Inside10
JF-Expert Member
- May 20, 2011
- 33,612
- 40,158
Msemaji wa kundi la waasi la M23 nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Willy Ngoma, ameuawa katika shambulizi la ndege zisizo na rubani mashariki mwa DRC siku ya Jumanne.
Reuters imemnukuu mwanadiplomasia wa eneo hilo, afisa mmoja mwandamizi wa kundi hilo na mshauri wa serikali ya nchi za Magharibi akithibitisha kifo chake.
M23 inadhibiti maeneo makubwa ya majimbo ya Kivu Kaskazini na Kusini baada ya mashambulizi ya mwaka 2025 ambapo waasi hao waliteka miji ya kimkakati ya Goma na Bukavu.
Source Trt Africa