moto wa kifuu
JF-Expert Member
- Sep 17, 2015
- 390
- 60
Mtikila anayo kura moja tu, sisi wenye nchi ndiyo tutaamua hapo 25/10/2015
Sa kama nchi ni yenu raisi mnatafuta wa nini?
Mtikila anayo kura moja tu, sisi wenye nchi ndiyo tutaamua hapo 25/10/2015
Mchungaji Christopher Mtikila amewasifu Dr Slaa na Prof Ibrahim Lipumba kwa kusikiliza na kutii sauti ya Mungu kupitia dhamira zao.
Amedai wagombea wote wawili wa CCM na CHADEMA wana mapungufu lakini kwa mtu yeyote mwenye akili timamu atajua wazi mapungufu yao yanazidiana kwa kiasi kilicho dhahiri mno!
Na kama kuna mtu haoni hilo basi anatakiwa kupimwa akili.
Tatizo ni watanzania wenyewe kuongozwa na hisia badala ya u halisia. Wagombea wanatoa ahadi ambazo hata kwenye Ilani zao hazipo. Wakishachaguliwa itakuwa rahisi kwao kutotekeleza na hakuna wa kuwauliza. Ahadi za huduma za bure ni Ujinga mtupu. Badala ya kuja na sera za kuondoa umaskini ili watu wawe na uwezo wa kulipia huduma hizo wanatuahidi huduma za bure na tunashangilia Kama mazuzu. Huko Ulaya mnakokimbilia kuomba misaada hakuna huduma ya bure ila watu wana uwezo kiuchumi. Hata Maisha magari ana miliki gari yake.
Wengine wanaahidi kuwasaidia bodaboda, mama ntilie na wenyewe wanafurahia, nilidhani watakuwa na sera za kuimarisha uchumi ili kuwe na ajira za kutosha kuondoka na na biashara hizo zisizo na tija. Hizi ni siasa rahisi.
Siasa za uongo ni mbaya, Chadema ni Chama kinachofuata misingi ya Kibepari, hiyo ni safi kabisa kwa maendeleo kuliko siasa za ujamaa kwa ninavyoamini. Lakini napata shida kusikia Mgombea wa. Chadema akiahidi huduma za bure Kama elimu sera ambayo ni ya kijamaa. Huku ni kuwadanganya wananchi ili wawachague.
Yeye Mwenyewe siyo timamu nani atamsikiliza
- Wingi wa sismizi haujengi mlima bali kichuguu.
- Kura za maoni zimeonyesha wazi kuwa, mikusanyiko ya wamachinga, kelele zao na vurugu kwenye mikutano ya FISADI LOWASSA sio kipimo cha umaaarufu.
- ​Wapiga kura halisi wana kazi zao na hawahangaiki na kumpigania FISADI.
Akamuulize kombani kuwa kati ya lowassa na yeye nani kabaki duniani anadunda. Maana nae akiongea shombo sana kuhusu lowassa na Mungu akamjibu
Mch. atafakari kazi za Mungu anayemwamini naugonjwa haumnyimi mtu haki ya kuongoza watu
Ok, well said. Kwa kuongezea tu, ukawa kama ukawa mission yao ilianzia kwenye katiba pendekezwa baada ya kuonekana bunge linatupa rasimu ya Warioba ndipo likapatikana wazo la kuunganisha nguvu hata kwenye chaguzi wakianzia December mwaka jana kwenye serikali za mitaa.
Sasa point ya mtikila iko wapi, ni pale tunapoona katika wenyeviti wenza waliokuwepo wakati wa kuanzisha, hakuna hata mmoja ambaye ameteuliwa kugombea nafasi ya juu yaani rais au makamu, si makatibu wakuu wao au hata makamu wenyeviti wao, au hata mwanachama yeyote mwanzilishi. Mbali na kushuhudia Prof. Lipumba na Dr. Slaa wakijiondoa. Badala yake tunaona watu wa kuazimwa kutoka ccm wakiongoza shughuli za kampeni, tena huyu mmoja (Sumaye) anaongea waziwazi kwamba amekuja kwa ajili ya kuwapa uzoefu. KIUKWELI UKAWA HAWANA SIFA ZA KUONGOZA TAIFA HILI
Swala sio kwamba atakufa au ataishi (tunaishi/tunakufa kwa mapenzi ya Mungu)...
Issue ni, huyo rais unayemchagua hayuko mentally fit kuweza kufanya maamuzi kama rais kwasababu ugonjwawake una affect thinking na decision-making! Ukishindwa kuelewa hapo basi utakuwa mfu wa kufikiri nifah Diva Beyonce
Habari yoyote ya Mtikila haina tofauti na tamko la Wema Sepetu,Ray na Anti Ezekiel.
Swala sio kwamba atakufa au ataishi (tunaishi/tunakufa kwa mapenzi ya Mungu)...
Issue ni, huyo rais unayemchagua hayuko mentally fit kuweza kufanya maamuzi kama rais kwasababu ugonjwawake una affect thinking na decision-making! Ukishindwa kuelewa hapo basi utakuwa mfu wa kufikiri nifah Diva Beyonce
Mkuu hongera kwa kuwa na upeo mpanaOk, well said. Kwa kuongezea tu, ukawa kama ukawa mission yao ilianzia kwenye katiba pendekezwa baada ya kuonekana bunge linatupa rasimu ya Warioba ndipo likapatikana wazo la kuunganisha nguvu hata kwenye chaguzi wakianzia December mwaka jana kwenye serikali za mitaa.
Sasa point ya mtikila iko wapi, ni pale tunapoona katika wenyeviti wenza waliokuwepo wakati wa kuanzisha, hakuna hata mmoja ambaye ameteuliwa kugombea nafasi ya juu yaani rais au makamu, si makatibu wakuu wao au hata makamu wenyeviti wao, au hata mwanachama yeyote mwanzilishi. Mbali na kushuhudia Prof. Lipumba na Dr. Slaa wakijiondoa. Badala yake tunaona watu wa kuazimwa kutoka ccm wakiongoza shughuli za kampeni, tena huyu mmoja (Sumaye) anaongea waziwazi kwamba amekuja kwa ajili ya kuwapa uzoefu. KIUKWELI UKAWA HAWANA SIFA ZA KUONGOZA TAIFA HILI
Mkuu..Am a very fair man..sifanyi mambo kishabiki..Pamoja na kwamba tuna tofauti zetu katika itikadi za kivyama na siasa kiujumla ila nilikuwa nakupenda sana sababu nilikuona una akili kwa kutokutumia propaganda ya ugonjwa ambao ni tuhuma tu.
Nasema tuhuma sababu hakuna mwenye ushahidi wa kitaalamu zaidi ya kuhukumu kwa macho tu.
Achana na hizi siasa za maji taka,you are better than that.
Mkuu..Am a very fair man..sifanyi mambo kishabiki..
Ila kama unamjua Lowassa (atleast kabla ya 2008), usingehitaji taabibu (physician) kukuthibitishia kuwa kuna tatizo.
huyo magufuli yuko mentaly FIT? si anatembea na kibobo cha DAWA
Kumbe jina lako maana yake iko kinyume.