganyika ambao wao walikuwa wanamzuia, vijana wengi hata wazee ambao walikuwa hawaijui bendera ya tanganyika walikuwa wanaionea nyumbani kwake ikipepea.
Mchungaji Mtikila ameshaipeleka Mahakamani Serikali kuhusiana na suala la mgombea binafsi ambapo Mahakama Kuu ilimpa ushindi dhidi ya Serikali lakini Serikali ikakata refaa Mahakama ya Rufani na kushinda.
Tume ya Katiba imetupatia Rasimu ya Katiba ambayo pamoja na masuala mengine imetuletea hoja ya kuundwa kwa Taifa la Tanganyika na pia kuwa na wagombea binafsi. Madai ambayo Mchungaji Mtikila alikuwa anayapigania sana na kwa uwazi hadi kugombana na dola.
Safi sana mchungaji Mtikila , wewe ni mfano wa kuigwa.
 
Christopher mtikila amesema kuwa ataenda mahakama ya kimataifa kwa ajili ya kufungua kesi kuhusu rasimu ya katiba kutoitambua tanganyika.....hapa namuunga mkono mia kwa mia. Mtakubaliana nami kuwa siku chache zilizopita tumesikia habari ya kutolewa kwa rasimu ya katiba....rasimu hii si katiba kamili bali ni hatua kuelekea katiba kamili. Rasimu hii inatoa fursa kwa watu mbalimbali kuikosoa au kueleza baadhi ya mambo ya kuongeza au kupunguza.



Kuna mambo machache ambayo tusipokuwa makini na kuendelea kuisifia sifia bila kuichambua kwa umakini tutakuja kushtukia '' majuto ni mjukuu''. Maneno haya hayamaanishi kuwa rasimu ni mbaya! Lahasha! Ina mambo mengi ambayo ni mazuri na yanayokidhi matakwa ya watanzania walio wengi. Kwa upande mwingine ina machache ambayo yasipowekwa sawa yataleta matatizo mbele....mfano...swala la kutoitambua tanganyika!!!!!!

Hatuwezi kuwa na serikali tatu mbili zinatambulika kwa majina sahihi wakati moja imenyimwa jina lake la asili....iweje isemwe kuwa serikali hizo tatu ni tanzania,zanzibar na tanzania bara hakuna nchi inaitwa tanzania bara...lazima katiba mpya itambue tanganyika kama moja wapo za serikali hizo tatu

Kwa uelewa wangu historia huwa haifutwi, na wakati mwingine ni makosa makubwa kuendelea kuwaza kuwa historia ilikosea wakati hayo makosa ni sehemu ya Historia pia. kwa historia tunayoelekea kuiandika nafikiri si busara kulifuta jina la Tanzania na kurudia jina la Tanganyika huu tukisema kuwa tulikosea kujiita Tanzania. Labda itabidi tufute kila karatasi lenye neno Tanzania, sa sijui tuliozaliwa wakati wa Tanzania tutakuwa halali au tutakubali kuitwa Watanganyika?// nafikiri Mtikila atakuwa na haraka sana atuachie Watanzania tuamue au aendelee kutushawishi tukubaliane nae. siamini kama kuna mahakama yeyote nje ya Tanzania itakayotuchagulia jina, hili liko ndani ya uwezo wetu hatuhitaji mtu wa nje kutuamulia.....Fanya Kampeni mkuu Mtikila!!!! usilazimishe mambo huenda kwa jinsi unavyoelewa wewe wenzio hawaelewi.. wanahitaji kueleweshwa!!!
 
mwacheni mtikila aende atarudi atatukuta tunaendelea kujenga tanzania yetu yawezekana yeye siyo mtanzania.
Tunataka Tanganyika yetu. What is Tanzania Bara?


Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
zile pesa alizopewa na rostam ashazirudishe uyu ni mnafiki,alikuwa anamponda rostam lakin ela zake anapokea,kuweni makin na awa wanasiasa wanafiki wasiwaingize mkenge

hela alizopewa mtikila na rostam aziz hazikuwa za rostam, bali rostam aliiba hela za umma hivyo mtikila hastahili kuzilipa. Rostam ni jizi lililokubuhu.
 
tanzania bara inaendana na tanzania visiwani na tanganyika inaendana na zanzibar. mia
 
Me hapo tu ndyo huwa nachoka
..unajua wanaamini watanganyika hawana kelee
ndyo maana wanawachagulia vitu. hii ndyo inayowafanya
wazanzibar kuamini watanganyika wanautaka muungano
na ndyo walioulazimisha muungano huu kwa mana wakomaa
na jina la tanzania na kusahau la kwao tanganyika me nadhani kuna haja ya
kuitambua tanganyika ya watu 45,000,000 kama inavotambulika zanzibar ya
watu 800,000. NB nasikia eti watani wa watu zanzibar per square meter umezidi
standard za kimataifa. sa inakuwaje hapo na wengine wapo tanganyika.

watu wachache sana lakini kelele ni nyingi mno,wanataka usawa na nchi yenye watu zaidi ya mil 45 ili hali wao hawafiki ata mil 3,eti wabunge 50 kwa 20 haiwezekani hvy ni lazima iwe 50 50,ama kweli hawa jamaa wengi wao ni mapimbi
 
Tunataka Tanganyika yetu. What is Tanzania Bara?


Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums

watu hawajui kuwa tanzania ilikuja baada ya zanzibar na tanganyika kuungana. wenye akili finyu wanadhani tanganyika ilibadilishwa ikawa tanzania. wamuulize yule mzee aliye buni jina la tanzania. mia
 
Hii ni draft tu. tutumie maabaraza ya katiba kupendekeza serikali ya bara iitwe serikali ya Tanganyika
 
ukisoma rasimu ya katiba ibara ya kwanza na ya tatu inatamka neno tanganyika

Ni kweli mkuu
Alama na Siku
Kuu za Taifa


3.-(1) Alama za Taifa ni:
(a) Bendera ya Taifa;
(b) Wimbo wa Taifa; na
(c) Nembo ya Taifa,
kama zitakavyoainishwa katika sheria itakayotungwa na Bunge.
(2) Siku Kuu za Kitaifa zitakuwa ni:
(a)Siku ya Uhuru wa Tanganyika, itakayoadhimishwa tarehe 9
Disemba;

(b)Siku ya Mapinduzi ya Zanzibar, itakayoadhimishwa tarehe 12
Januari;
(c)Siku ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar,
itakayoadhimishwa tarehe 26 Aprili; na

(d)Siku Kuu nyingine zitakazoainishwa na sheria za nchi.
(3) Kila Siku Kuu ya Kitaifa itakuwa ni siku ya mapumziko.

Sasa hapa mimi najiuliza, kama wanaitambua Tanganyika, sasa kwa nini Wanataka nchi mojawapo ya Ushirika wa Muungano iitwe Tanzania Bara??????? - We are crying for you TANGANYIKA
 
Nimeisoma sana hii Rasimu ya katiba...cha ajabu neno Tanzania Bara limetumika alikadhalika na Tanganyika...nauliza hivi Tanganyika = Tanzania Bara? Kwa kawaida neno BARA (mfano: Wa-Bara) maeneo ya Pwani linatumika kama kejeli kwa watu wasio wenyeji wa maeneo ya Pwani. Sasa kwa nini turuhusu wengine kunyanyapaliwa...na kama kuna Tanzania Bara kwa nini kusiwepo Tanzania Visiwani vile vile???!!!!
 
