Mtatiro amkubali Slaa

Mtatiro amkubali Slaa

Tafuta gazeti la tanzania daima toleo la 03/1/2013 utaikuta hii habari.Sasa kama tanzania daima limekuwa la udaku, uhuru na mzalendo yataitwaje?
Nakuunga mkono kwa sababu niliangalia kipindi, jamaa kakuza hili suala kama habari za kwenye magazeti ya udaku.
 
rejea nyekundu= jibu-ni jibu ni ndio maana umoja ni nguvu kwa wao kufanya kazi kama timu wanajenga chma chenye nguvu na imara .bluu=jibu ni ndio chama chenye nguvu kinamtoa kiongozi imara wa kupeperusha bendera ya urais ambaye ni dr. slaa amaye kiukweli mi kama mimi nampenda na ktk hali ya kawaida ukiangalia bila malice utaona walio wengi wanampa sifa na nafasi japo chama kinaweza kuamua vinginevyo........sabababu za mimi kumpam urais moja ndiye mgombea pekee aliyepata kunivutia na mpaka leo napenda pia apeperushe bendera,pili ni mtu pekee inayesemekekana ni mpinzani wa kwanza kushinda urais tangu nchi ipate uhuru na kufanyiwa hila na hakudai kwa nguvu(busara) ,tatu hakurupuki na mtu mwenye uwezo wa kufanya maamuzi magumu........n.k
sina ubishi la ww kumpenda slaa, hapa kidogo ntaomba ufafanuzi ' waliowengi wanampa nafasi' napenda kujua ni wengi wapi? wana CDM , wapinzani kwa ujumla wao au wananchi waliowengi wa TANZANIA, unadhani chama kinaweza kuamua tofauti kwa mizengwe au demokrasia ambayo kwako ameshinda[waliowengi] kisha naomba kujua ninani , au ushahidi upi? uliokusadikisha uamini kuwa MH SLAA alishinda uchaguzi wa rais na kufanyiwa hila. naomba kujua wakati huo ww ulikuwa wapi? na nini ? msimamo wa CDM tuko wakati huo, mpaka leo hii juu ya dai hilo. mwisho naomba unishawishi / uwashawishi WATANZANIA wengine maamuzi gani? magumu aliyokwisha yafanya nje na ndani ya chama.
 
Julias: Simple logic,kama kweli unakubali sera za CDM na unamfagilia Katibu Mkuu wake ambaye ndiye liwalo na liwe atakuwa mgombea wa Urais 2015 sasa unaonaje dhana nzima ya kuunganisha nguvu ili tuunde serikali ya umoja wa kitaifa 2015?

Hili linawezekana endapo mwenyekiti wako atakubaliana na hilo kutogombea na badala yake kum-support mgombea wa CDM -Baada ya ushindi wa kishindo (ambao nina uhakika nao) serikali ya umoja wa kitaifa itaundwa na miaka 5 ya mwanzo Prof Lipumba atasaidiana sana na Rais aliyeko madarakani kujenga uchumi akiwa mshauri mkuu pale white House yetu.(magogoni)

Wenzetu wakenya hawana uadui wa milele, leo maadui kesho wanaugana kwa maslahi ya taifa lao. Tunachotaka sisi si chama gani kiongoze dola hapana, tunachopigania sisi ni kuiondoa serikali ya CCM madarakani na kuua mizizi yote ya ukandamizaji na undugu-naizesheni - ili tujipange upya as a nation!!

Umenipata Mkuu? si kumsifia tu DR. Slaa funguka kamanda wangu!!! muda unayoyoma huu kuelekea ukombozi wa kweli wa taifa letu.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Kwanza kabisa Karibu sana JF. Pili Acha upotoshaji mkuu,wengi tulifuatilia mdahalo ule, alichokisema Mtatiro ni kuwa watakuwa tayari kushirikiana na watu potential bila kujali vyama vyao kumtaja Dr Slaa ilikuwa ni mfano tu lakini hakusema watahakikisha wanamshirikisha Dr Slaa kwenye serikali ya CUF.
Wewe ndo haujamuelewa mleta mada,na yeye kasema hivyo hivyo kuwa mfano dr slaa..
that means dr slaa ni msafi na wengine mithili yake wote wanahitajika...
hata hivyo nadhani ni wazi kuwa cuf inaihitaji sana chadema kuliko vinginevyo...
cuf <<<<<<<chadema
so dr slaa cant be contained in cuf but opposite can work.
 
