Msafara wa Waziri Mkuu wa Uingereza

Msafara wa Waziri Mkuu wa Uingereza

ng'ombo

JF-Expert Member
Joined
Dec 1, 2014
Posts
418
Reaction score
619
Huu ndo msafara wa Waziri Mkuu wa Uingereza. Nchi ya tano kwa uchumi mkubwa duniani, bila shaka kuna jambo la kujifunza kwa viongozi wetu wa nchi changa za kiafrika especially sisi Tanzania.
Screenshot_2018-12-11-14-45-51-1.jpeg
 
😂😂😂 njoo matopeni huku, shemeji yake 🔑🔑🔑 akiwa anatoka airport tu, ujue safari za gongo la mboto town shida
 
Kujifunza ni ruksa. Lakini kuiga ni kitu kingine, ni utumwa. Mazingira ya nchi yake yanamruhusu kuwa hivyo.
Swali kwa nini misafara ya wakuu wetu mfano mkuu wa mkoa awe na msafara wa magari kumi? Ni mazingira gani yanatuma viongozi wetu wawe na msafara wa magari mengi? Nauliza kama mtu asiyeelewa.
 
Kwa hiyo ulitaka nasi tuwaige? Hivi watanzania huu utamaduni wa kuiga na kufuata mila za watu utaisha lini? Ilianza hizi dini za maboti zisizo na tija kwetu, tumejimilikisha na kuacha imani zetu, kuna waafrika wanafunga ndoa wamevaa kanzu na masime kiunoni kujifananisha na jamii fulani bila hata kujuwa ukweli wa huo uvaaji. Kwa kweli wacha waafrika tuendelee kuchekwa tu.
 
Kwa hiyo ulitaka nasi tuwaige? Hivi watanzania huu utamaduni wa kuiga na kufuata mila za watu utaisha lini? Ilianza hizi dini za maboti zisizo na tija kwetu, tumejimilikisha na kuacha imani zetu, kuna waafrika wanafunga ndoa wamevaa kanzu na masime kiunoni kujifananisha na jamii fulani bila hata kujuwa ukweli wa huo uvaaji. Kwa kweli wacha waafrika tuendelee kuchekwa tu.
Kweli kabisa! Tuache kuigaiga tamaduni na uvumbuzi usio wetu.
Tungerudi kwenye kuvaa magome ya miti na ngozi kwani nguo hizi tumeiga tamaduni za watu. Turudi kwenye aina ya makazi tuliyokuwa nayo kabla hata ya wafanyabiashara wa mbali kuja, kwani hizi za kisasa nikuiga tu. Kwanini tutumie magari, kompyuta au simu? Hata hii mitandao tunayotumia tumeiga mifumo ya mawasiliano, turudi kwenye mifumo yetu ya zamani ya mawasiliano. Hakuna haja ya kuiga kitu chochote kutoka mataifa ya nje wala kutumia uvumbuzi wa wengine, tunaweza kuishi kivyetu kwa kutumia vya kwetu tu, tutakuwa "developdi dona kantri" mapema sana. Kuiga chochote kile ni kujididimiza kiakili na tutaendelea kuchekwa tu.
 
Huu ndo msafara wa Waziri Mkuu wa Uingereza. Nchi ya tano kwa uchumi mkubwa duniani, bila shaka kuna jambo la kujifunza kwa viongozi wetu wa nchi changa za kiafrika especially sisi Tanzania. View attachment 965169
Na mshahara wake ni pauni laki moja na elfu arubaini na tisa kwa mwaka 149,000 sterling pounds. NARUDIA TENA KWA MWAKA
 
Kweli kabisa! Tuache kuigaiga tamaduni na uvumbuzi usio wetu.
Tungerudi kwenye kuvaa magome ya miti na ngozi kwani nguo hizi tumeiga tamaduni za watu. Turudi kwenye aina ya makazi tuliyokuwa nayo kabla hata ya wafanyabiashara wa mbali kuja, kwani hizi za kisasa nikuiga tu. Kwanini tutumie magari, kompyuta au simu? Hata hii mitandao tunayotumia tumeiga mifumo ya mawasiliano, turudi kwenye mifumo yetu ya zamani ya mawasiliano. Hakuna haja ya kuiga kitu chochote kutoka mataifa ya nje wala kutumia uvumbuzi wa wengine, tunaweza kuishi kivyetu kwa kutumia vya kwetu tu, tutakuwa "developdi dona kantri" mapema sana. Kuiga chochote kile ni kujididimiza kiakili na tutaendelea kuchekwa tu.


Umemaliza kumwaga povu? Kwa kweli watu kama nyinyi mna akili za kuazima, ila si kosa lako.
 
Huu ndo msafara wa Waziri Mkuu wa Uingereza. Nchi ya tano kwa uchumi mkubwa duniani, bila shaka kuna jambo la kujifunza kwa viongozi wetu wa nchi changa za kiafrika especially sisi Tanzania. View attachment 965169
Mbona ni msafara wa kawaida tu kama wa Mh.waziri mkuu wa nchi kubwa na yenye nguvu kiuchumi Africa nchi ya Tanzania,embu tutumie picha za msafara wa malkia wa uingereza ili tuone,halafu ndio uludi na swali lako la kipopoma jukwaani.
 
Ukiliangalia katika muktadha wa muonekano ni sawa kabisa, Ila kwa namna nyengne jarbu kuwaza security system ambayo iko ndan ya hilo gari plus other softicated security system ambazo wenzetu wame invest into... So inawezekana securty ya kimfumo ni kubwa sana kuliko ya kimuonekano.
 
Swali kwa nini misafara ya wakuu wetu mfano mkuu wa mkoa awe na msafara wa magari kumi? Ni mazingira gani yanatuma viongozi wetu wawe na msafara wa magari mengi? Nauliza kama mtu asiyeelewa.
Kabla ya kukuelewesha kwanza tujue una umri gani?maana watoto chini ya umri wa miaka 18 hawaruhusiwi kumiliki simu.
 
Back
Top Bottom