Imani za kishirikina zimetawala UBONGO wako
imani ya kishirikina umeiona wapi katika maelezo yake? wewe mwenyewe ndo mshirikina. sikio lako umeliandaa kusikia ushirikina tu wala sio maajabu ya sayansi ya uumbaji wa mwenyezi Mungu.
Ni kawaida baadhi ya miti wakati wa jua kali kutoa maji maji lakini haipendezi kukaa chini ya mti saa 7 mchana wakati wa jua kali unawezwa kukumbwa Shetani mbaya kwani mashetani huwa wanakimbilia kwenye miti wakati wa jua kali. Huo ndio ushauri wangu.inawezekana ni transpiration inafanyika yaani kitendo cha mmea kupoteza maji yakiwa katika hali ya mvuke kupitia stomata ambazo zipo kwenye majani .pia hujatuambia upo wapi wapi kulingana na hali ya hewa hawa maji yakatoka katika hali ya kuwa yamepoa gutation.lakini pia ningependa mzizimkavu unisaidie scientific name ya huo mti au mtoa mada
Muulize kapuya,c utani ni mtaalamu wa mimea aliyebobea,hawa wengine wanahisi tu,ktk hali isiyo ya kawaida nami pia nimewahi kushuhudia mmea mmoja mdogo ambao ukiunyoshea kidole tu unasinyaa wenyewe,mmea huo ni ngumu sana kuuona,na kwa taarifa nilizopewa na yule mzee mwenyeji wangu ktk lile pori la kutisha,(nahifadhi jina) ni kwamba mmea huo hutumiwa sana na wachawi pamoja na waganga hatari wa kienyeji.
refer notice za form two biology, transpiration
![]()
...mbona siyaoni hayo matone yakidondoka...?
yeye huyaona yakimdondokea yeye hivyo subiri akawaulize na wengine aje akujibu.sasa huwa yanakudondokea wewe tu? au unakuta chini ni pabichi?
Mbona unajihami baada ya kutaja ushirikina. Huwa unaushiriki au umeshawahi kuushiriki? Sio kosa lako. Tatizo shallow mind. Duniani hakuna mti wa namna hiyo. Nimesoma miti ya aina mbalimbali, hakuna mti wa aina hiyo. Kama unathibitisha naomba unitajie jina la mti huo kwa lugha ya kitaalamu au hata kwa lugha ya kabila lako.
Hao ni wadudu fulani ambao hukaa vikundi vidogovidogo juu miti mbalimbali, fanya uchunguzi wa kina utagundua hilo, hakuna maajabu yoyote hapo. Kwa sisi tuliokulia vijijini wadudu hao wanaishi hata kwenye miti ya mihogo wakati wa jua kali.
inawezekana ni transpiration inafanyika yaani kitendo cha mmea kupoteza maji yakiwa katika hali ya mvuke kupitia stomata ambazo zipo kwenye majani .pia hujatuambia upo wapi wapi kulingana na hali ya hewa hawa maji yakatoka katika hali ya kuwa yamepoa gutation.lakini pia ningependa mzizimkavu unisaidie scientific name ya huo mti au mtoa mada
Maelezo yako ni sahihi kabisa,nipo maeneo ya Mkoa wa Pwani miti hiyo ni mingi sana na wenyeji wanaiita miombo.Asili ya maji hayo ni mikojo ya hao wadudu na atawaona akichunguza kwa makini .
Sio mtaalamu wa masuala ya misitu ila kwakuwa ninautimamu wa akili ninaweza nikagundua vitu mbalimbali katika mazingira ninayoishi,mfano ni huo mti hapo.
Huo mti upo maeneo ambayo ninapita pindi ninapoelekea katika shughuli zangu za kila siku sio mbali sana na nyumbani ninapoishi.
Mara nyingi ninapopita chini ya mti huo huo ninahisi kuna vitone vinanidondokea,siku ya kwanza nilidhani labda itakuwa ni dalili za mvua kwa maana kulikuwa na wingu la mvua ingawa haikunyesha siku hiyo.
Siku ya pili nilipita jua lilipokuwa kali mno majira ya saa saba,nikadondokewa tena na vitone mithili ya vinyunyu vya mvua ila hakukuwa na wingu pindi nilipoangalia angani,nikashtuka nikajua labda itakuwa ni nyoka anajaribu kunishambulia kwa mate.
Nilipokagua katika matawi na kutupa mawe kadhaa juu ya mti sikufanikiwa kuona kile nilichokuwa ninahisi (Nyoka).
Ila yale matone yaliendelea kudondoka kwa nyakati tofauti tofauti kutoka katika kila tawi,mmh nikaona bora nisepe labda kuna wadudu wanakojoa.
Siku ya tatu ndipo nikaona hapana leo lazima nitoke na jibu kamili ni kitu gani hasa kinaendelea katika mti huo??,
Nikaenda mida ileile ya saa saba kisha nikaukagua sana ule mti sijaona ndege wala aina ya ndege na kama kawaida nikaona matone yakitoka katika kila tawi la huu mti,ilikuwa ni ajabu sana kwangu nadhani hata kwako pia kama endapo hujawahi kuona ama kushuhudia kitu kama hicho.
Na mpaka leo ukifika mida ya jua kali chini ya mti huo utashuhudia mfululizo wa vitonetoka katika majani machanga ya mti huo,kama wewe ulishawahi kuona haya!!,ila kwangu ni maajabu tosha.