RUSTEM PASHA
JF-Expert Member
- Jan 26, 2016
- 4,734
- 11,462
Mkuu kwahiyo kutoka na GPA kubwa ndio ubovu wa elimu?.St. Joseph ujanjaujanja mwingi sana, biashara zaidi kuliko elimu bora. Watu wanaenda pale wamefeli wanatoka na GPA ya 4.9 hadi 3.5, mbaya zaidi graduate wake pamoja na kuwa na ufaulu mkubwa kichwani hawana kitu yaani ni mizigo makazini. Ni wachache sana wenye uwezo
Kwa nini hujiuliza kwa nini st Joseph kila kipindi wanaita majina kwa mwanafunzi alieoko darasani,na asipofikisha wastani wa mahudhulio unaotakiwa hafanyi UE?.
Kwa nini hujiulizi kwa nini wanafany CAT zaidi ya mbili,Modal halafu ndio UE.
Kwa nini hujiulizi kwa nini wanafanya assignment kumi wakati vyuo vingine wanafanya mbili?.
Kwa nini hujiukizi time table yao kila mwanafunzi anapewa mwanzo wa semister wakati vyuo vingine lecturer wanakurupuana bila taifa?.
Kwa nini hujiulizi mwanafunzi anapochelewa harusiwi kuingia darasani mpaka kipindi kiishe?.
Kwa nini hujiulizi darasa lao moja halizidi wanafunzi 80 wakati vyuo vingine wanafundisha wanafunzi zaidi ya 500 kipindi kimoja?.
All in all ufahamu wa vitu upo kwenye juhudi za mwanafunzi husika na sio chuo husika.