Laurence
JF-Expert Member
- Jun 11, 2011
- 3,104
- 426
Heshima mbele wakuu wote wa Jf;mimi ni wakala wa Mpesa;Airtel Money na tigo Pesa;kuna mtu alimtumia msichana sms kwamba mimi boss wake nahitaji kiasi hicho cha fedha huku akimweleza kuwa mimi yani akimaanisha mimi boss wake sitokuwa hewani kwa sababu nimeishiwa chaji na inaonekana ali hack namba yangu mana msichana anasema sikuwa hewani lakn muda wote nilikuwa hewani;sasa mara baada ya kutuma fedha kiasi cha millioni moja ndipo binti akanipigia simu baada ya muda akiniuliza nishapata hela? Nikamwambia sijahitaji hela yoyote kwako na ukitizama sms ya kwanza aliomtumia ilionekana ndilo jina ambalo amenisave huyo msichana wangu wa kazi;je naweza mpata kama nikimwaga namba zake hapa? Maana alitumia namba nyingi mbali mbali kutumiwa hyo fedha;maoni yenu tafadhari na funzo kwa wenzangu