Zakamwamoba
Senior Member
- Jul 28, 2016
- 175
- 609
Picha ya Marehemu enzi za uhai wake
Simanzi na majonzi vimetawala kwa Watanzania waishio nchi China baada ya kuondokewa na Mtanzania mwenzao ndugu HAMIS RUHABAYE.
Hamis ambae alikuwa Mfanyabiashara katika mji wa Guanzhou kwa muda mrefu na alikuwa anaishi pamoja na familia yake amefariki Dunia leo Jumatano Januari 17,2018.
Kwa mujibu wa Taarifa kutoka kwa Bw. Abraham ( Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Wafanyabiashara wa Kitanzania wanaoshi China) Amesema Marehemu alifariki ghafla kutokana Matatizo ya Moyo.
Bw. Abraham amesema tayari wamekaa na wameafikiana kwamba Bajeti inayohitajika kwa ajili ya kusafirisha Mwili, Familia na Mizigo mbalimbali hadi Tanzania ni 20,000 USD.
Watanzania waliopo nchini humo kwa pamoja wameanza kuchangishana ili kupata kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya kufanikisha zoezi la usafirishaji.
MTILAH BLOG
http://www.mtilah.com/2018/01/mfanyabiashara-mtanzania-afariki-ghafla.html