TIMING
JF-Expert Member
- Apr 12, 2008
- 24,891
- 11,288
Mkuu, kama sikosei, saa ya ukombozi ni sasa ilikua katika kitabu cha kuli tulichotumia kwenye fasihi O-level starring akiwa Rashid Majaliwa... yeye alikopi na kupestiNamkubali Mtikila, ukitaka kujua umuhumu wake kwa jamii nenda pale Rugakingira kituo cha sheria Kijitonyama. uone wanavy omsifia kuwa ni mtu aliyeleta mageuzi ya kisheria nchi hii japo yeye si mwanasheria.
Kwa wale wanaofuatilia siasa zake Mtikila alikuwa sumu hata utawala wa Mwinyi na swala la OIC.ndo alilipinga vikali, na kwake ikulu ilikuwa kama sebuleni.
Ndo huyu aliyeingiza misamiati mipay katika lugha yetu, neno kama "MLALA HOI" tungelipata wapi kama siyo Mtikila, neno kama "Gabachori" japo halikuvuma sana, mwanzilishai ni yeye aliwa ana nadi sera zake za "SAA YA UKOMBOZI NI SASA".
Mtikila akiibua kitu anakuwa amefanya research na anajua mwanzo na mwisho wake, na ndo maana kesi zake nyingi hushinda.
Tatizo la huyu mtu ni kushindwa kujimeneji mwenyewe, angekuwa mkombozi wa kweli ktkt nchi hii.