onkoko
JF-Expert Member
- Aug 23, 2016
- 514
- 480
Naomba ushauri ndugu zangu, mimi ni kijana wa miaka 30, nimeoa na nimebatika kupata mtoto mmoja wa kike. Nimepanga nyumba mbezi beach yenye chumba na sebule. Sasa naishi na mtoto wa dada ya mke wangu ambaye pia ana mtoto na pia yupo dada wa kazi ambaye hubaki na watoto pindi tunapoenda kutafta mkate asubuhi. Tatizo ni kuwa huyu binti ya dada wa mke wangu amekuwa na dharau mpaka nakosa uhuru had anadiriki kuingia chumbani tukiwa tumelala mimi na mke wangu bila hodi na kuingilia faragha zetu. Wakati mwingine anaingia chumbani nikiwa pekee angu na huku nimevaa boxer tuu. kitu cha kushangaza nikimwambia mke wangu amrudishe kwao yeye hugoma na kusema hawatamwelewa kwao huku dharau zikiongezeka dhidi yangu.
Sasa huwa nafikiria kuachana na mke wangu maana naona nakosa uhuru kitu ambacho nahitaji uhuru pili kipato changu ni kidogo kias kwamba kuhudumia watu saba kila siku na kwa uchumi huu inanaipa ugumu wa kufanya maendeleo yoyote yale.
NB: mke wangu ni mchaga na Mimi mtu mbeya.
Sasa huwa nafikiria kuachana na mke wangu maana naona nakosa uhuru kitu ambacho nahitaji uhuru pili kipato changu ni kidogo kias kwamba kuhudumia watu saba kila siku na kwa uchumi huu inanaipa ugumu wa kufanya maendeleo yoyote yale.
NB: mke wangu ni mchaga na Mimi mtu mbeya.

