MTEI: Nililipwa Mshahara sawa na Nyerere

amakyasya

JF-Expert Member
Joined
Jun 26, 2013
Posts
3,480
Reaction score
918
Edwin Mtei akiwa gavana anasema alilipwa mshahara sawa na Nyerere akiwa Rais ili kupunguza tabaka la wenye kipato cha juu kutokana na uadilifu wa mwl. Nyerere ambapo kwa sasa ni vigumu sana.
==================================

Chanzo;
Mwananchi
 
Edwin Mtei akiwa gavana anasema alilipwa mshahara sawa na Nyerere akiwa Rais ili kupunguza tabaka la wenye kipato cha juu kutokana na uadilifu wa mwl. Nyerere ambapo kwa sasa ni vigumu sana.
==================================


Chanzo;
Mwananchi

Mzee umechoka pumzika, Maelezo yako yanadhihirisha ulivyo na hata Chama chako pia. Bila aibu unawaambia watz Kuwa ulipunguza mshahara wako kwa Kuwa Mwalimu Nyerere alipunguza wa kwake na kwa kuona Kuwa usingefanya hivyo mshahara wako ungekuwa mkubwa kuliko was Mwalimu, kumbe hukusukumwa na uzalendo wala huruma kwa wananchi wa kipato cha chini, una tofauti gani na wale waliopunguziwa kwa nguvu? Huu ni unafiki usiovumilika kusikika masikioni. Eti Huyu ndio mwasisi wa Chama mbadala! Tumekusikia Mzee hatutafanya makosa kamwe.
 
Ujinga mwingine unatisha sana,

Hivi Nyerere hata asipochukuwa mshahara alikuwa anashida ipi, nyumba bure, kula bure, kulala bure, na huku anazidi kuiangamiza Tanzania kuwa nchi masikini ya mwisho duniani.

Mtei asitafute umaarufu wa Kisiasa kwa kupitia jina la Nyerere, yeye kwanini aliachia/aliachishwa uwaziri? aeleze ukweli.
 
Uwe unasoma na kuelewa kabla Ya kupost, Mshahara wake ulikuepo kisheria na sheria ilikua inamlinda asiguswe na mamlaka yoyote ile juu mshahara wake. Hivyo uamuzi wa kupunguza kipato chake ilikua ni heshima kwa mkuu wake na kwa wananchi.

Je, kwenye CCM Ya sasa nani anaweza kupunguza mshahara wake kwa hiyari achilia mbali kwa lazima.?
 
Huyo mzee hakutaka kabisa kutumikia wa-Tz, hakushiriki kabisa hata kutafuta uhuru japo tayari alikuwa ana kaelimu kake. Na hata kuja kufanya kazi Tz ilikuwa ni kwa masharti ya kulipwa pesa nyingi sana. Hana hata chembe ya uzalendo.

 
Viongozi na wana siasa wetu wapunguze mishahara yao?Thubutu
 
Inaonekana una chuki kubwa sana na mwl nyerere
 
Huyu mzee hakuwa na moyo wa kutumikia watanzania kabisa, ndio maana wakati anakula ajira alitaka hata sheria za kulinda mshahara wake ziwepo.

Nani anayeweza akatuambia mzee Mtei amefanya nn nchi hii zaidi ya kuanzisha CHADEMA SACCOS?

Big up jembe letu la moshi mtei
 

Jamani lini tutaacha ushabiki? Wakati mwingine tutumie akili ya kawaida kubishana wakati aliyoyasema Mtei ni mambo ya msingi na hayagusi vyama kabisa. Yana akisi utaifa mbele na si vinginevyo.

Kuhusu Nyerere hata asipochukua mshahara alikuwa na shida ipi? Jamani! Kama rais hana shida kwa vile anapewa kila kwa nini wanalipwa mshahara wa zaidi ya mil.30?
 
kipind hcho naona huyu mze alikuwa bado na akili kichwani. Sasa amebaki vacum tu
 
Huyo mzee hakutaka kabisa kutumikia wa-Tz, hakushiriki kabisa hata kutafuta uhuru japo tayari alikuwa ana kaelimu kake. Na hata kuja kufanya kazi Tz ilikuwa ni kwa masharti ya kulipwa pesa nyingi sana. Hana hata chembe ya uzalendo.

mtei atueleze kwanini alikataa kupigania uhuru na nyerere?
Kwa nini alitaka kuiuza nchi kwa wazungu?
 
Angalia kuongea bila kufikiri kunaonesha uwezo wa akili uliyonayo kwamba bado changa. Nyerere alijitahidi sana, kuongoza nchi kwa wakati ule ilikuwa kazi ngumu sana ukizingatia na idadi ya uchache wa wanataaluma na Ukabila ambao ulikuwepo. Lakini katika yote aliweza kuwaunganisha watanzania wakaacha ukabila wao, na Serikali kwa wakati ule ilikuwa inatatua mambo ya msingi tofauti na ilivyo kwa sasa. Viongozi wanapenda kuendeshwa kwenye V8 wakati hospital hazina dawa na vifaa vya kutosha, kuuwa viwanda na ukosefu wa ajira, ufisadi.

Hatusemi kuwa Nyerere hana mapungufu ila kwa kiasi chake alifanya zaidi kuliko inavyostahili, kwa hiyo ni miongoni mwa viongozi Bora AFRIKA tena sio Tanzania.

 
Mkweo mbona anatafuna ruzuku kama hana Akili nzuri kwenye Saccoss yenu?


Sent from my iPad Air using JamiiForums mobile app
 
Nyerere hakuwa mhuni, wanaogombea urais hivi sasa wote ni wahuni na wanawekwa na wahuni wenzao, Mtu kama Rage au Kinana eti ni viongozi tegemea watachagua viongozi aina gani?

ni kweli mkuu,ukiwaangalia kinana na rage,sidhani km wana hadhi ya vyeo walivyonabyo,uaani ni wahuni wahuni tu,km ilivo kina membe na bos wake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…