Gwappo Mwakatobe
JF-Expert Member
- Nov 22, 2019
- 1,494
- 1,874
Yanapokuja masuala ya mitazamo au mitizamo (attitudes) kila mtu yuko sahihi kwa upande wake. Kwahiyo hakuna aliye sahihi zaidi kuliko mwingine, wala anayekosea maana ni mtazamo wake.
Wale wanaoona Maalim Seif kakosea tusiwabeze, wana hoja zilizo sahihi kwa mtazamo wao. Na wale wanaoona kapatia wana hoja sahihi kwa upande wao pia. Suala linalobaki kuwa gumu ni je, kugawana vyeo kwa wanasiasa wa juu ndiko kunaleta umoja wa kitaifa kwa Wazanzibari?
Ubaguzi wa kusema huyu chotara, huyu mwarabu, huyu Mpemba, huyu wa Unguja, huyu wa Bara, nk; unaisha? Na ilikuwaje mashehe waliwekwa ndani wakati wa serikali ya umoja wa kitaifa? Ilisaidiaje na itasaidiaje walioteswa kipindi hiki? Kupindua matokeo hadi kufuta uchaguzi kulikujaje chini ya SUK!? Ilikuwaje aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais Maalim Seif hadi akaishia kutopeana mkono na aliyekuwa Rais Dkt Ali Shein, tena msibani?
Umoja wa kitaifa usiwe wa kugawana vyeo kwa wanasiasa wachache, bali uwe wa kuwaunganisha watu, kuondoa dhuluma, ufisadi, ubaguzi na kujaliana Wazanzibar wote. Usiwe wa kuwajali au kuwashabikia wasaka tonge na umaarufu wao pamoja na vyama vyao. Chama pekee cha kukijali na kukijenga iwe ni Zanzibar pekee, basi!
Wale wanaoona Maalim Seif kakosea tusiwabeze, wana hoja zilizo sahihi kwa mtazamo wao. Na wale wanaoona kapatia wana hoja sahihi kwa upande wao pia. Suala linalobaki kuwa gumu ni je, kugawana vyeo kwa wanasiasa wa juu ndiko kunaleta umoja wa kitaifa kwa Wazanzibari?
Ubaguzi wa kusema huyu chotara, huyu mwarabu, huyu Mpemba, huyu wa Unguja, huyu wa Bara, nk; unaisha? Na ilikuwaje mashehe waliwekwa ndani wakati wa serikali ya umoja wa kitaifa? Ilisaidiaje na itasaidiaje walioteswa kipindi hiki? Kupindua matokeo hadi kufuta uchaguzi kulikujaje chini ya SUK!? Ilikuwaje aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais Maalim Seif hadi akaishia kutopeana mkono na aliyekuwa Rais Dkt Ali Shein, tena msibani?
Umoja wa kitaifa usiwe wa kugawana vyeo kwa wanasiasa wachache, bali uwe wa kuwaunganisha watu, kuondoa dhuluma, ufisadi, ubaguzi na kujaliana Wazanzibar wote. Usiwe wa kuwajali au kuwashabikia wasaka tonge na umaarufu wao pamoja na vyama vyao. Chama pekee cha kukijali na kukijenga iwe ni Zanzibar pekee, basi!