sina ubishi la ww kumpenda slaa, hapa kidogo ntaomba ufafanuzi ' waliowengi wanampa nafasi' napenda kujua ni wengi wapi? wana CDM , wapinzani kwa ujumla wao au wananchi waliowengi wa TANZANIA, unadhani chama kinaweza kuamua tofauti kwa mizengwe au demokrasia ambayo kwako ameshinda[waliowengi] kisha naomba kujua ninani , au ushahidi upi? uliokusadikisha uamini kuwa MH SLAA alishinda uchaguzi wa rais na kufanyiwa hila. naomba kujua wakati huo ww ulikuwa wapi? na nini ? msimamo wa CDM tuko wakati huo, mpaka leo hii juu ya dai hilo. mwisho naomba unishawishi / uwashawishi WATANZANIA wengine maamuzi gani? magumu aliyokwisha yafanya nje na ndani ya chama.

wangapi ni suala gumu kubainisha namba yao ila anatosha kusema wengi maana amekuwa gumzo sehemu yoyote ninapofika na kukuta hoja juu yake zaidi hata mkuu wa kaya na hata hapa najua hata wewe kuanza mjadala wa majibizano na mimi ni jibu tosha kwako kuwa huyu slaa ni gumzo japo waweza kataa kwa sababu uzijuazo wewe mwenyewe na huenda na ubishi wa kimazoea tu,pili si wapinzani tu wanaomkubali hata magamba wanamkubali(rejea kauli za samwel sita bukoba kuwa tishio ni dr,slaa) ipa mtatiro jana kawakilisha cuf kumkubali dr slaa wangu,viongozi wa dini (rejea kauli za padri mapunda mara kwa mara),mikusanyiko mikubwa ya watu anapokuwa anatembea poipote mikoani ni ishara tosha,tatu ushaidi wangu kuwa alishinda ni kushindwa kwa tume ya uchaguzi kutupa matokeo mpaka leo yenye mchanganuo wa kimajimbo mwisho siwezi kukwambia mimi nilikuwa wapi kwani si muhimuzaidi ya hayo......may be nzi ...over.....when FBI investigates FBI is your challenge
 
UJIRA WA MWIHA? NAMKUMBUKA MZEE WA NDIMI 2 a.k.a KIRUSI,NA YUKO WAPI SIKU HIZI? BADO MBUNGE WA MASWA?
 
wangapi ni suala gumu kubainisha namba yao ila anatosha kusema wengi maana amekuwa gumzo sehemu yoyote ninapofika na kukuta hoja juu yake zaidi hata mkuu wa kaya na hata hapa najua hata wewe kuanza mjadala wa majibizano na mimi ni jibu tosha kwako kuwa huyu slaa ni gumzo japo waweza kataa kwa sababu uzijuazo wewe mwenyewe na huenda na ubishi wa kimazoea tu,pili si wapinzani tu wanaomkubali hata magamba wanamkubali(rejea kauli za samwel sita bukoba kuwa tishio ni dr,slaa) ipa mtatiro jana kawakilisha cuf kumkubali dr slaa wangu,viongozi wa dini (rejea kauli za padri mapunda mara kwa mara),mikusanyiko mikubwa ya watu anapokuwa anatembea poipote mikoani ni ishara tosha,tatu ushaidi wangu kuwa alishinda ni kushindwa kwa tume ya uchaguzi kutupa matokeo mpaka leo yenye mchanganuo wa kimajimbo mwisho siwezi kukwambia mimi nilikuwa wapi kwani si muhimuzaidi ya hayo......may be nzi ...over.....when FBI investigates FBI is your challenge
naona unaniwekea mazingira ya kukubaliana nawe kwa nguvu, maana unalazimisha kuwa hata mimi natambua kuwa MH SLAA ni gumzo, labda nilete ubishi wa kimazoea. kwanza nakubali nabisha ili nielewe. na kutoa fursa pia kwa wengine kuelewa.ktk maelezo yako umewaelezea watu mashuhuri na viongozi wa jamii ambao wamekiri kuwa MH SLAA ni tishio, swali tishio la nini? na kwa sababu gani ? nakubaliana nawe kuwa mh, slaa popote anapokanyaga anavuta umati mkubwa ambao kwa imani inaonekana wanamuunga mkono.lkn hata CCM wanapopita nao umati unawaunga mkono kwa maana ya kujitokeza na hili limejidhihili ktk chaguzi ndogo zilizokwisha fanyika zinaonyesha ushindi kwa CDM/CCM lkn chama kilichoshindwa kinapata kura nyingi zenyekuonesha nacho kinawafuasi wengi ktk eneo hilo. KUTOTOLEWA matokeo kwa mchanganua wa majimbo yaani kwa kutofanyika hilo tu. takwimu zako zinampa ushindi MH SLAA kwanini ? takwimu hizo zisikuongoze kumpa MH KIKWETE au MH LIPUMBA? dhahiri jibu lako kwa kuwa una mapenzi naye. MWANZO ULIMTAMKA KUWA NI MTU WA MAAMUZI MAGUMU nimekuuliza maamuzi yapi? magumu aliyowahi kufanya ndani ya chama na nje hujajibu.MWISHO; AUGUSTINE LYATONGA MREMA alikuwa hashauliki kwa sababu tu ,alikuwa na mtaji wa wapiga kura 2,000,000 kwa ubishi na kutotaka ushauri walipepea wote, mh SLAA naye anao mtaji aulinde asirudie makosa ya MREMA.
 
