Wana jukwaa nipo chalinze,naomba mwenye ufahamu na bei ya cherahan cha kawaida,mashine za kudarizi vitambaa na mashuka pamoja na mashine zingine zinazohusiana na ushonaji,lakin pia yanakopatika maduka yanayouza bidhaa hizi.
Cherehani inategemea kama ni mtumba au dukani, za mtumba ziko juu kidogo na imara kuliko za dukani.
Huku Mbeya, bei inaanza na 160,000 na kuendelea.
Mimi mwenyewe nataka nianzishe hii biashara , ila bado sijapata wazo kamili kulingana na hali yangu ( Mimi ni mtumishi wa uma)
Je ni vizuri kumpa mtu- kumkodishia mtu, au niajiri Taylor awe anafundisha vijana, au nipangishe watu wawe wananilipa kwa siku?
Hii thread ya muhimu ila haikuwa na muendelezo