Stori: Paparazi Wetu
BAADA ya minong'ono ya muda mrefu, hatimaye staa wa Bongo Fleva, Estelina Sanga ‘Linah' ameweka wazi kuwa anatoka kimapenzi na Nagari Kombo.
Akiteta na kona hii, wikiendi iliyopita jijini Dar es Salaam, Linah alisema: "Ni kweli kwa sasa natoka na Kombo, ndiye mwanaume wangu, sina haja ya kuficha. Mimi na Amini imebaki stori tu, hata yeye ana mtu wake."
Kombo alijipatia umaarufu siku za nyuma baada ya kuingia uwanjani na kumkumbatia mchezaji Ricardo Kaka wa Timu ya Taifa ya Brazil iliyokuwa ikichuana na Taifa Stars katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
GPL
uyo aliingiaga uwanjani ghafla kwenye mechi ya Tanzania na Brazil ili kumkumbatia Kaka na alikula kipigo kizito,wabongo naona wanamuita mtu maarufu mweee!! ngoja nitupitie mapicha yake zaidi ufaidi
Shadarack Nsajigwa (namba 14) kapteni wa Taifa Stars akishangaa jamaa aliyejitosa kwenda katikati ya uwanja kumkumbatia KAKA wakati mechi inaendelea...
Kijana wetu huyu hana tatizo huyu, ni mshabiki tu kama mashabiki wengine, lakini tunaye...
Nagery Ally Kondo (21) akiwa ndani ya ofisi za Clouds FM Radio katika kipindi cha 'Power Breakfast' na Gerald Hando (shati jekundu) na Paul James (PJ) mwenye kofia.
Money Stunna nimecheka sana hizo picha za uwanjani hasa pale nsajigwa anapomshangaa.
Yaani wenzake wapo katikati ya mechi ye anaenda mkumbatia kaka uwanjani???
Ila pamoja na ushabikii yaan mwanaume mwenzio unamkimbiliaa aisee ningekua mimi angekua kaniabisha sanaa maana ningeona kaka ni wa mana kuliko yeyee tenaa