Nilimsikia,na mh Mwigulu
akamwambia asiwasemehe wengine,akisemee cuf,namshauri dr Slaa nae atamke
kuwakubali cuf au baadhi ya viongozi wa cuf

Huyu Mwigulu N, niliambiwa akiwa chuoni alikuwaga mwana chadema. Lakini alipomaliza chuo akarubuniwa na mafisadi wa iramba. source udsm room mate wake.
 
Kwanza kabisa Karibu sana JF. Pili Acha upotoshaji mkuu,wengi tulifuatilia mdahalo ule, alichokisema Mtatiro ni kuwa watakuwa tayari kushirikiana na watu potential bila kujali vyama vyao kumtaja Dr Slaa ilikuwa ni mfano tu lakini hakusema watahakikisha wanamshirikisha Dr Slaa kwenye serikali ya CUF.

mkuu ITEGAMATWI utakuwa na mtindio wa ubongo, mbona unabishana mwenyewe??
hebu rudia kusoma vizuri post then usome na kioja chako!!!!
kweli magamba hamnazo
 
Nasema hivi dr slaa ni jembee na kiongoi mahirii kwa watz nashuruu mtatiroo kulijuaa hilooo na badoooo
 
Kwanza kabisa Karibu sana JF. Pili Acha upotoshaji mkuu,wengi tulifuatilia mdahalo ule, alichokisema Mtatiro ni kuwa watakuwa tayari kushirikiana na watu potential bila kujali vyama vyao kumtaja Dr Slaa ilikuwa ni mfano tu lakini hakusema watahakikisha wanamshirikisha Dr Slaa kwenye serikali ya CUF.

wewe utakuwa mwehu, sasa hapo kama alitoa mfani kwa nini asingemtolea JK ila akamtolea Dr Slaa. unapinga halafu unatoa mfano ule ule.
 
mkuu ITEGAMATWI utakuwa na mtindio wa ubongo, mbona unabishana mwenyewe??
hebu rudia kusoma vizuri post then usome na kioja chako!!!!
kweli magamba hamnazo


Hebu soma tena post ya mleta mada then usome na yangu halafu kimya kimya utaona kati yetu yupi ana mtindio wa ubongo!!Tena wewe inaonekana hata mwezi haujamaliza tangu uripoti milembe!! Nguchiro wewe.
 
Wewe ndo haujamuelewa mleta mada,na yeye kasema hivyo hivyo kuwa mfano dr slaa..
that means dr slaa ni msafi na wengine mithili yake wote wanahitajika...
hata hivyo nadhani ni wazi kuwa cuf inaihitaji sana chadema kuliko vinginevyo...
cuf <<<<<<<chadema
so dr slaa cant be contained in cuf but opposite can work.


Jamani sijui kwanini hamtaki kunielewa!!Sijakataa kuwa kwa mujibu wa mtatiro Dr Slaa siyo potential!Ninachopinga ni matumizi ya neno watahakikisha kuwa Dr Slaa anakuwa miongoni mwao! Mtatiro hajasema watahakikisha.
 
- kwani cuf ni wapinzani au tawi la ccm?

Le mutuz

Kweli nimeamini Le mutuz akili zako zina walakini, umekuwa ccm wa kwanza kutamka hili neno la CUF kuwa tawi la CCM. Kumbe ndo maana ukigombea CCM unashindwa, wanahisi wewe hauko sawa!!!!
 
Dr slaa yuko makini sana,watanzania tunampenda na tuna imani nae.
 
Back
Top Bottom