Nyamburi
JF-Expert Member
- Oct 28, 2011
- 306
- 36
Wadau salaam!mim nimeingia matatizoni na mwenye nyumba yangu juu ya suala la upangaji,mkataba wangu uliisha mwishoni mwa mwezi july 2012,na mkataba wa awali ulikua wa miezi sita,baada ya kuongea na muwakilisha wa mwenye nyumba tulikubaliana kua ningeongeza mkataba wa miezi minne kwa kua natarajia kuhama mkoa mwishoni mwa mwaka,tulikubaliana nikamtumia mwenye nyumba kiasi cha shilingi 340,000 na kuahidi kummalizia 60,000 pindi atakaponikabidhi mkataba wangu,cha ajabu juzi amenipigia simu na kuniambia kua amepata mpangaji mwingine atakaempa tshs 120,000 kwa mwezi,hivyo nimruhusu huyo mpangaji mpya kuingia ndani kukagua vyumba na natakiwa niwe nimehama ndani ya siku tatu naye angekata hela niliyokaa kwenye nyumba na kunirudishia iliyobaki,maelezo hayo alinipa kwenye simu bila maandishi,mimi sijamjibu lolote mpaka sasa,naomba msaada wenu kisheria wadau,je hakuna sheria inayonilinda mimi kama mpangaji katika suala ili!asanteni