Mimi nilipata mkopo mwaka Jana ila niliscreenshot allocation za miaka yote 3 na mpaka sasa ninazo licha ya hvyo hata zingepotea Leo siwezi kusahau allocation zangu.
Allocation zilianza kupotea baada ya kufunguliwa kwa OLAMS kwa mwaka mpya wa masomo kisha kuruhusu wanafunzi wapya kuomba mikopo.
Ila uhalisia ni kuwa allocation ulizowekewa kwa miaka yako yote mitatu haziwezi kubadilika, Me nakumbuka kuwa tulikatwa boom quarter 4 kwa mwaka wa kwanza(41,000Tsh).
Ila mwaka huu bodi wamekuja kitofauti kwa hawa ndugu zetu, wameonesha allocation kwa mwaka wa kwanza tu, miaka mingine hawajaweka na hata mwanafunzi hawezi kujua kuwa kapata kiasi gani miaka yake ijayo ya masomo hii ingeweza kupunguza Frustrations kwa wanafunzi kutokana na ufinyu wa kiasi cha pesa kwa mwaka wa kwanza..!!
Labda inamaaan kuwa kiasi alichopata mwaka huu wa kwanza ndicho kitadominate miaka yake yote ya masomo(Yaan kama inaonesha mwanafunzi kapata 20% ya ada basi miaka yote atapata hiyohyo).