Mti wa Ajabu

Mti wa Ajabu

dasenior

Senior Member
Joined
Jul 24, 2012
Posts
138
Reaction score
57
Sio mtaalamu wa masuala ya misitu ila kwakuwa ninautimamu wa akili ninaweza nikagundua vitu mbalimbali katika mazingira ninayoishi,mfano ni huo mti hapo.

Huo mti upo maeneo ambayo ninapita pindi ninapoelekea katika shughuli zangu za kila siku sio mbali sana na nyumbani ninapoishi.
Mara nyingi ninapopita chini ya mti huo huo ninahisi kuna vitone vinanidondokea,siku ya kwanza nilidhani labda itakuwa ni dalili za mvua kwa maana kulikuwa na wingu la mvua ingawa haikunyesha siku hiyo.

Siku ya pili nilipita jua lilipokuwa kali mno majira ya saa saba,nikadondokewa tena na vitone mithili ya vinyunyu vya mvua ila hakukuwa na wingu pindi nilipoangalia angani,nikashtuka nikajua labda itakuwa ni nyoka anajaribu kunishambulia kwa mate.
Nilipokagua katika matawi na kutupa mawe kadhaa juu ya mti sikufanikiwa kuona kile nilichokuwa ninahisi (Nyoka).

Ila yale matone yaliendelea kudondoka kwa nyakati tofauti tofauti kutoka katika kila tawi,mmh nikaona bora nisepe labda kuna wadudu wanakojoa.

Siku ya tatu ndipo nikaona hapana leo lazima nitoke na jibu kamili ni kitu gani hasa kinaendelea katika mti huo??,

Nikaenda mida ileile ya saa saba kisha nikaukagua sana ule mti sijaona ndege wala aina ya ndege na kama kawaida nikaona matone yakitoka katika kila tawi la huu mti,ilikuwa ni ajabu sana kwangu nadhani hata kwako pia kama endapo hujawahi kuona ama kushuhudia kitu kama hicho.

Na mpaka leo ukifika mida ya jua kali chini ya mti huo utashuhudia mfululizo wa vitonetoka katika majani machanga ya mti huo,kama wewe ulishawahi kuona haya!!,ila kwangu ni maajabu tosha.
 

Attachments

  • 1385189536909.jpg
    1385189536909.jpg
    220.3 KB · Views: 5,874
Imani za kishirikina zimetawala UBONGO wako
 
...mkuu mti unapumua ni kawaida kwa viumbe hai...
 
hayo ni maji ya baraka,ukae hapohapo chini ya mti unyeshewe
 
inawezekana ni transpiration inafanyika yaani kitendo cha mmea kupoteza maji yakiwa katika hali ya mvuke kupitia stomata ambazo zipo kwenye majani .pia hujatuambia upo wapi wapi kulingana na hali ya hewa hawa maji yakatoka katika hali ya kuwa yamepoa gutation.lakini pia ningependa mzizimkavu unisaidie scientific name ya huo mti au mtoa mada
 
sasa huwa yanakudondokea wewe tu? au unakuta chini ni pabichi?
 
Mkuu dasenior ni kwa vile umeuliza tena ni vizuri tu ukapata jibu la kisayansi.
Mimi nimesoma biolojia miaka mingi sana lakini ingalau ile sayansi bado imebaki bado kichwani na haijaondolewa na lager ya kila jioni!!!
Hiyo process inaitwa transpiration hata kwa mimea.
Najua humu jamvini kuna mabingwa wa biolojia wanaweza kuongez ufahamu.

Drip.jpg
Dripping Houseplant Leaves.
Photo: © Marie Iannotti (2008) licensed to About.com, Inc.


Question: Why Do the Leaves of My Houseplant Drip?
I haven't been able to find anything about this online, so I thought I’d ask. I brought my potted elephant ear in for the winter and the leaves are "leaking" water on my floors. Is this just a phase until it adjusts to the indoors? Thank you, Kerry.
Answer: This is probably just transpiration, the plant equivalent of sweating. When plants take in more water than they need or if it's really humid or dewy out, they release the excess through the leaves. I see this a lot on my Pothos plants in the summer, but I'm surprised it's happening to you in winter, unless it's been rainy or humid there. It's a normal function, although messy, and it can be controlled by cutting back on the water you give the plant.
 
kwann usiamue kupanda huko huko juu ya mti ukajionee hayo matone yanatokana na nini mkuu

#kunjani kuti
 
dasenior hapa ninapo ishi, mbona ni kawaida kuona miti iki tonesha maji? Ungekuwa na uwezo ungepanda ukaona chanzo ni nini. Kuna mti nilijaribu kuchunguza ile sehemu inayo dondosha matone ya maji ilikuwa imezungukwa na aina flani ya vijiwadudu. Kwa ngu mimi naona ni hali ya kawaida
 
Last edited by a moderator:
Muulize kapuya,c utani ni mtaalamu wa mimea aliyebobea,hawa wengine wanahisi tu,ktk hali isiyo ya kawaida nami pia nimewahi kushuhudia mmea mmoja mdogo ambao ukiunyoshea kidole tu unasinyaa wenyewe,mmea huo ni ngumu sana kuuona,na kwa taarifa nilizopewa na yule mzee mwenyeji wangu ktk lile pori la kutisha,(nahifadhi jina) ni kwamba mmea huo hutumiwa sana na wachawi pamoja na waganga hatari wa kienyeji.
 
Back
Top Bottom