Msaada wa haraka kwa tapeli huyu!

Msaada wa haraka kwa tapeli huyu!

Zeroth

Member
Joined
Jan 26, 2017
Posts
25
Reaction score
18
Habar,

Wakuu mama yangu aliibiwa simu sikukui ya idd maeneo ya Magomeni ikiwa na laini mbili ya tigo na zantel,tuliwapigia tigo tukawaambia waifungie laini wakakubali lakini hawakufanya hivyo kama walivyotuahidi. Sasa hii leo huyo jamaa amekua akitumia watu wa kwenye majina ya muke kwenye simu sms ya kitapeli kupitia laini ya tigo, sms ni hii " Habari Za Leo Samahani Kuna Afisa Miradi Na Utalii Yeye Ni Jamaa Yangu Yupo Serengeti Hifadhi Ya Wanyama Pori Yuko Na Watalii/wazungu Wanakuja Leo Wanahitaji Bidhaa Za Kitalii Kama Vinyago Vya Kuchongwa Kwa Miti Picha Za Michoro,vikoi,mashuka Ya Kimasai Pamoja Na Vitu Vingine Tenda Hiyo Niliwahi Kuisimamia Mimi Ila Kwa Leo Hali Yangu Kiafya Sio Nzuri Nasumbuliwa Kifua Pamoja Na Tonses Hata Sauti Imekauka Hivyo Nakuomba Usimamie Kwa Leo Kama Uko Tayari Nijulishe Nikuunganishe Ili Akupatie Mwongozo Jinsi Ya Kusimamia Wanalipa Posho Nzuri Nakutegemea Sana Naomba Usiniangushe"

Hapa nilipo natokea polisi lakini wameniambia kuwa niende kesho nikaonane na mpelelezi, na sisi hatua tuliyoichukua mpaka sasa ni kuwajulisha watu kua hiyo sms waipuuze.pia dada amejaribu kuchati naye anasema yeye yupo Bagamoyo .
Sasa nilikua naomba mawazo yenu wana jf jinsi ya kumkabili huyu tapeli na ikiwezekana tumkamate kabisa!
 
huwa washenzi sana hao wananikera sana kwanini wasitafute pesa kihalali tu
 
Mm liliwahi kunitokea nikamtumia jamaa kwenye tigopesa kumbe line alishaiba zamani.
 
Na sasa hivi kuna mtu kamwambia yupo manzese
 
Ilitakiwa baada ya kuwapigia wenye kampuni za simu zifungwe mda huohuo. Nimeibiwa mara nyingi sana lakini kila nikipiga tigo na voda wanafunga mda huohuo. Kuna uzembe mkubwa sana. Aende makao makuu ya kampuni hizo.
 
Tapeli yupo busy kufanya yake ila Geshi letu tukufu linasema uende home urelax na kurudi kesho. Hakyamamaa jeshi letu ni la mfano na hakunaga dunia nzima.

Wapigieni simu hao customer care wa Tigo waifunge hiyo line. Lakini pia ujanja wa huyo tapeli ni wa kizamani sana na ni mgeni tu ndo ataingia king.
 
Ndiyo maana huwa nasema kila tukifanyacho hapa "Bongo" ni maigizo tu. Matapeli wapo kazini kila kukicha hawakamatwi, badala yake wanazingatia wanaotoa uzi wenye akili eti wanaingilia serikali!
 
Mwambie huyo mama YAKO aende akai-renew iyo simcard yake, ,,au ameenda kuiswap wakamkatalia?,????Au ni gharama kubwa sana sasaivi
 
Mjinga huyo mama YAKO, ,,sa si aliRenew simcad,,,au mpo koromije
Hakuna siku ambayo JF nimeiona chungu kama hii leo, yani nina machungu ya mama kuibiwa nikaona ni vyema niwashirikishe wana jf wenzangu kwa msaada zaidi but unfortunately naambulia kumtukanisha mama hivhiv yani. Binafsi siwezi matusi na wala majibizano na watu na sijawahi kufanya hivyo hata humu JF so inabidi mkuu nivumilie tu japo kua imeniuma mno na kunikereketa sana nafsi yangu na naishia kujilaumu tu kwanini nilianzisha hii thread!!
 
