Mtatiro(CUF), Nape(CCM) na Erasto Tumbo(CDM) "LIVE" on MLIMANI TV Leo saa 2 usiku

mtutuma

Member
Jun 6, 2011
18
7
Nimejulishwa na Mliman TV kuwa hawa jamaa wataunguruma mida ya usiku wa leo LIVE juu ya muelekeo wa nchi, na kama sikosei Nape ataenda kueleza namna CCM ilivyoleta maendeleo ya kufa mtu, Sijui patakuwaje maana ake atakutana na vichwa. Ama ndi Gamba litavuliwa Live leo.
 
nina majonzi sababu leo eneo letu ni zamu ya kukata umeme so nitakosa uhondo huu. wanakata saa 12 hadi saa tano usiku.
 
Nimejulishwa na Mliman TV kuwa hawa jamaa wataunguruma mida ya usiku wa leo LIVE juu ya muelekeo wa nchi, na kama sikosei Nape ataenda kueleza namna CCM ilivyoleta maendeleo ya kufa mtu, Sijui patakuwaje maana ake atakutana na vichwa. Ama ndi Gamba litavuliwa Live leo.

Nape ni katibu wa itikadi na uenezi wa ccm

Tumbo ni katibu wa itikadi na uenezi wa chadema

Mtatiro ni Kaimu katibu mkuu wa cuf bara

Hivi cuf hawana katibu wa itikadi na uenezi hadi wampeleke mtatiro kila tukio?? ama wanae lakini tia maji tia maji mbele ya makatibu uenezi wa ccm na chadema?

anyway, nadhani mtanange utakuwa mzuri, ccm wameanza kampeni ya kuwalazimisha watanzania kuona mafanikio ya miaka 50 ya uhuru.
 
Nape ni katibu wa itikadi na uenezi wa ccmTumbo ni katibu wa itikadi na uenezi wa chademaMtatiro ni Kaimu katibu mkuu wa cuf baraHivi cuf hawana katibu wa itikadi na uenezi hadi wampeleke mtatiro kila tukio?? ama wanae lakini tia maji tia maji mbele ya makatibu uenezi wa ccm na chadema?anyway, nadhani mtanange utakuwa mzuri, ccm wameanza kampeni ya kuwalazimisha watanzania kuona mafanikio ya miaka 50 ya uhuru.
Mtatiro kama mtatiro ni jembe.
 
Mtatiro kama mtatiro ni jembe.

Hilo halina ubishi, mimi nilitaka kujuan kwa nini kila tukio kubwa wanampeleka mtatiro? kitengo cha itikadi na uenezi kiko wapi? kabla ya mabadiliko ya uongozi walau tulikuwa tunamuona yule dada mustafa akijitahidi kuiwakilisha cuf lakini tangu aenguliwe aliyekabidhiwa mikoba haonekani wala hajulikani.
Ama ndo kama zile za bashange, aliteuliwa kuwa naibu katibu mkuu lakini akawa haonbekani hadi mtatiro kampokonya nafasi~~
 
Nape ni katibu wa itikadi na uenezi wa ccm

Tumbo ni katibu wa itikadi na uenezi wa chadema

Mtatiro ni Kaimu katibu mkuu wa cuf bara

Hivi cuf hawana katibu wa itikadi na uenezi hadi wampeleke mtatiro kila tukio?? ama wanae lakini tia maji tia maji mbele ya makatibu uenezi wa ccm na chadema?

anyway, nadhani mtanange utakuwa mzuri, ccm wameanza kampeni ya kuwalazimisha watanzania kuona mafanikio ya miaka 50 ya uhuru.

Unachokosea ni kwamba wote ni watendaji katika vyama vyao, naibu katibu mkuu ni mtendaji na makatibu wa itikadi ni watendaji kwa hiyo mtatiro(Naibu katibu mkuu) na nape - katibu wa uenezi hawana tofauti kubwa sana, ambacho ni muhimu kukitizama ni kuwa wote bi vijana wenye uwezo mkubwa wa kujenga hoja na wana uwezo wa kushawishi mambo fulani.
 
