Kwa kawaida inatakiwa uongezewe hiyo incrememt mara unapopeleka transcript. Miaka mitatu utakuwa unaenda daraja lingine
Ha ha ha pole sana Mkuu, wengine hatuko hivo, bado kuna watu tuko clean MkuuHua inachikua muda huo hata zaidi maana ma afisa utumishi serikalini hujiona ka miungu mtu,wanakimbizana tu na posho inshort hakuna uwajibikaji.
Kwa kawaida inatakiwa uongezewe hiyo incrememt mara unapopeleka transcript. Miaka mitatu utakuwa unaenda daraja lingine
Mkuu kwenye ground hakuko hivyo hizo ni sheria tu. Niliamua kuacha kazi ya Ualimu kutokana na mambo kama haya. nilipoenda ku upgrade kutoka kwenye certificate to diploma nilikaa miaka mitatu bila kupandishwa huo mshahara wala daraja. kama ni barua niliandika hadi nikamaliza rim Paper hakuna kitu, ndipo nilipoamua kuchepuka na kusomea degree ya vitu tofauti na kuachana nao Ualimu. Kuna rafiki zangu wali upgrade kutoka certificate direct to bachelor, tokea wamemaliza mwaka juzi mpaka sasa wanalipwa mshahara wa TGTS C na wamechoka kuandika hizo barua za kupanda vyeo. Tatizo la Idara ya elimu bado wanafanya mambo ki local sana yaani unaenda wilayani Afisa elimu hana Data Base ya walimu wake ndo maana unakuta hadi waliofariki wanapanda madaraja, mie tokea nimeacha kazi ya ualimu ni miaka mitano sasa lakin nasikia mwaka jana jina langu lilikuwemo kati ya watu waliopanda daraja
Ukimaliza level ya Masters unaongeezewa increment 2 tu, yaani ongeza 9000 mara mbili kwenye basic salary yako unayopata kutokana na Bachelor. Katika utumishi wa kawaida wa serikali ukiondoa vyuo vikuu, Masters degree ina faida baada ya miak 12 ambapo utapanda hadi TGTS H. Aidha itakuwezesha pia kuteuliwa kushika nafasi kama vile Afisa Elimu (W), Mkoa na/ au Ukurugenzi wizara au ukuu wa idara nyingine serikalini. Hakuna sheria au kawaida ya kupandishwa daraja baada ya kusoma Masters. That's all
Waheshimiwa wana JF,
Kwa yeyote anayefahamu naomba anifahamishe hili jambo:
1.Ukiwa mwajiriwa wa serikali kwa level ya bachelor degree(B.Ed) as Education officer II, then ukapata promotion ya kuwa Education Officer I (I mean baada ya kufanya kazi kwa miaka 3), na baadae ukajiendeleza kimasomo na hatimaye kuwa na Master degree on the similar field/education:-
(a) JE KWA SHERIA ZA KAZI ZA UTUMISHI SERIKALINI/ UALIMU NI DARAJA GANI NINASTAHILI KUPANDISHWA?(Promotion) mfano: TGTSF? TGTSG? au TGTSH?
(b) Kutokana na sheria za utumishi serikalini, ni kiasi gani cha mshahara huwa anaanza kulipwa mfanyakazi mwenye elimu ya UZAMILI (Master degree), I mean kianzio cha mshahara - basic salary? huku ukitambua kuwa wa bachelor degree anaanza na TGSD1 au TGTSD1 kwa ngazi ya shahada (bachelor) , je vipi kuhusu wa master degree?
Natanguliza shukrani zangu za dhati kwa wanaJF.