Mshahara wa Rais, Waziri Mkuu, Mawaziri na Watendaji Wakuu Serikalini

Wanafanya siri kwa sababu itakuwa aibu sana mishahara yao itakapolinganshwa mshahara wa kima cha chini wa Mtanzania!
 
Transparency, freedom of expression, the right to get information, the right to question etc are crimes in this paradise-country; an island of peace where the oppressed find refuge and the (indegenous) suffer more than the refugees. If you question expect to be Kolimbered, ulimbokered, kubenaired, kibandered and the like. The good thing is we are so humble to the extent of been tickled into our eyes. The sukuma have no difficult times because to them every situation good or bad they say 'NDUHU TABU' (this means no problem), so are all tanzania.....Lets enjoy our problems
 
acha ungese dogo

Unajua huyo dogo bado hajaanza kulipa kodi na kwa hiyo hajui kwa nini sisi walipa kodi tuna machungu na kutaka kujua ni kodi yetu kiasi gani hao wakuu wa nchi wanaitumia na je inaendana na hali halsi ya maisha ya watanzania ambao wengi wao ni maskini wa kutupwa wanaoishi chini ya dola 1 kwa siku???
 
kwa kuzingatia hali yetu ya uchumi wetu na uroho wa viongozi wetu nadhani kama rais wetu akilipwa mshara na marupurupu yanayofikia 20 milioni TSH angalau itakuwa inaelezeka zaidi ya mapato ya shilingi 20 milioni kwa mwezi si kwamba tu ni ufisadi,haielezeki bali pia ni ujinga maana kuwa tajiri kwa kuwaibia maskini ni kiwango kikubwa kabisa cha ujinga yaani ni zaidi ya kuzungusha NECTA
 
Kwani hakuna mzalendo au wote wameoza hakuna hata mmoja. Nina walenga wahasibu wanaoandika hizo hundi si watuwekee hapa.
 
Mishahara yao ni siri bali pensheni ni 80% ya mishahara ya wenzio walio kazini kwa sasa. Kama wanaosema kuwa mishahara yao ni zaidi ya mshahara wa marekani ni sawa, basi hata wastaafu wanapata pesa kama pensheni ambazo ni za kutisha. Wakati haya yakifanyika wastaafu waliokuwa watumishi enzi hizo ambao hawakuwa viongozi, pensheni zao haziwatoshi kwa wiki moja.
 
Ukitaka kujua mshahara wa rais wa nchi muulize maana yeye ndio shahidi, usiwaulize wengine watakudanganya.

Nina Imani kuwa UKONGA IMEJAA hivyo nitamuuliza Rais lakini kama iko na Nafasi simuulizi Ng'o sitaki kwenda HUKO
 
[FONT=Open Sans, arial, sans-serif]The president of Tanzania Kikwete salary per annul is T sh 300,000,000/= three hundred million of which if convert to US D is $187,500/ the president gets many benefits free accommodation at resident all food and laundry and transportation is fully paid the president gets full medical including all his family members president also gets clothing allowance, travel and entertainer allowance.[/FONT]

Source: What is the salary of Tanzania president



Wakuu tukiwa kama waajili wa hawa Viongozi ni shurti na haki yetu kujua malipo yao, hapa naongelea Mishahara yao, Posho zao, Marupurupu na Pension.

Tumejua ya wawakilishi wetu bungeni, na sasa ni hawa viongozi waandamizi wa Serikali.

Tumepiga kelele na kupinga ongezeko la sitting allowance (Posho) za wabunge na nadhani kwa kiasi kikubwa tuko mbioni kufanikiwa sasa ni wakati wa kuangalia malipo na posho za hawa viongozi wengine, hali ya maisha kwa mtanzania wa kawaida ni ngumu huku asilimia kubwa ikiishi chini ya Usd 1 kwa siku.

Mwenye hizi data atuwekee hapa, tuzijue na kuzipitia.

Asalaam

MODs Please msiunganishe thread hii na nyingine yeyote please.
 
Back
Top Bottom