MSIMAMO WANGU
1. Changu ni changu, cha mume/mpenzi wangu tunashea.
2. Mwanaume bahili akae mbali na mimi.
3. Sina huruma na pesa ya mwanaume, labda atakaekuwa mume wangu wa ndoa.
4. Ntafanya majukumu yote kama mpenzi/mke wake, lakini when it comes to my money asahau, imeandikwa "mwanamke atazaa kwa uchungu na mwanaume atakula kwa jasho" so let him provide.
5. Ni marufuku mambo ya joints a/c eti mmoja wetu anaweza kutoa pesa pasipo saini ya mwingine sitaki.
6. Pesa zangu ni zangu ata password cmpi, bora nimpe Mama angu ata nikifa ajifutie nazo machozi.
7. Hata kama nina pesa kuliko yeye, mwanaume ni lazima awajibike, sio pesa ake awanufaishe wengine, maana kuna wanaume ndani wabahili ila nje wanahonga balaa.
8. Nyumba tutasaidiana kujenga, na itakuwa na jina langu na lake, au kama tutakuwa na watoto nao tutawaweka humo.
9. Ni marufuku ndugu wa mume kujihusisha na mali zetu, narudia tena ni marufuku ndugu wa mume kujisogeza karibu na mali zangu mm na mume wangu! Hizi haziwahusu kabisa tena mkae mbali.
NIMEMALIZA
sawasawa,, huu ni msimamo wangu mimi kama mmeo.
1. familia ni jukumu langu, nitawajibika mimi pekee na kuhakikisha mnaishi maisha basic, hamna mbwembwe.
2. sina haja ya joint account na wewe, nitakupa pesa kulingana na mahitaji and not otherwise. nataka kila senti itakayotumika iwe documented,,risiti will be highly appreciated.
3. ni marufuku ndugu zako kuhamia kwangu,, na kama watakuja kutembea hawaruhusiwi kulala zaidi ya siku moja. pia aje mmoja mmoja at a time, not otherwise.
3. huruhusiwi kwenda kwenu kutembea, unless wazazi ama ndugu zako waandike barua maalum ya maombi na wakutumie nauli.
4. sihitaji kusaidiana nawewe kujenga nyumba,, niachie hilo jukumu. nitajenga mwenyewe na kuandika jina langu, lako halina haja.
5. jukumu langu na familia yangu tu (wewe na watoto), matatizo ya ndugu zako hayanihusu. ndugu zako ni mzigo wako, huruhusiwi hata kuniomba ushauri.
nadhani tutaenda sawa, wako mmeo!!