Msaada wa ushauri mahusiano yangu yamevurugika

Msaada wa ushauri mahusiano yangu yamevurugika

ankai

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2017
Posts
3,282
Reaction score
4,259
Wakuu habari za asubuhi, kama kichwa kinavyojielezea kuna mwanamke niko naye kwenye mahusiano kwa muda wa miaka miwili sasa lakini baada ya muda tuliojiwekea kwamba tuharalishe mahusiano yetu mwenzangu anaonekana kama tayari ame loose interest na mimi na hataki tena niende kwako,

Story ya mahusiano yetu iko ivi

Mwaka 2018 /01 /01 mimi na uyu binti tulianza rasmi mahusiano yetu kila mmoja akiwa anampenda mwenzake kwa dhati sana ilituchukua miezi minne katika mahusiano yetu tukaamua tuanze kuishi pamoja kienyeji nikimaanishaa yeye kutoka kwao na kuja kwangu tukaanza maisha,

Maisha yetu yalikuwa ya furaha japo ups and downs hazikukosa zikiwa zabkutosha tu kama ilivyo ada ya mahusiano yoyote yale baada ya miezi 5 ya kuishi pamoja mwenzangu alipata tatizo la kuugua na tukakubaliana aende nyumbani akanywe dawa za asili maana dawa za hospitali zilidunda nilitafuta nauli akaenda om mi nikaendelea na mishe mishe za maisha uku nikiendelea nae japo kwa kusua sua kama mnavyojua japo mapenzi yangu kwake hayakuwahi kupungua lakini kama binadamu yeyote yule kupitiwa kupo hasa kukiwepo na umbali kati ya wenza wawili.

Muda umeenda sana na kwa sasa muda rasmi niliomuahidi kwamba ndo muda tunaotakowa kuhararisha mahusiano yetu
Kushughurikia taratibu za kimila kidini na mambo mengine ndo umewadia.

Lakini baada y kumgusia mwenzangu swala hili hajalipokea kama nilivyotarajia na pia ushirikiano wake kwangu umekuwa mdogo sana na kuna muda ananiambia ili swala lisubiri kwanza ama tusilifanye kabisa kifupi nimeshindqa kumuelewa na imekuwa kinyume na matarajio yangu mambo yapo mengi yaliyotokea apo katikati katika safari yetu kuanzia tulipoanza mahusiano mpaka leo na siwezi kuyaandika yote nikayamaliza .

Wakuu naomba msaada wa kimawazo mtu mtu uyu nimfanyeje nimwelezeje ama nitumie nini ili niwese kumrudisha kwangu maana kwa sasa inaonyesha mapenzi yake kwangu yamepungua na pia najua kuna mwana anaweza naye akawa member wa Jf na akasoma huu uzi labda ndo anatoka naye kwa sasa na ndo amemfanya abadiri malengo

Kifupi uyu ni mwanamke ninayempenda sana sana sana namuhitaji mnowala sihitaji kumpoteza maana mapenzi yangu kwake ni makubwa lakini kwa kwa sasa amekuwa ni mtu ananifungia mlango hanipi ushirikiano sometimes majibu yake ni ya kuniumiza mno.

Nakiri mimi ni binadamu nina mapungufu yangu kama alivyo yeye .

Mwisho naomba msaada kwa yeyote yule ambaye aliwahi kuipitia hali kama hii na akaishinda alifanyaje alitumia nini ama alimtumia nani namaanisha aliyepitia hali hii na akafanikiwa kumrjesha himayani mwenzi wake basi anipwe msaada kimawazo kiushauri ama msaada wowote anaoweza kuutoa kwangu ili mradi nifanikiwe kumrejesha uyu shemeji yenu na wifi yenu himayani tafadhali wakuu.

Hili jambo ni serious mno kwangu na kwa ustawi wa afya yangu japo najua kuna watakao nibeza kuniona boya kunisimanga yote ni sawa maana hii hali na machungu haya ninaye yapitia ni mimi

Bado naamini Jf ni sehemu salama na bado kuna waungwana wengi na wenye hekima na busara wengi ivyo naamini nitapata msaada wa kutataua changamoto yangu

Ankai ..nwasirisha!!

Nb pm yangu iko wazi ntashukuru kwa msaada na kejeli yoyote mtakayonipatia.
 
Ukiona mtu amelose interest ni bora umuache, kumlazimisha arudishe feelings unakosea...anaweza akakubali kwa kukuonea huruma mwisho wa siku ukaja kulia hapa. Kuwa makini kwenye kuoa..usioe mtu ambae unaona kabisa hataki.
 