Hakuna siku ambayo JF nimeiona chungu kama hii leo, yani nina machungu ya mama kuibiwa nikaona ni vyema niwashirikishe wana jf wenzangu kwa msaada zaidi but unfortunately naambulia kumtukanisha mama hivhiv yani. Binafsi siwezi matusi na wala majibizano na watu na sijawahi kufanya hivyo hata humu JF so inabidi mkuu nivumilie tu japo kua imeniuma mno na kunikereketa sana nafsi yangu na naishia kujilaumu tu kwanini nilianzisha hii thread!!
Mpuuzie huyo binadamu aliyekosa busara
Btw hyo text tushaipata whatsap fanya tu mchakato wa kufunga hyo line
 
Kwanini umtukane Mama wa mwenzako?Unaujua umri wake?Ukitukaniwa mama yako utajisikiaje?Akiwa ni mwenye umri sawa na Mama yako huoni kuwa hujatenda sawa?

Kulikuwa na haja ya kutukana?Kwanini usitoe ushauri bila kashfa?Jiangalie mkuu

Mkuu nimerekebisha kauli yangu,,,,ila mama yake nadhani nipo nae sawa kiumri,,,, ila we uhoni kama hao ni wazembe sana,,maana kawaida ukipoteza Simu unaenda kuSwap simcard nyingine ni dakika chache tu ,, ,,vitu vingine tunawalaumu bure mitandao ya Simu mkuu, ni uzembe wetu wenyewe,,
 
Hakuna siku ambayo JF nimeiona chungu kama hii leo, yani nina machungu ya mama kuibiwa nikaona ni vyema niwashirikishe wana jf wenzangu kwa msaada zaidi but unfortunately naambulia kumtukanisha mama hivhiv yani. Binafsi siwezi matusi na wala majibizano na watu na sijawahi kufanya hivyo hata humu JF so inabidi mkuu nivumilie tu japo kua imeniuma mno na kunikereketa sana nafsi yangu na naishia kujilaumu tu kwanini nilianzisha hii thread!!
Sorry Mkuu, ,nilikosea kweli ilo neno mjinga, ,,ila mwambie akai-renew iyo simcard mkuu
 
Kuhusu hapo simu sana sana uifungie isitumike kama una IMEI ya simu
 
Tapeli yupo busy kufanya yake ila Geshi letu tukufu linasema uende home urelax na kurudi kesho. Hakyamamaa jeshi letu ni la mfano na hakunaga dunia nzima.

Wapigieni simu hao customer care wa Tigo waifunge hiyo line. Lakini pia ujanja wa huyo tapeli ni wa kizamani sana na ni mgeni tu ndo ataingia king.
Hata usajili hauna maana yoyote.
 
Sorry Mkuu, ,nilikosea kweli ilo neno mjinga, ,,ila mwambie akai-renew iyo simcard mkuu
Poa mkuu usiwaze, lakini ili urenew lain inabidi iwe offline at least siku tatu mfululizo. Lakin hiyo lain bado ipo hewani so inabidi tuiblock kwanza then iwe offline kwa muda huo ndio tuta-renew
 
Hakuna siku ambayo JF nimeiona chungu kama hii leo, yani nina machungu ya mama kuibiwa nikaona ni vyema niwashirikishe wana jf wenzangu kwa msaada zaidi but unfortunately naambulia kumtukanisha mama hivhiv yani. Binafsi siwezi matusi na wala majibizano na watu na sijawahi kufanya hivyo hata humu JF so inabidi mkuu nivumilie tu japo kua imeniuma mno na kunikereketa sana nafsi yangu na naishia kujilaumu tu kwanini nilianzisha hii thread!!
Pole sana.....ndo vijana wa siku hizi hawa.
 
Back
Top Bottom