Just Pray
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 2,142
- 4,779
Kupitia ukurasa wake kwenye mtandao wa Instagram mtangazaji wa kabumbu wa Azam Tv, na msemaji wa Timu ya Azam FC ametangaza nia yake ya kugombea ubunge wa jimbo la Mwanga mkoani Kilimanjaro.
==
MWANGA NI YETU, KAZI NA UTU TUNASONGA MBELE....
Salamu kwa Vijana wenzangu,
Huu ni wakati wa kusimama imara, kuchukua nafasi, na kuwa sehemu ya mabadiliko tunayoyataka kuyaona katika jamii zetu.
Maendeleo hayaji kwa kusubiri, yanajengwa na watu wenye maono, bidii, na moyo wa kujitolea. Na hakuna kikundi chenye nguvu, maarifa, na ari kubwa kama sisi vijana.
Tuna nguvu. Tuna uwezo. Tuna wajibu.
Tushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo ikiwemo suala la uongozi kuchora dira yetu wenyewe.
Kama si sisi, ni nani? Kama si sasa, ni lini?
NATANGAZA RASMI NIA YANGU THABITI YA KUOMBA RIDHAA YA CHAMA CHA MAPINDUZI CCM YA KUPEPERUSHA BENDERA YA CHAMA JIMBO LA MWANGA KILIMANJARO MKOA ΝΑ WILAYA NINAYOTOKA.
Tuungane kwa pamoja, tuamke, na tuijenge Tanzania mpya yenye maendeleo ya kweli yanayoanzia kwa vijana.
MWANGA NI YETU, KAZI NA UTU TUNASONGA MBELE.
==
MWANGA NI YETU, KAZI NA UTU TUNASONGA MBELE....
Salamu kwa Vijana wenzangu,
Huu ni wakati wa kusimama imara, kuchukua nafasi, na kuwa sehemu ya mabadiliko tunayoyataka kuyaona katika jamii zetu.
Maendeleo hayaji kwa kusubiri, yanajengwa na watu wenye maono, bidii, na moyo wa kujitolea. Na hakuna kikundi chenye nguvu, maarifa, na ari kubwa kama sisi vijana.
Tuna nguvu. Tuna uwezo. Tuna wajibu.
Tushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo ikiwemo suala la uongozi kuchora dira yetu wenyewe.
Kama si sisi, ni nani? Kama si sasa, ni lini?
NATANGAZA RASMI NIA YANGU THABITI YA KUOMBA RIDHAA YA CHAMA CHA MAPINDUZI CCM YA KUPEPERUSHA BENDERA YA CHAMA JIMBO LA MWANGA KILIMANJARO MKOA ΝΑ WILAYA NINAYOTOKA.
Tuungane kwa pamoja, tuamke, na tuijenge Tanzania mpya yenye maendeleo ya kweli yanayoanzia kwa vijana.
MWANGA NI YETU, KAZI NA UTU TUNASONGA MBELE.