GE2025 Mtia nia wa ubunge jimbo la Vunjo afika kuchukua fomu akiwa na mbwa

GE2025 Mtia nia wa ubunge jimbo la Vunjo afika kuchukua fomu akiwa na mbwa

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Mkalukungone Mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
2,437
Reaction score
5,235
Faustin Mtui, mwanasheria na mkazi wa kata ya Marangu Magharibi, amejiunga rasmi katika mbio za kuwania nafasi ya ubunge wa Jimbo la Vunjo kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), akiambatana na mbwa maalum wa doria waliompatia umaarufu katika mapambano dhidi ya uhalifu.

Soma Pia: Uzi maalum wa wanaotia nia kugombea Ubunge Uchaguzi Mkuu 2025

Mtui alifika katika ofisi za CCM Wilaya ya Moshi vijijini akiwa na mbwa waliovutia hisia za wengi, akieleza kuwa uamuzi wake wa kuwania ubunge umetokana na msukumo wa wananchi waliothamini juhudi zake za kupambana na uhalifu bila kuwa na cheo chochote cha uongozi.

 
Mwaka huu tutaona mengi, sasa huyo mbwa mmoja ndiye analinda Marangu yote??
Ccm kwa utapeli wameshindikana!
 
2025😁😂😂😂🙌🏿🙌🏿🙌🏿👉🏿
Asante Mungu kwa uhai
Kuishi kwingi ni kuona mengi.
 
POLISI JAMII “ATINGA “ NA MBWA WA DORIA KUCHUKUA FOMU YA UBUNGE VUNJO

Katika tukio lisilo la kawaida lakini lenye ujumbe mzito kwa jamii, Faustin Mtui, mwanasheria na mkazi wa kata ya Marangu Magharibi, amejiunga rasmi katika mbio za kuwania nafasi ya ubunge wa Jimbo la Vunjo kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), akiambatana na mbwa maalum wa doria waliompatia umaarufu katika mapambano dhidi ya uhalifu.

Mtui alifika katika ofisi za CCM Wilaya ya Moshi vijijini akiwa na mbwa waliovutia hisia za wengi, akieleza kuwa uamuzi wake wa kuwania ubunge umetokana na msukumo wa wananchi waliothamini juhudi zake za kupambana na uhalifu bila kuwa na cheo chochote cha uongozi.

"Nilikuwa mwanasheria nikiwa nimeajiriwa, lakini niliamua kuacha kazi zangu ili niwahudumie wananchi. Nilirudi nyumbani kutoka masomoni nikakuta kata ya Marangu Magharibi imekumbwa na wimbi la wizi na uhalifu wa usiku.

Nikaanzisha kikosi cha Polisi Jamii na tulianza doria tukisaidiwa na mbwa wetu hawa tuliowafundisha kunusa wahalifu," alisema Mtui mbele ya wanahabari.

Kwa mujibu wa Mtui, mbwa hao waliwezesha kukamatwa kwa wahalifu mbalimbali kwa kunusa hadi kufika walipojificha. Tangu mwaka 2020, amesema, hali ya uhalifu katika Marangu Magharibi imepungua kwa kiasi kikubwa hadi kufikia kutoweka kabisa.
 
Ubunge limekiwa sehemu halina heshima tena, Proff Assad alikuwa sawa kuita dhaifu
 
Back
Top Bottom