Kweli mkuu tunaomba akina Warioba na timu yake warekebishe haraka kasoro hiyo. Hakuna nchi inayoitwa Tanzania Bara. Nchi iliyoungana na Zanzibar ni Tanganyika full stop. Waache ubabaishaji kwa kututungia jina ambao halipo. Nchi yetu ni Tanganyika na tunataka Serikali ya Tanganyika!
Christopher mtikila amesema kuwa ataenda mahakama ya kimataifa kwa ajili ya kufungua kesi kuhusu rasimu ya katiba kutoitambua tanganyika.....hapa namuunga mkono mia kwa mia. Mtakubaliana nami kuwa siku chache zilizopita tumesikia habari ya kutolewa kwa rasimu ya katiba....rasimu hii si katiba kamili bali ni hatua kuelekea katiba kamili. Rasimu hii inatoa fursa kwa watu mbalimbali kuikosoa au kueleza baadhi ya mambo ya kuongeza au kupunguza.

Kuna mambo machache ambayo tusipokuwa makini na kuendelea kuisifia sifia bila kuichambua kwa umakini tutakuja kushtukia '' majuto ni mjukuu''. Maneno haya hayamaanishi kuwa rasimu ni mbaya! Lahasha! Ina mambo mengi ambayo ni mazuri na yanayokidhi matakwa ya watanzania walio wengi. Kwa upande mwingine ina machache ambayo yasipowekwa sawa yataleta matatizo mbele....mfano...swala la kutoitambua tanganyika!!!!!!

Hatuwezi kuwa na serikali tatu mbili zinatambulika kwa majina sahihi wakati moja imenyimwa jina lake la asili....iweje isemwe kuwa serikali hizo tatu ni tanzania,zanzibar na tanzania bara hakuna nchi inaitwa tanzania bara...lazima katiba mpya itambue tanganyika kama moja wapo za serikali hizo tatu
 
Hakuna nchi iliyowahi kutambulika kwa jina hilo tanzania bara hata wakoloni wote waliotutawala wajerumani na waingereza walitambua na kutuachia nchi ikiitwa Tanganyika
 
me hapo tu ndyo huwa nachoka
..unajua wanaamini watanganyika hawana kelee
ndyo maana wanawachagulia vitu. Hii ndyo inayowafanya
wazanzibar kuamini watanganyika wanautaka muungano
na ndyo walioulazimisha muungano huu kwa mana wakomaa
na jina la tanzania na kusahau la kwao tanganyika me nadhani kuna haja ya
kuitambua tanganyika ya watu 45,000,000 kama inavotambulika zanzibar ya
watu 800,000. Nb nasikia eti watani wa watu zanzibar per square meter umezidi
standard za kimataifa. Sa inakuwaje hapo na wengine wapo tanganyika.

hakuna tena tanganyika ndani ya muungano.
 
Mtikila yupo sahihi maana nakumbuka tangu mwanzo amepigania hii nchi kwa kiwango kikubwa hata hawa tunaowaamini hawajaligundua hili la kuwa na katiba mpya na nakumbuka kipindi anawaita wahindi MA--------- na leo hii ameona kweli inakuja Tanganyika yetu lakini sasa inachakachuliwa.

Hata mie naunga mkono haki ya Mtikila na mie ni haki yangu kuwa TANGANYIKA yetu irudi na tuimiliki ili tuje tuijenge wenyewe na inahitajika na kizazi ili kijue kuwa tuna TANGANYIKA yetu ambayo tuliipoteza zamani....

BIG UP MTIKILA Mch.
 
sure!hata mimi nilishangaa sana maana kuna sehemu inasema jmt imeundwa na zilizokuwa jamh ya watu wa zanzibar na jamhuri ya tanganyika Then hapo kwenye suala la serikali wanasema zanzibar na TANZANIA BARA!!!
 
naamunga mtikila mkono ukisoma rasimu ibara ya 1 inatambua Tanganyika wakati ukisoma ibara ya 2 inaitaja Tanzania bara kama sehemu ya muungano wamejichanganya mkuu
 
Back
Top Bottom