GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,694
- 109,128
Halafu nikija kuwasema humu JF mnaanza kukasirika na hadi kuninunia wakati kumbe ukweli ni kwamba mnafanya makosa makubwa sana ya Kitaalauma na Kiueledi hasa katika suala zima la Utangazaji na niwaahidi tu kuwa sitowanyamazia hadi pale mtakapobadilika.
Leo asubuhi kuanzia Saa 12 na nusu hadi Saa 1 na nusu hivi TBC1 walikuwa wakifanya mahojiano na Paul Makonda ( nachelea kumwita Mkuu wa Mkoa kwakuwa bado hajatupa uthibitisho kamili wa Cheti chake ) na Mtangazaji aliyepewa jukumu la kumhoji alikuwa anaitwa Khalid Gangana.
Binafsi kabisa leo nilitegemea kuona very hot and critical interview kutoka TBC1 na badala yake niliishia tu Kukasirishwa na aina ya Kipuuzi ya jinsi Mtangazaji wa TBC1 Khalid Gangana alivyokuwa anamhoji Paul Makonda.
Hivi Mtangazaji mahiri kweli wa TBC1 anaweza kumhoji Mtu ambaye tayari nchi na pengine hata dunia kama siyo hata Mbinguni wanajua kuwa ana matatizo makubwa na matendo ya ajabu ajabu yanayotia doa utendaji wake maswali kama haya yafuatayo?
Mtangazaji huyu Khalid Gangana hakuishia tu hapo kukubali rasmi kujitolea Kwake kulishwa matango pori ( Kudanganywa ) pale ambapo tena Paul Makonda alimwambia kuwa Kidunia Tanzania ni nchi ya Tisa ( 9 ) inayokuwa Kiuchumi wakati kwa data za hivi karibuni ni nchi ya Angola ndiyo inayokuwa kwa Kasi sana Kiuchumi na Tanzania hata katika 20 bado hatupo.
Kitaaluma Mwandishi wa Habari hatakiwi Kudanganywa ( kulishwa tango pori ) na Source wake na inaruhusiwa pia kama akiona Source wake anakengeuka / anakosea basi anatakiwa kufanya kupinga na kukubali Watazamaji wake walishwe Sumu ya Uwongo uliotukuka.
Na kilichonikera zaidi huyu Mtangazaji Khalid Gangana Yeye muda wote wa Interview yake na Paul Makonda alikuwa akicheka cheka bila hata sababu ya msingi na niseme tu ukweli huwa natizama sana Interviews mbalimbali za Waandishi Nguli kabisa wa BBC, CNN na SKYNEWS na sijawahi kuona wakiwa na Characteristics kama za Mtangazaji Khalid Gangana.
Ningekuwa Mimi ndiyo Mtangazaji Khalid Gangana leo ningemuuliza Paul Makonda maswali haya yafuatayo:
Leo asubuhi kuanzia Saa 12 na nusu hadi Saa 1 na nusu hivi TBC1 walikuwa wakifanya mahojiano na Paul Makonda ( nachelea kumwita Mkuu wa Mkoa kwakuwa bado hajatupa uthibitisho kamili wa Cheti chake ) na Mtangazaji aliyepewa jukumu la kumhoji alikuwa anaitwa Khalid Gangana.
Binafsi kabisa leo nilitegemea kuona very hot and critical interview kutoka TBC1 na badala yake niliishia tu Kukasirishwa na aina ya Kipuuzi ya jinsi Mtangazaji wa TBC1 Khalid Gangana alivyokuwa anamhoji Paul Makonda.
Hivi Mtangazaji mahiri kweli wa TBC1 anaweza kumhoji Mtu ambaye tayari nchi na pengine hata dunia kama siyo hata Mbinguni wanajua kuwa ana matatizo makubwa na matendo ya ajabu ajabu yanayotia doa utendaji wake maswali kama haya yafuatayo?
- Paul Makonda hivi huwa unalala Saa ngapi?
- Naona mwili wako umejengeka sana Kimazoezi.
- Nasikia unapenda mno mchezo wa Ndondi je ni kweli?
Mtangazaji huyu Khalid Gangana hakuishia tu hapo kukubali rasmi kujitolea Kwake kulishwa matango pori ( Kudanganywa ) pale ambapo tena Paul Makonda alimwambia kuwa Kidunia Tanzania ni nchi ya Tisa ( 9 ) inayokuwa Kiuchumi wakati kwa data za hivi karibuni ni nchi ya Angola ndiyo inayokuwa kwa Kasi sana Kiuchumi na Tanzania hata katika 20 bado hatupo.
Kitaaluma Mwandishi wa Habari hatakiwi Kudanganywa ( kulishwa tango pori ) na Source wake na inaruhusiwa pia kama akiona Source wake anakengeuka / anakosea basi anatakiwa kufanya kupinga na kukubali Watazamaji wake walishwe Sumu ya Uwongo uliotukuka.
Na kilichonikera zaidi huyu Mtangazaji Khalid Gangana Yeye muda wote wa Interview yake na Paul Makonda alikuwa akicheka cheka bila hata sababu ya msingi na niseme tu ukweli huwa natizama sana Interviews mbalimbali za Waandishi Nguli kabisa wa BBC, CNN na SKYNEWS na sijawahi kuona wakiwa na Characteristics kama za Mtangazaji Khalid Gangana.
Ningekuwa Mimi ndiyo Mtangazaji Khalid Gangana leo ningemuuliza Paul Makonda maswali haya yafuatayo:
- Ni kwanini hutulii Mkoani Kwako na muda wote unazunguka zunguka tu Mikoani?
- Je unazikumbuka ahadi zako ulizozitoa kwa Mkoa? Je kuna ambayo imeshafanikiwa?
- Nini kinakufanya usimalize huu Utata wako wa Cheti Feki?
- Mbona mwanzoni ulikuwa hutujali TBC na ulikuwa karibu sana na Clouds Tv na Radio?
- Je ile kamata kamata yako ya Dawa za Kulevya unaona imesaidia kumaliza kama siyo kupunguza tatizo au ndiyo umesaidia kuleta Ubunifu wa matumizi na uingizwaji wa dawa za Kulevya nchini?
- Je unadhani nafasi hii uliyonayo iliwahishwa Kwako au labda bado ulipashwa kubakia pale ulipokuwa ili uendelee kujifunza zaidi masuala ya Uongozi na Utawala?
- Kila mara unasikika ukipenda kulitaja mno jina la Mungu je Ndugu Paul Makonda unadhani matendo yako unayoyafanya kwa Wenzako au Wana Dar es Salaam au Watanzania yanamfurahisha Mungu na kwamba pengine unavyomtaja na Yeye huko alipo anafurahi?