Ukiona mtu amelose interest ni bora umuache, kumlazimisha arudishe feelings unakosea...anaweza akakubali kwa kukuonea huruma mwisho wa siku ukaja kulia hapa. Kuwa makini kwenye kuoa..usioe mtu ambae unaona kabisa hataki.

Kweli kabisa kaka
 
Kile kilichosababisha mkapendana naimani kabisa ukiweza kukihuisha mapenzi yatarudi kama awali!
Daaah kuna ugumu kidogi kwenye hili ndugu hili tuko mbali mbali niko dar yuko mkoa mambo ni mengi sema kila kitu kinapangwa na je ni vip kama labda Mungu alipanga tuipitie njia hii ndo tufike kwenye mahusiano yenye mafanikio maana najua ata whine haipikwei kwa siku moja inachukua process mpaka kuja kuwa tamu kama tunavyoiona leo!!
 
Daaah kuna ugumu kidogi kwenye hili ndugu hili tuko mbali mbali niko dar yuko mkoa mambo ni mengi sema kila kitu kinapangwa na je ni vip kama labda Mungu alipanga tuipitie njia hii ndo tufike kwenye mahusiano yenye mafanikio maana najua ata whine haipikwei kwa siku moja inachukua process mpaka kuja kuwa tamu kama tunavyoiona leo!!

 
Wakuu habari za asubuhi, kama kichwa kinavyojielezea kuna mwanamke niko naye kwenye mahusiano kwa muda wa miaka miwili sasa lakini baada ya muda tuliojiwekea kwamba tuharalishe mahusiano yetu mwenzangu anaonekana kama tayari ame loose interest na mimi na hataki tena niende kwako,

Story ya mahusiano yetu iko ivi

Mwaka 2018 /01 /01 mimi na uyu binti tulianza rasmi mahusiano yetu kila mmoja akiwa anampenda mwenzake kwa dhati sana ilituchukua miezi minne katika mahusiano yetu tukaamua tuanze kuishi pamoja kienyeji nikimaanishaa yeye kutoka kwao na kuja kwangu tukaanza maisha,

Maisha yetu yalikuwa ya furaha japo ups and downs hazikukosa zikiwa zabkutosha tu kama ilivyo ada ya mahusiano yoyote yale baada ya miezi 5 ya kuishi pamoja mwenzangu alipata tatizo la kuugua na tukakubaliana aende nyumbani akanywe dawa za asili maana dawa za hospitali zilidunda nilitafuta nauli akaenda om mi nikaendelea na mishe mishe za maisha uku nikiendelea nae japo kwa kusua sua kama mnavyojua japo mapenzi yangu kwake hayakuwahi kupungua lakini kama binadamu yeyote yule kupitiwa kupo hasa kukiwepo na umbali kati ya wenza wawili.

Muda umeenda sana na kwa sasa muda rasmi niliomuahidi kwamba ndo muda tunaotakowa kuhararisha mahusiano yetu
Kushughurikia taratibu za kimila kidini na mambo mengine ndo umewadia.

Lakini baada y kumgusia mwenzangu swala hili hajalipokea kama nilivyotarajia na pia ushirikiano wake kwangu umekuwa mdogo sana na kuna muda ananiambia ili swala lisubiri kwanza ama tusilifanye kabisa kifupi nimeshindqa kumuelewa na imekuwa kinyume na matarajio yangu mambo yapo mengi yaliyotokea apo katikati katika safari yetu kuanzia tulipoanza mahusiano mpaka leo na siwezi kuyaandika yote nikayamaliza .

Wakuu naomba msaada wa kimawazo mtu mtu uyu nimfanyeje nimwelezeje ama nitumie nini ili niwese kumrudisha kwangu maana kwa sasa inaonyesha mapenzi yake kwangu yamepungua na pia najua kuna mwana anaweza naye akawa member wa Jf na akasoma huu uzi labda ndo anatoka naye kwa sasa na ndo amemfanya abadiri malengo

Kifupi uyu ni mwanamke ninayempenda sana sana sana namuhitaji mnowala sihitaji kumpoteza maana mapenzi yangu kwake ni makubwa lakini kwa kwa sasa amekuwa ni mtu ananifungia mlango hanipi ushirikiano sometimes majibu yake ni ya kuniumiza mno.

Nakiri mimi ni binadamu nina mapungufu yangu kama alivyo yeye .

