Msichana huyu asaidiweje?

Eeka Mangi

JF-Expert Member
Jul 27, 2008
3,173
481
Naam wapendwa,,, baada ya kalikizo kangu ka machungu nimerejea rasmi katika kijiji changu,,,, Moshi. Siku iliyofuta tu napata sms toka kwa mtu nisiyemfahamu anaomba kuniona,,, nilisita kidogo lakini nikasema sina budi kumwona. Anafika ofisini kwangu mida ya saa 5 asubuhi. Ni binti mdogo wa miaka kama 18 au 19 hivi. Ananisalimu anajitambulisha kisha ananielezea shida yake.
Binti huyu yupo kidato cha sita MUKONO HIGH SCHOOL UGANDA. Alipelekwa huko na mama yake na kwa sasa ameshindwa kurejea shule kwa kuwa mama yake ni mgonjwa na hivyo hawezi kuendelea na shule maana anatakiwa alipe ada ya takribani dola 400. Hivyo ananiomba nimsaidie. Namuuliza alipataje jina na namba yangu ya simu,,, anajibu kuwa aliwahi kunisikia katika kipindi fulani cha redio kuhusu masuala ya elimu. Well,,, ni kweli niliwahi kuchukua vijana ambao niliwasaidia na kwa sasa wengi wao ama wako vyuoni ama wamemaliza kidato cha nne na wanaedelea form 5. Nilikuwa na wadhamini fulani huko nyuma waliokuwa wananisaidia kuwalipia,,, lakini kwa sasa hawa waliobakia (ninao watoto 4 ninaowasaidia) ninajinyima na kutoa fungu mfukoni mwangu. Sina msaada wo wote kwa sasa.
Ombi la kwenu wana JF, ni taasisi gani ambayo naweza kuwasiliana nayo ili imsaidie huyu binti. Kwangu anaonekana kama ana kiu ya elimu. Na hata kama sio lazima arudi Uganda basi asidiweje ili atimize hiyo kiu yake.
Tushauriane na tuone tutamsaidiaje.
Nwatakia weekend njema
 
Kwanza una uhakika gani kwamba huyo binti siyo katika matapeli wa mjini? Siku hizi wapo wengi wenye stori kama hizo ndugu yangu, unakumbuka ya Taasisi ya WAMA hivi karibuni?

Sio vibaya kumtafutia msaada ikiwa kweli ana shida. Anaweza kusaidiwa kwa kusoma hapa hapa na sio lazima Uganda. Vile vile ni vyema akakupatia address ya huko shuleni kwao ukahakikisha kwamba ni kweli alikuwa mwanafunzi. Jaribu kucheki by email, website au hata kwa njia nyengine.

All the best na hongera kwa kuwa na moyo wa kusaidia vijana.
 
Kwanza una uhakika gani kwamba huyo binti siyo katika matapeli wa mjini? Siku hizi wapo wengi wenye stori kama hizo ndugu yangu, unakumbuka ya Taasisi ya WAMA hivi karibuni?

Sio vibaya kumtafutia msaada ikiwa kweli ana shida. Anaweza kusaidiwa kwa kusoma hapa hapa na sio lazima Uganda. Vile vile ni vyema akakupatia address ya huko shuleni kwao ukahakikisha kwamba ni kweli alikuwa mwanafunzi. Jaribu kucheki by email, website au hata kwa njia nyengine.

All the best na hongera kwa kuwa na moyo wa kusaidia vijana.

Asante kwa mchango wako. JF is The home of great thinkers ndio maana nikaja hapa. Nitajaribu kufuatilia kwa karibu na nitawajuza zaidi kama ni kweli alikuwa akisoma huko ama vipi. Wazo la kusaidiwa hapahapa nyumbani ni zuri zaidi. Anaweza akasoma hapahapa sio lazima Uganda.
 
Back
Top Bottom