Wakuu,
Kuna taarifa kuwa mtambo mwingine wa kuzalisha umeme wa kampuni ya Songas wenye uwezo wa kufua umeme kiasi cha 20MW upo down tangu asubuhi hii. Sababu za kuzimwa mtambo huo bado hazijapatikana. Hii inapelekea kampuni hiyo kutozalisha jumla ya 60MW ukijumlisha na ule mtambo wa 40MW ambao ulipata ajali ya moto wiki iliyopita na ambao hadi sasa bado upo kwenye matengenezo.
Vilevile kuna taarifa kuwa mtambo wa kuzalisha umeme wa kampuni ya Dowans wenye uwezo wa kuzalisha 40MW ambao uliwashwa kinyemela mwanzoni mwa juma tayari umeshazimwa baada ya wananchi kugundua mtambo huo kuwashwa kinyemela.
Kuna hatari makali ya mgawo wa umeme yakaongezeka.
Kuna taarifa kuwa mtambo mwingine wa kuzalisha umeme wa kampuni ya Songas wenye uwezo wa kufua umeme kiasi cha 20MW upo down tangu asubuhi hii. Sababu za kuzimwa mtambo huo bado hazijapatikana. Hii inapelekea kampuni hiyo kutozalisha jumla ya 60MW ukijumlisha na ule mtambo wa 40MW ambao ulipata ajali ya moto wiki iliyopita na ambao hadi sasa bado upo kwenye matengenezo.
Vilevile kuna taarifa kuwa mtambo wa kuzalisha umeme wa kampuni ya Dowans wenye uwezo wa kuzalisha 40MW ambao uliwashwa kinyemela mwanzoni mwa juma tayari umeshazimwa baada ya wananchi kugundua mtambo huo kuwashwa kinyemela.
Kuna hatari makali ya mgawo wa umeme yakaongezeka.