Ikifika mahala Mtatiro naye ni kichwa Tanzania imeoza inatoa na funza.

Mtatiro unayemdharau huyu hapa;
Waziri wa mikopo UDSM - 2006-2007,
Waziri Mkuu UDSM - 2007-2008,
Katibu Mkuu wa vyuo vikuu Tanzania 2007 -2008,
Mkurugenzi wa haki za binadamu na sheria CUF - 2009 - 2010,
Kaimu katibu Mkuu CUF(bara) - Dec 2010 - May 2011,
Naibu Katibu Mkuu CUF(bara) - May 2011 - To date.
Wewe weka CV yako hapa tuone, unadhania mtu anaweza kupitia post zote hizo kwa kubahatisha?
Mtatiro ni kamanda wa kufa mtu labda wenye wivu ndo tunambania tu.
 
Hilo halina ubishi, mimi nilitaka kujuan kwa nini kila tukio kubwa wanampeleka mtatiro? kitengo cha itikadi na uenezi kiko wapi? kabla ya mabadiliko ya uongozi walau tulikuwa tunamuona yule dada mustafa akijitahidi kuiwakilisha cuf lakini tangu aenguliwe aliyekabidhiwa mikoba haonekani wala hajulikani.
Ama ndo kama zile za bashange, aliteuliwa kuwa naibu katibu mkuu lakini akawa haonbekani hadi mtatiro kampokonya nafasi~~

Kwa CUF kitengo hicho kinaitwa KURUGENZI YA HABARI,UENEZI NA HAKI ZA BINADAMU, inaongozwa na Mhe. Amina Mwidau(MB) - Viti maalum kutoka mkoa wa Tanga(M.A in Mass Communication). Kwa sasa yuko bungeni na kipindi kiko Dar kwa hiyo inahitaji upeleke mtu mwingine, na kwa sababu Nape ni mtu wa propaganda kali inahitaji apambane na watu wenye uelewa mkubwa thats why tumempeleka Mtatiro kwa kuamini uwezo wake.

Lakini katika programu mbalimbali za TV na REDIO tumekuwa tukiwapeleka watu tofauti, siku kadhaa zilizopita katika mjadawa wa asubuhi TBC alikwenda AMINA MWIDAU mwenyewe na mara nyingi sana tunawapeleka watu tofauti, Mtatiro ni mmoja wao tu na hatuna Ubaguzi.

Kwa sasa ASHURA Mustapha yuko busy na umaliziaji wa dissertation yake ya M.A na akikamilisha najua mtamuona akitumika kwa shughuli kama hizi.

Nadhani nimekujibu vizuri.
 
Mtatiro unayemdharau huyu hapa;
Waziri wa mikopo UDSM - 2006-2007,
Waziri Mkuu UDSM - 2007-2008,
Katibu Mkuu wa vyuo vikuu Tanzania 2007 -2008
,
Mkurugenzi wa haki za binadamu na sheria CUF - 2009 - 2010,
Kaimu katibu Mkuu CUF(bara) - Dec 2010 - May 2011,
Naibu Katibu Mkuu CUF(bara) - May 2011 - To date.
Wewe weka CV yako hapa tuone, unadhania mtu anaweza kupitia post zote hizo kwa kubahatisha?
Mtatiro ni kamanda wa kufa mtu labda wenye wivu ndo tunambania tu.

Wewe ongelea hizo vyeo vyenu vya CUF, vya UDSM usiongee kwa kuwa nilikuwa behind kumpa vyeo vyote hivyo, aliletwa ofisini kwangu na Daud Deo nimsaidie nikafanya hivyo kwa kuwapa fund na back up ya watu wangu wote wa UDSM, hakuwahi kushinda na anaogopa uchaguzi. Kwa vyeo vya CUF kama mwenyeketi ni Lipumba sishangai hata mkiokota mwehu akawa katibu mkuu.
 
