Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,437
- 5,235
Katibu Mwenezi wa ACT Wazalendo Mkoa wa Dar es Salaam, Monalisa Ndala, amewasili katika Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Jumamosi Agosti 23, 2025 kwa ajili ya kikao cha dharura kilichoitishwa kujadili malalamiko aliyowasilisha dhidi ya uongozi wa chama hicho, hususan kuhusu uteuzi wa Luhaga Mpina kuwa mgombea urais wa Tanzania kupitia chama hicho.
Monalisa amewasili katika ofisi hizo akiwa ameambatana na mawakili wake watatu na alipokelewa na Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa, Sisty Nyahoza.
Akizungumzana na Jambo TV kuhusu suala hilo, Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo, Ado Shaibu, amesema kwamba wamepata nafasi ya kuendelea kusisitiza hoja zao ambazo awali waliziwasilisha kimaandishi kwamba uteuzi wa Mpina ulikuwa halali hivyo chama hicho kinasubiri uamuzi wa Msajili.
Monalisa amewasili katika ofisi hizo akiwa ameambatana na mawakili wake watatu na alipokelewa na Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa, Sisty Nyahoza.
Akizungumzana na Jambo TV kuhusu suala hilo, Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo, Ado Shaibu, amesema kwamba wamepata nafasi ya kuendelea kusisitiza hoja zao ambazo awali waliziwasilisha kimaandishi kwamba uteuzi wa Mpina ulikuwa halali hivyo chama hicho kinasubiri uamuzi wa Msajili.