Msaada: Wataalam wa kutengeneza maturubai

Msaada: Wataalam wa kutengeneza maturubai

mafia boy

JF-Expert Member
Joined
Jan 7, 2013
Posts
268
Reaction score
82
Habari wanajamvi,

Poleni na majukumu.

Wanajamvi wenzangu, mimi nipo kijijini huku, nimeiona changamoto moja nahitaji kuifanya fursa, changamoto yenyewe ni ukosefu wa maturubai ya kutundika kwenye sherehe au misiba.

Huku kijijini tunapata kazi ya kukata miti au kupita kuazima kwa watu binafsi sasa nikipita pita huko mijini kwenu nayaona maturubai mnatundika na yanakua na nguzo za chuma, nimeyapenda na nataka kua nayo.

Please kwa yoyote anaejua mafundi/wataalam wa kuyatengeneza anisaidie hapa na bei zake kabisa.

Nahitaji kama 3 hivi.
 
nilitengeneza la futi 20 kwa fut15 kwa laki nane na nusu. nikiikumbuka namba ya fundi ntaiweka hapa mkuu mafia boy
 
Niambie Uko mkoa gani mkuu. Hiyo ni moja ya kazi kwa kiwanda changu kidogo. Kama vipi ni PM Ntumie na namba tuongee!! Am serious
 
Nitafute nikutengenezee huwa nayatengeneza sana tu,
 
Back
Top Bottom