Wewe ongelea hizo vyeo vyenu vya CUF, vya UDSM usiongee kwa kuwa nilikuwa behind kumpa vyeo vyote hivyo, aliletwa ofisini kwangu na Daud Deo nimsaidie nikafanya hivyo kwa kuwapa fund na back up ya watu wangu wote wa UDSM, hakuwahi kushinda na anaogopa uchaguzi. Kwa vyeo vya CUF kama mwenyeketi ni Lipumba sishangai hata mkiokota mwehu akawa katibu mkuu.

Kama ulimfund mwehu basi uwezo wako ni wa kutiliwa mashaka

Na inawezekana wewe ndo una matatizo hayo unayompachika kamanda mtatiro.
 
Wewe ongelea hizo vyeo vyenu vya CUF, vya UDSM usiongee kwa kuwa nilikuwa behind kumpa vyeo vyote hivyo, aliletwa ofisini kwangu na Daud Deo nimsaidie nikafanya hivyo kwa kuwapa fund na back up ya watu wangu wote wa UDSM, hakuwahi kushinda na anaogopa uchaguzi. Kwa vyeo vya CUF kama mwenyeketi ni Lipumba sishangai hata mkiokota mwehu akawa katibu mkuu.

UDSM unayoiongelea ni ipi? kila mtu alikuwa UDSM bradha,
Mtatiro ni jembe na watu wanamuamini, sema tu humu JF kuna baadhi ya watu kama wewe ambao wanataka watu fulanifulani tu ndio wapewe credit.

Mimi nimemfahamu mtatiro katika harakati zake na hata hizo enzi za DARUSO, alim_outnumber president magesa mwita hadi magesa akamvua uwaziri two weeks before another DARUSO election ambapo kwa vyovyote Mtatiro ndio alikuwa the next President.
Nakumbuka jamaa wa magamba waliingilia uchaguzi ule kwa kumtumia Ridhiwani na Kingunge na ndipo Mtatiro alitolewa ghafla katika screening na nakumbuka kitendo cha mtatiro kutolewa miongoni mwa wagombea kilileta kizazaa cha mgomo mkubwa ambao kabla haujaanza mtatairo aliwatuliza wanafunzi na akawaahidi serikali ijayo angekuwemo ndani na kuwa wasiwe na wasiwasi itaundwa serikali ya makamanda.

Na kwa taarifa yako katika historia ya DARUSO ule ndio ulikuwa uchaguzi mwepesi mno kwani wanafunzi wengi walisubiri kujua Mtatiro angempigia debe nani. Ilipoonekana Mtatiro anamnadi DEO tayari sehemu kubwa ya wanafunzi tukaamua kumchagua Deo na kila siku tulikuwa tunakutana Uwanja wa mpira kuchangishana kwa ajili ya kampeni hiyo.

Kwa hakika nakumbuka hakuna watu waliomjua vizuri DAUDI DEO kabla na kwa hakika DEO alipata urais wa DARUSO kwa sababu Mtatiro alismama upande wake na kwa wakati ule ingetokea Mtatiro akamuunga mkono MALIMA wa BED maana yake ni kuwa MALIMA angekuwa rais wa DARUSO bila kupinga.

Mimi nafahamu kuwa Mtatiro ana uwezo mkubwa mno na kwa vyovyote vile siyo mtu wa kumkejeli na kumdharau.
Naungana mkono na Marmoboy kuwa tuwekee CV yako hapa ya nyadhifa za kiuongozi ulizopitia. Haiwezekani mtu apitie posts muhimu namna hiyo za kiuongozi halafu unatudanganya hapa eti alipewa, eti alitumia pesa. Kama vipi tuwekee hapa CV ya magamba wenzio.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom