Mtandao wa tiGO upo slow mpaka unaboa

Mtandao wa tiGO upo slow mpaka unaboa

mtandao unaboa sasa wa tigo bira kuwachana nao kama mie maisha yangu yotee ilikuwa nautumiya nakusifiya sasa hivi nimesaliti mwenyewe
 
Halotel nao saiz wamekua jipu, wameshazoea mazingira
 
Dah,mtandao wa tiGO kwenye internet ni wa kipuuzi,unakosesha raha baadala ya mtu ku-enjoy,page ina-load weeeeeee.....!!!! mpaka inakata yenyewe,ukinunua bando linaisha ukiwa umefanya machache katika mengi uliyokusudia.
Kwanza tiGO inamaliza chaji ya simu haraka kwa nguvu nyingi inayotumia bila mafanikio.Ukitumia 2G ili uokoe chaji ni shida,ukitumia 3G ili u-download speed yake ni kichefuchefu.
Wahudumu wake washamba,vitu vingine vinavyohusiana na mtandano wao ukiwauliza hawajui.
Voda na ninyi mshaanza kuwa kama tiGO,shauri yenu,mtahamwa,watu hatuangalii majina,tunaangalia ubora.
Hapa kilichobaki ni kuhamia halotel mazima,halotel ndiyo jembe la uhakika,mi' mwenyewe nawakubali.
kuna watu bado wanatumia internet ya tigo?
 
Mimi nikiendaga dukani huwa sisemi naomba vocha ya tigo, huwa nasema "nipe vocha ya ule mtandao wa magumashi" muuzaji aulizi mtandao gani ananipa tigo nasepa.
 
mm nipo Dodoma hawa Tigo wapo safi sana na ni faster kwa internet, Whatsapp, Imo, Mabdro nk
Halotel kuna kipindi ukiitumia hata kwenye simu km sio Line yake ina-block sembuse internet
Bado Dodoma hutudanganyi kwa Tigo hata 3G ni faster
Ukisikia mawakala wa tiGO ndiyo hawa.
Zao kutetea vibovu tu ili wauze,tiGO haiwezi kutia mguu kwa halotel hata siku moja.
Mi' mwenyewe nimeshatumia sana hii mitandao yote miwili,halotel 2G browsing speed ni sawa sawa na tiGO 3G browsing speed.
 
Nimecheka sana "kwanza tiGO inamaliza chaji ya simu haraka kwa nguvu nyingi inayotumia bila mafanikio"
 
Back
Top Bottom