PreGE2025 Msajili avitaka Vyama vya siasa kuheshimu sheria wawapo katika mikutano yao ya hadhara

PreGE2025 Msajili avitaka Vyama vya siasa kuheshimu sheria wawapo katika mikutano yao ya hadhara

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Wont be the same

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2024
Posts
1,564
Reaction score
2,483
Wakuu

Huenda hizi amsha amsha za CHADEMA huko mikoani ndizo zilizomtoa Msajili wa vyama vya siasa kuja kusema chochote kitu? Au kuna kaupenyo kanatafutwa hapa.

====

Yah: MWITO KWA VYAMA VYA SIASA KUHESHIMU SHERIA YA VYAMA VYA
SIASA SURA YA 258

Naomba mrejee suala tajwa hapo juu.

2. Katika mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa inayoendelea, Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa imebaini uwepo wa vitendo vya ukiukwaji wa Sheria ya Vyama vya Siasa Sura 258, kwa baadhi ya vyama vya siasa kuruhusu wanachama na mashabiki wake kutumia maneno ya uongo, kashfa na uchochezi dhidi ya chama kingine, mtu binafsi, taasisi au Serikali. Hivyo, Msajili wa Vyama vya Siasa anatumia fursa hii kukiasa kila chama cha siasa chenye usajili kamili, kuwaelimisha na kuwadhibiti wanachama na mashabiki wake, kuhakikisha hawakiuki sheria za nchi, hususani Sheria ya Vyama vya Siasa na kanuni zake wakati wa mikutano ya hadhara.

3. Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa inaendelea kutekeleza wajibu wake wa kufuatilia mienendo ya viongozi, wanachama na mashabiki wa vyama vya siasa katika mikutano hiyo, ili kubaini endapo kuna ukiukwaji wa sheria ya vyama vya siasa unaoendelea. Aidha, Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa haitasita kuchakua hatua za kisheria kwa chama cha siasa au mwanachama wa chama cha siasa ambaye atapuuza
mwito huu.

4. Nashukuru kwa ushirikiano wako.
====

Pia soma

 

Attachments

Akapate uthibitisho wa consignment ya virus vya Ebola na Mpox kwanza ili apate uhalali wa kuhoji uongo wa wengine
 
Wakuu

Huenda hizi amsha amsha za CHADEMA huko mikoani ndizo zilizomtoa Msajili wa vyama vya siasa kuja kusema chochote kitu? Au kuna kaupenyo kanatafutwa hapa.

====

Yah: MWITO KWA VYAMA VYA SIASA KUHESHIMU SHERIA YA VYAMA VYA
SIASA SURA YA 258

Naomba mrejee suala tajwa hapo juu.

2. Katika mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa inayoendelea, Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa imebaini uwepo wa vitendo vya ukiukwaji wa Sheria ya Vyama vya Siasa Sura 258, kwa baadhi ya vyama vya siasa kuruhusu wanachama na mashabiki wake kutumia maneno ya uongo, kashfa na uchochezi dhidi ya chama kingine, mtu binafsi, taasisi au Serikali. Hivyo, Msajili wa Vyama vya Siasa anatumia fursa hii kukiasa kila chama cha siasa chenye usajili kamili, kuwaelimisha na kuwadhibiti wanachama na mashabiki wake, kuhakikisha hawakiuki sheria za nchi, hususani Sheria ya Vyama vya Siasa na kanuni zake wakati wa mikutano ya hadhara.

3. Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa inaendelea kutekeleza wajibu wake wa kufuatilia mienendo ya viongozi, wanachama na mashabiki wa vyama vya siasa katika mikutano hiyo, ili kubaini endapo kuna ukiukwaji wa sheria ya vyama vya siasa unaoendelea. Aidha, Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa haitasita kuchakua hatua za kisheria kwa chama cha siasa au mwanachama wa chama cha siasa ambaye atapuuza
mwito huu.

4. Nashukuru kwa ushirikiano wako.
====

Pia soma

Watu watangaze sera zao
 
5fb83bfb-4fca-419f-beb5-1b3689a90c0c (3).jpeg
 
Back
Top Bottom