Msigwa: Serikali za Tanzania na Qatar zilipanga dili kuiba wanyama nchini

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,555
35,880
Mchungaji Msigwa Peter ambaye ni mbunge wa Iringa mjini (Chadema) na waziri kivuli wa maliasili na utalii ameshusha tuhuma nzito baada ya kuzihusisha serikali za juu za Tanzania na Qatar na ujangili unaoendelea chini, imefahamika.

Hayo aliyaeleza jana kujibu swali la kutoroshwa twiga wawili wakiwa hai kwenye uwanja wa ndege wa KIA.

Akiongea kwa kujiamini alipokuwa akihojiwa jana kwenye kipindi cha dakika 45 kinachorushwa na kituo cha ITV, mchungaji Msigwa alidai hayo huku akitolea ufafanuzi swala la uchunguzi wa sakata hilo lililokwamishwa kwa makusudi na serikali ya Qatar.

Katika maelezo ya balozi wa Qatar nchini ambayo yalinukuliwa na mchungaji Msigwa, balozi huyo alitajwa kuizuia viza ambayo ilikuwa itolewe kwa jopo la wachunguzi kutoka Tanzania ili waingie nchini Qatar kuchunguza sakata hilo.

"Mimi siwezi kutoa viza kwenye jambo hili wakati hawa wanyama tumeuziwa na serikali ya Tanzania, sasa tunataka kuchunguza nini tena? Hii ni biashara baina yetu na serikali ya Tanzania" alisema balozi huyo.

Katika sakata hilo mchungaji Msigwa alidai kuwa biashara hiyo ya wanyama kati ya serikali za Tanzania na Qatar ni ya muda mrefu na inafahamika vyema na serikali zote mbili.

Aidha alisema kuwa watanzania wasahau fikra za kutoroshwa kwa wanyama kwani hakuna kitu kama hicho bali ni biashara iliyohalalishwa na viongozi wa juu wa serikali ya Tanzania.
 
sasa serikali ni wananchi, unaposeama dili lilifanywa na serikali ina maana umma ulishirikishwa kupitia bunge?
 
Hii itakuwa JK ana % yake hapo kwenye hiyo zoo ya Qatar.
Waafrika aliyetuloga kafa
 
Siku zote wanaoangusha serikali ni watendaji wenyewe wa serikali. Maana wanyama hao wanaposafirishwa kwenda hko hawaendi kuchinjwa bali wanawekwa katika zoo za maonyesho na watu huenda kuwatazama kwa viingilio.

Sasa hebu tujiulize, kila siku wizara yetu ya maliasili imekuwa ikihangaika kutangaza utalii ili wagen waje kwa wingi.

Sasa madhala ambayo tutayapata kwa kuruhusu wanyama wetu kwenda kuwekwa kwenye zoo za huko moja wapo kwanza ni kupunguza idadi ya watalii kutoka nchi husika ambao walikuwa waje katika mbuga zetu, maana kama ni twiga si wanae hapo katika zoo na vile vile simba, chui na kila mnyama wanae mhitaji.sasa waje kuangalia nini hku wakati hadi faru wanae hko?

Yani huwa nikifikiria hawa viongozi wetu wanaoongozwa na tamaa badala ya maono nasikitika sana.
 
Aaaaargh huyu jamaa bhana.......kuitwa anazurura tu na waziri husika halafu hapa anatapika nini!!!!?????
 
Jamani hivi kweli mpaka Mch Msigwa aseme ndiyo muamini kwamna kuilkuwa na dili kati ya viongozi wa juu wa SMT na serikali ya Qatar kuiba wanyamapori hai.

Watanzania mna bore stiff! Hivi kweli mna IQ kidogo hivyo kiasi kwamba you can't put two and two together!

Hata kama Tanzania ni Banana Republic, ulishawahi kuona/kusikia wapi ndege ya KIJESHI ya nchi nyingine ikaingia nchini, bila Chief of Defence Force kujua, bila Commander in Chief of the Armed Forces kujua. Ikachukua wanyamapori hai wakubwa kama Twiga na kadhalika bila mamlaka nilizotaja hapo juu kujua!

Baadaye dege hilo la kijeshi likapaa likaondoka zake, bila rada zetu, tena tulizonunua kwa bei mbaya kuliona, lika vanish kwenye anga ya Tanzania hadi kwao Qatar.

Mpaka hapo bado the bell doesn't ring anything to you!

Eti mpaka Msigwa aseme Dk 45 ITV ndiyo hiyo miwani ya mbao inawandondoka?! Kweli watanzania mna BORE STIFF, kwa kujifanya hamnazo kichwani wakati mimi ninajua mnazo, ila kwa makusudi mmegoma kuzitumia. Poor Tanzanians
 
Huyu naye kihoro cha jimboni kwake , nasikia amekaliwa vibaya.
Bila kujali kama wana Iringa watamchagua Msigwa au laa, naomba kujua kutoka kwako cause nina hakika we upo makao makuu ya chama, serikali ilifanya biashara hiyo na Qatar au laa!? Jenga tabia ya kujikita kwenye maada husika badala ya kubadiri badiri topic.
 
Jamani hivi kweli mpaka Mch Msigwa aseme ndiyo muamini kwamna kuilkuwa na dili kati ya viongozi wa juu wa SMT na serikali ya Qatar kuiba wanyamapori hai.

Watanzania mna bore stiff! Hivi kweli mna IQ kidogo hivyo kiasi kwamba you can't put two and two together!

Hata kama Tanzania ni Banana Republic, ulishawahi kuona/kusikia wapi ndege ya KIJESHI ya nchi nyingine ikaingia nchini, bila Chief of Defence Force kujua, bila Command in Chief of the Armed Forces kujua. Ikachukua wanyamapori hai wakubwa kama Twiga na kadhalika bila mamlaka nilizotaja hapo juu kujua!

Baadaye dege hilo la kijeshi likapaa likaondoka zake, bila rada zetu, tena tulizonunua kwa bei mbaya kuliona, lika vanish kwenye anga ya Tanzania hadi kwao Qatar.

Mpaka hapo bado the bell doesn't ring anything to you!

Eti mpaka Msigwa aseme Dk 45 ITV ndiyo hiyo miwani ya mbao inawandondoka?! Kweli watanzania mna BORE STIFF, kwa kujifanya hamnazo kichwani wakati mimi ninajua mnazo, ila kwa makusudi mmegoma kuzitumia. Poor Tanzanians
Hakuna cha maana hapo msigwa anahangaika kama mpita njia aliyekuta njia imefungwa ndiyo maana hata hajitambui hata kwenye jimbo hajafanya cha maana hata kimoja.
 
Huyu naye kihoro cha jimboni kwake , nasikia amekaliwa vibaya.

Kwani uongo yaani nchi ndege ya jeshi inaingia na kutua na kuondoka na twiga wazima halafu viongozi wenu waliopo chini ya ccm wapo tu hawaelewi unajua nyie machalii mnatia hasira sana haya na meno ya tembo mliowapa wachina au jeshi lenu lilikuwa likizo likipambana na magaidi kule Amboni namtafuta mwandishi mzuuri anitungie kitabu manake Tanzania kuna maajabu mengi sana.
 
Hakuna cha maana hapo msigwa anahangaika kama mpita njia aliyekuta njia imefungwa ndiyo maana hata hajitambui hata kwenye jimbo hajafanya cha maana hata kimoja.

Majibu kama haya tuimeisha yazoea, hata mawaziri na wabunge wa ccm huwa wanayatoa. Hapa unajidai kukashifu ili kumfurahisha bwana 'ako, lakini pembeni unaning'unika. Utumwa huu mpaka lini?
 
Hoja yenyewe ya kilevi kwani kunakitu cha maana hapo hata kimoja?

Hivi unajua hata Twiga ni nini au unamuonaga kwenye picha tu?
Sidhani kama unajua hata ana faida gani kwako zaidi ya kusema 'nalichukiaga hili limdudu lireefuu'
 
Huyu naye aache kutubabaisha

atueleze msimamo wa kambi ya upinzani juu ya mgogoro wa Kenya

Hivi pesa zote walizonazo Qatar wana shida ya kuiba wanyama? ninavyoeelewa wale wanawanunua tuu hao mbilikimo wenu. Sote tunajua tatizo sio hawa wageni tatizo liko kwetu

tuwe wakweli
 
Msigwa pia alisema kama serikali haikufanya biashara hii haramu na Qatar, iweje ile tume iliyoundwa kwenda Qatar kuchunguza ilinyimwa visa kwenda Qatar ?
 
Back
Top Bottom