Wakati CCM inaundwa Kikwete ndio alikuwa amemaliza chuo kikuu miaka miwili kabla, na yeye alikuwa ni mtumishi wa ngazi za chini katika hicho chama; inashangaza kuona kuwa watu wazima waliohusika na uamzishwaji wa hiki chama leo hii wanaona ukoo wa kikwete wanakifanya chama kama vile no mali yao na kufanya kila wanalotaka bila ya watu kuwakemea!! Itakuwaje leo mtoto wa Rais ajifanye na yeye ni Rais wa nchi pia na watu wakakaa kimya wakati mali za nchi zinahujumiwa kwa jina la chama? Kuna umuhimu wa watu kuwa na ujasiri wa marehemu Rajab Diwani na Masudi Mtandika na kuhoji tabia ya mwenyekiti kukifanya chama mali ya ukoo wake!!