Msimamo wangu

Msimamo wangu

Atoto

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2013
Posts
89,332
Reaction score
176,126
MSIMAMO WANGU

1. Changu ni changu, cha mume/mpenzi wangu tunashea, kifupi chake ni chetu.

2. Mwanaume bahili akae mbali na mimi, unless huo ubahili anaufanya kwenye mambo mengine ili amake more money ila sio kwangu. Tuzitumie zituzoee.

3. Sina huruma na pesa ya mwanaume, labda atakaekuwa mume wangu wa ndoa, ila hata yeye asijisahau sana nitakuwa na huruma nazo tu kwavile ni zetu. Akileta ng'e ng'e ng'ee nazo sizihurumii.

4. Ntafanya majukumu yote kama mpenzi/mke wake, lakini when it comes to my money asahau, imeandikwa "mwanamke atazaa kwa uchungu na mwanaume atakula kwa jasho" so let him provide.

5. Ni marufuku mambo ya joint a/c eti mmoja wetu anaweza kutoa pesa pasipo saini ya mwingine sitaki. Na hiyo accout ni yeye ndio atakuwa anaweka pesa tu.

6. Pesa zangu ni zangu ata password simpi, bora nimpe Mama yangu ata nikifa ajifutie nazo machozi. Tena akileta za kuulizia mshahara wangu naacha kazi ili tutumie zake vizuri.

7. Hata kama nina pesa kuliko yeye, mwanaume ni lazima awajibike, sio pesa yake awanufaishe wengine, maana kuna wanaume ndani wabahili ila nje wanahonga balaa.

8. Nyumba tutasaidiana kujenga, na itakuwa na jina langu au kama tutakuwa na watoto nao tutawaweka humo. Kaka tayari unayo/unazo basi uhakikishe zinakuwa na majina ya watoto pindi tutakapowapata.

9. Ni marufuku ndugu wa mume kujihusisha na mali zetu, narudia tena ni marufuku ndugu wa mume kujisogeza karibu na mali zangu mm na mume wangu! Hizi haziwahusu kabisa tena mkae mbali.

10. Nikitangulia mbele za haki kabla yako ole wako uoe mwanamke mwingine, nitakutokea ndotoni hadi ujute. Hata kifo jakitutenganishi.


NIMEMALIZA
 
Kabla sijachangia ningependa kujuwa umri wako kwanza halafu nenda kasome kuna thread humu ya mapenzi na umri ndio tutaelewana.

Maana yake tusije kujadili mambo ya pesa hapa kumbe hujawahi hata kumiliki 1 million yako mwenyewe wakati humu kuna watu millioni kwao ni buku tu.
 
Subir uletewe shetani mmoja kutoka kwa gabriel ndo atakuwa na hayo unayoyataka
 
Mume wako akitengwa na ndugu zake,utamhamishia kwenu?,hta ww kuna mambo ya msing na ndg zko mume hatopaswa kuyawekea msimamo,coz yanareflect ya moja kwa moja kat yko ww na familia ya kwenu.
 
Kabla sijachangia ningependa kujuwa umri wako kwanza halafu nenda kasome kuna thread humu ya mapenzi na umri ndio tutaelewana.

Maana yake tusije kujadili mambo ya pesa hapa kumbe hujawahi hata kumiliki 1 million yako mwenyewe wakati humu kuna watu millioni kwao ni buku tu.

haina mahusiano kabisaaa, changu changu, chake chetu
 
Back
Top Bottom