Ng`wanakidiku
JF-Expert Member
- Apr 18, 2009
- 1,195
- 232
MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Pius Msekwa amesema wananchi wanapaswa kuwapima wanasiasa wanaotumia silaha wakati wa kuomba kura kama wanafaa au hawafai kuwa viongozi.
Lakini akaeleza kuwa taratibu za CCM zinasema wanaotumia silaha au kushiriki vurugu kwenye mikutano ya kuomba kura au kufanya kampeni, hawafai kuwa viongozi kwa kuwa wanaleta taswira mbaya kwa wananchi.
Kauli hiyo ya Msekwa imekuja takriban juma moja tangu Mbunge wa Nzega, Dk Hamis Kigwangwalla na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Vijana (UVCCM), Hussein Bashe kudaiwa kutishiana bastola hadharani, huku kila mmoja akimtupia lawama mwenzake.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Msekwa alisema vitendo hivyo vinasababisha wanasiasa kujenga chuki hivyo wanaohusika wanapaswa kuchukuliwa hatua za kisheria ili iwe fundisho kwa wengine. "Tumesikitishwa sana na vitendo vya kutishiana bastola wakati wa kufanya kampeni.
Hii inaleta taswira mbaya kwa wananchi na wanasiasa, kutokana na hali hiyo wanapaswa kuchukuliwa hatua za kinidhamu kwa sababu kitendo hicho ni kosa la jinai kisheria," alisema Msekwa. Msekwa alisema CCM hakiwezi kuwaonya makada hao kwa maneno na wakaelewa hivyo sheria inapaswa kuchukua mkondo wake. Alisema, kiongozi bora ni yule anayetoa hoja na kuzijibu bila ya kuwekeana chuki.
Ugomvi au kutoleana maneno ya kebehi vinadumaza chama na haviwezi kukuza demokrasia. "Hoja zinajibiwa kwa hoja na si kutumia silaha, matusi au maneno ya kusababisha ugomvi. Nawataka wapiga kura wawapime wagombea wa namna hiyo ili wasichague kiongozi ambaye anatumia mabavu kupata madaraka, kwa sababu mwisho wa siku anaweza kusababisha matatizo," alisema. Source: http://mwananchi.co.tz/habari/-/25955-msekwa-wanaotumia-silaha-hawafai-kuwa-viongozi
Maoni yangu:
Kweli CCM haina muelekeo. Wanaona kabisa madhara ya kutumia vurugu (Polisi) ili kukandamiza watu bado unakuta hao hao wanalaani. Nadhani kuna umuhimu CDM kila wanapofanya M4C wawaeleze wananchi kuwa CCM na polisi ni wauaji na waandae CD 2015 waziuze ili uma wa watanzania waelewe 2010-2015 jinsi ambavyo CCM imeshiriki kuua watu wasio kuwa na hatia.
Lakini akaeleza kuwa taratibu za CCM zinasema wanaotumia silaha au kushiriki vurugu kwenye mikutano ya kuomba kura au kufanya kampeni, hawafai kuwa viongozi kwa kuwa wanaleta taswira mbaya kwa wananchi.
Kauli hiyo ya Msekwa imekuja takriban juma moja tangu Mbunge wa Nzega, Dk Hamis Kigwangwalla na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Vijana (UVCCM), Hussein Bashe kudaiwa kutishiana bastola hadharani, huku kila mmoja akimtupia lawama mwenzake.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Msekwa alisema vitendo hivyo vinasababisha wanasiasa kujenga chuki hivyo wanaohusika wanapaswa kuchukuliwa hatua za kisheria ili iwe fundisho kwa wengine. "Tumesikitishwa sana na vitendo vya kutishiana bastola wakati wa kufanya kampeni.
Hii inaleta taswira mbaya kwa wananchi na wanasiasa, kutokana na hali hiyo wanapaswa kuchukuliwa hatua za kinidhamu kwa sababu kitendo hicho ni kosa la jinai kisheria," alisema Msekwa. Msekwa alisema CCM hakiwezi kuwaonya makada hao kwa maneno na wakaelewa hivyo sheria inapaswa kuchukua mkondo wake. Alisema, kiongozi bora ni yule anayetoa hoja na kuzijibu bila ya kuwekeana chuki.
Ugomvi au kutoleana maneno ya kebehi vinadumaza chama na haviwezi kukuza demokrasia. "Hoja zinajibiwa kwa hoja na si kutumia silaha, matusi au maneno ya kusababisha ugomvi. Nawataka wapiga kura wawapime wagombea wa namna hiyo ili wasichague kiongozi ambaye anatumia mabavu kupata madaraka, kwa sababu mwisho wa siku anaweza kusababisha matatizo," alisema. Source: http://mwananchi.co.tz/habari/-/25955-msekwa-wanaotumia-silaha-hawafai-kuwa-viongozi
Maoni yangu:
Kweli CCM haina muelekeo. Wanaona kabisa madhara ya kutumia vurugu (Polisi) ili kukandamiza watu bado unakuta hao hao wanalaani. Nadhani kuna umuhimu CDM kila wanapofanya M4C wawaeleze wananchi kuwa CCM na polisi ni wauaji na waandae CD 2015 waziuze ili uma wa watanzania waelewe 2010-2015 jinsi ambavyo CCM imeshiriki kuua watu wasio kuwa na hatia.