Msaada: Ushauri kozi nzuri ya Masters

Msaada: Ushauri kozi nzuri ya Masters

Hongera sa kwa aspirations zako mkuu. Kama unataka kuwa lecturer siku za mbeleni basi hauna budi kufanya Master of Science with Education.
Ukispecialize kwenye Chemistry sio mbaya sana na hata Biology. Uwanja wao wa kazi bado ni mkubwa kwa sababu hao watu sio wengi sana. Kama unataka pure degree za Chemistry au Biology basi fanya MSc zake lakini ina ramifications ukizingatia wewe tayari ni mwajiriwa wa kada ya ualimu.
Vinginevyo, ninakutakia kila la kheri
Mkuu nashukuru kutoa muda wako kunishauri kwenye jambo hili. Nitafanya ya Biology, msc applied zoology ya msc physics nahofia mathematics maana si mzuri sana kwenye adv mathematics
 
Mkuu nashukuru kutoa muda wako kunishauri kwenye jambo hili. Nitafanya ya Biology, msc applied zoology ya msc physics nahofia mathematics maana si mzuri sana kwenye adv mathematics
kama mdau alivyokushauri piga msc ya biology ili utoke na gpa kali uwe lecturer....maana physics ni full namba kama sio mzuri sana itakushusha gpa
 
Salaam nyote wanajukwaa. Poleni na hongereni kwa juhudi zote mzichukuazo dhidi ya janga hatari la corona.
Naomba niende kwenye mada moja kwa moja.

Mimi muhitimu wa shahada ya sayansi elimu (bsc ed, masomo yakiwa Physics & Biology) kwa sasa ni mtumishi wa umma, idara ya elimu yaani mwalimu, na mwaka moja na miezi 6 sasa tangu niajiriwe.

Sasa nimefikiria kusoma masters ya kozi kadhaa ambazo naomba kwa mwenye ufahamu aniongezee kama ni bora kwa soko la ajira la Tanzania, lengo kuu hasa la kusoma masters ni kuja kua LECTURER (bsc ed gpa ni 3.9) au kupata kazi yenye maslahi zaid kwenye MASHIRIKA MAKUBWA duniani kama Save the children, Norwegian refugee council (NRC) na nakadhalika.

Kozi nilizozifikiria hizi hapa;
1. Masters in Public health chuo ni MUHAS
2. Masters of science in Biochemistry chuo ni MUHAS/UDSM/SUA
3. masters of science in Physics chuo ni. UDSM (japo si mzuri sana kwenye mathematics, hasa advanced mathematics nadhani nitatoboa japo kwa mbinde sana)
4. Masters of science in Zoology/ Botany chuo ni UDSM
5. Masters of science with education in Physics/Zoology/ Botany chuo ni UDSM
6. Masters of science in Microbiology au Biotchenology chuo ni UDSM/ SUA

Naomba ushauri na mawazo kwa wajuzi wa haya mambo japo kuna baadhi ya kozi nadhani nikiende kuzisoma mshahara nitakosa ila sitajali sana.

Kama kuna kozi bora zaid na naweza kuisoma bas naomba pia iongezwe kwa wenye ufahamu.

Ahsante, nasubiri mrejesho wako.
Kama unataka kufanya kazi mashirika makubwa duniani yenye mishahara mikubwa kapige MPH pale MUHAS hautojuta.

Kama unataka uwe lecturer kapige MSc Physics. Hii itakuja kukulipa sana baadae mkuu.
 
Mkuu mtoa mada samahani, Ila na wewe Naomba nikuulize Pamoja na Wakuu wengine watakaoweza kusaidia japo post Sio yangu, Nina shemeji yako Hapa ambae pia Ni mwalimu Mwenzako sema yeye amesoma Bachelor ya Biology and Chemistry na akapata GPA ya 3.2, anawezaje kujiendeleza kusoma Masters Maana tulijaribu kufatilia ikaonekana Vyuo vingi wanataka GPA kwanzia 3.5 kwenda juu..

Ni Kozi gani anaweza akasoma ama Kuna Utaratibu gani apitie ili aweze kusoma Masters na yeye, Natanguliza shukrani
 
Achana na Biology mkuu, KASOME ISSUE YEYOTE YA PHYSICS biology wapo wengi mnoo. Kuna watu wana hizo masters lakini bado walimu wa secondary.
 
Mkuu mtoa mada samahani, Ila na wewe Naomba nikuulize Pamoja na Wakuu wengine watakaoweza kusaidia japo post Sio yangu, Nina shemeji yako Hapa ambae pia Ni mwalimu Mwenzako sema yeye amesoma Bachelor ya Biology and Chemistry na akapata GPA ya 3.2, anawezaje kujiendeleza kusoma Masters Maana tulijaribu kufatilia ikaonekana Vyuo vingi wanataka GPA kwanzia 3.5 kwenda juu..

Ni Kozi gani anaweza akasoma ama Kuna Utaratibu gani apitie ili aweze kusoma Masters na yeye, Natanguliza shukrani
Masters anaweza kusoma ila ni kwa course work and dissertation, masters by thesis ndiyo inataka gpa 3.5, kwahy gpa masters anaweza sana kusoma
 
Achana na Biology mkuu, KASOME ISSUE YEYOTE YA PHYSICS biology wapo wengi mnoo. Kuna watu wana hizo masters lakini bado walimu wa secondary.
Mkuu Physics nahofia mathematics inaweza kunishusha gpa, maana nimesikia walimu wa pale udsm wanapenda sana kukomoa watu hasa department ya Physics, all in all ntajaribu mkuu. Thanks kwa mawazo yako
 
Mkuu Physics nahofia mathematics inaweza kunishusha gpa, maana nimesikia walimu wa pale udsm wanapenda sana kukomoa watu hasa department ya Physics, all in all ntajaribu mkuu. Thanks kwa mawazo yako
Sio wana penda kukomoa watu bali wana kupika uive haswa ili usije tema maboko mbele safari .... Jikaze ukapambane hakuna kilicho rahisi kwa maana ukitaka cha uvunguni lazima utakipatia uvunguni sio juu ya kitanda. NENDA uD ndio chuo chenye heshima kubwaaa miongoni mwa vyuo vya EAC kwinginepo utaenda kupiga soga tu.

Kwaheri Mtahiniwa
 
Back
Top Bottom