Mwisho naomba msaada kwa yeyote yule ambaye aliwahi kuipitia hali kama hii na akaishinda alifanyaje alitumia nini ama alimtumia nani namaanisha aliyepitia hali hii na akafanikiwa kumrjesha himayani mwenzi wake basi anipwe msaada kimawazo kiushauri ama msaada wowote anaoweza kuutoa kwangu ili mradi nifanikiwe kumrejesha uyu shemeji yenu na wifi yenu himayani tafadhali wakuu.

Hili jambo ni serious mno kwangu na kwa ustawi wa afya yangu japo najua kuna watakao nibeza kuniona boya kunisimanga yote ni sawa maana hii hali na machungu haya ninaye yapitia ni mimi

Bado naamini Jf ni sehemu salama na bado kuna waungwana wengi na wenye hekima na busara wengi ivyo naamini nitapata msaada wa kutataua changamoto yangu

Ankai ..nwasirisha!!

Nb pm yangu iko wazi ntashukuru kwa msaada na kejeli yoyote mtakayonipatia.

Kuhama inaruhusiwa tu . kwan mmezaliwa wote? Acha stress hamia kwingine tu. Mapenzi mbinguni tu duniani maigizo
 
Jipe Muda tu utazoea. ..Wakati huponya ---jitahidi kujiepusha 'kumpenda mtu ambaye amepoteza upendo na wewe. ..mbaya zaidi amesha kueleza kabisa ''

Yaani mkuu mwanamke akisha kueleza muachane fanya hima sana kutekeleza Shauri lake --' la sivyo baadae utakuja kulia na kusaga meno
 
Daaah kuna ugumu kidogi kwenye hili ndugu hili tuko mbali mbali niko dar yuko mkoa mambo ni mengi sema kila kitu kinapangwa na je ni vip kama labda Mungu alipanga tuipitie njia hii ndo tufike kwenye mahusiano yenye mafanikio maana najua ata whine haipikwei kwa siku moja inachukua process mpaka kuja kuwa tamu kama tunavyoiona leo!!
Mdogo wangu mahusiano ya mbali sijui niyafananishe na nini...haiwezekani kibinadamu mtu kukutana na mazingira mapya bila kuwa na interaction na watu wengine! Namini hata wewe una mbadala unayemmezea mate kila akipita mbele yako na kutingisha minyama. Ushauri wangu ni kwamba tafuta pesa,jijenge kimaisha,mapenzi yalikuwepo tokea sodoma na gomora...kama alipangwa kuwa wako atakua na kama hakupangwa hata ukipewa ushauri page 200 hautabadili meaning!
 
Jipe Muda tu utazoea. ..Wakati huponya ---jitahidi kujiepusha 'kumpenda mtu ambaye amepoteza upendo na wewe. ..mbaya zaidi amesha kueleza kabisa ''

Yaani mkuu mwanamke akisha kueleza muachane fanya hima sana kutekeleza Shauri lake --' la sivyo baadae utakuja kulia na kusaga meno
Duuh mbona ushauri wote umu ndani ni wa kinivunja moyo jamani yaani hakuna ata mmoja anayeweza kunipa ushari wa kuyajenga mapenzi yangu na uyu binti ata wewe braza kweli huna option nyingine ninayoweza kui apply hadi nikalirejesha penzi langu!!
 
Ndugu pole sana, unafanya shughuli gani?

Kama Una business zako jikite huko utumie muda mwingi kwenye biashara, ukiwa na biashara na mipango inaondoa mambo ya kufikiri mapenzi. Siku ya siku atakuambia naomba tuachane ndo utazidi kuumia.
Kama umejitandaa kisaikologia uwezi kuanza kumfikiria yeye. Hakuna mwanamke asiyependa kutolewa barua wala kuolewa ukiona hivyo ujuwe mtoto wa kike ana balance mizani.

Anza kutuma TIGOPESA, M PESA, AIRTEL MONEY kwa uwingi uangalie mwelekeo wake. Unaweza kurudisha upendo
 
Ukiona maisha magumu achana nayo Fanya kitu kingine. Halafu bila shaka wee utakua msukuma au kutoka kanda ya ziwa manake nyie ndio mnakua washamba washamba sana kwenye mapenzi,mwanamke amelose interest kwako halafu bado unamnng'ang'ania wa nini,acha uboya tafuta demu mwingine mtembezee rungu maisha yaendelee utamsahau tu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom