Msaada unahitajika haraka au ndoa inavunjika

Msaada unahitajika haraka au ndoa inavunjika

Demokrasia katika Mapenzi inatumika pale tu mnapokubaliana kuongea lugha moja., kinyume na hapo Udikteta unachukuwa nafasi yake!!!
 
Hapo kazi kwelikweli mkuu...duuuh

Mfundishe adabu kidogo
 
Yaani haya ni madhara ya kuona wakati akili zenu hazijajiandaa kuwa mke na Mme

Kaa nae mwelekeze kuwa hiyo tabia sio nzuri mwelekeze kwa ustarabu sio unamwelekeza na wewe ukiwa umepaniki

Halafu umeoa na una familia unawezaje kuangaliea x

Ukisha fika umri wa kuwa na familia utoto huwa tunaweka pembeni
 
Mtie makofi mawili ya nguvu atabadilika maana unakaa naye kama dadako.
 
Sikiliza mkuu dawa ya mwanamke mwenye wivu ni kumpenda zaidi, mwenye kukosa imani nawe ni kuwa mwaminifu zaidi, mwenye kukukagua simu yako ni kumpa akae nayo muda awezavyo.Kuwa mwamninifu, mwanamke akichukua simu yako ukawa na mawenge au kumkataza ni kipimo cha kwanza kabisa kwake kuwa wewe hauko salama kiuaminifu. Kama unajiamnini lakini mwachie simu yako akiitaka, usiwe na mawenge mwachie uhuru akukague kwani anayo haki ya kufanya hivyo. Ondoa mapini na mapasiwedi asishindwe kufika popote anapotaka kufika na kuangalia. Unaogopa nini kukaguliwa? au michepuko sana? akikaa na simu yako bila kuambulia sms ya ajabu au ya demu wako, call ya ajabu au ya demu wako atakuamini na atajiweka sawa, kwa sasa kuna vitu vichafu anahisi unavifanya ila akigundua huna hata wazo mwenyewe atakutumai na kukurudishia matuaini yake kwako.
 
Acha kutumiana x kwenye magroup na kuforward huo ni uhuni huni flani huna mipaka
Si uangalie kwenye simu yako kutumiana ya nini?
 
Huyo ana wivu wakipuuzi kabsa!nimeshakumbana na mwanamke wa aina hiyo!mwisho wa siku nilimshindwa kabsa!kukupenda,anakupenda 101%.
 
Mkuu naona unatonesha tu vidonda vya wadau yaani... nilishawahi kuwa na wa aina hiyo mwenye wivu kupindukia alikua anasoma mpaka sms za mimi na washkaji zangu baada ya kuzikosa za wadada.. tulishindwana baadae.. ila ya kudai talaka kila mkitofautiana jua ya kwamba anajihami, kwa 99% ana mchepuko..mark my words..
 
Pole sana!
Mkeo ana wivu wa kijinga sana ambao una dalili za kuwa ukichaa. Kuchukua simu yako na kuwatukana watu asiowajua ni kukutia aibu na kukudharirisha, na kuna siku inaweza kukuletea kesi kubwa tu, rejea makosa ya mtandao.Kutuma clip ya x hadi kwa wazazi wako u ujinga uliopita kipimo, na nikusifu kwa uvumilivu wako!! Kama ana shangazi au dada zake wakubwa waombe wazungumze naye na kumuonya. na ukumbuke mara nyingi watu wa aina ya mkeo wana mambo yao ya siri hivyo muda wote hufikiri anayoyafanya na wewe unafanya, mchunguze pia!! akishindwa kujirekebisha mrudishe kwao kwa muda wakati ukitafakari!!
Nashukuru wagabuli kwa ushauri wako...nitazungumza na Dada yake mkubwa...huezi amini nilikua sina kabisa wazo hilo
 
Mkuu pole sana kwa unayokutana nayo kwa mkeo
 
Kaa utathmini tatizo lilipo myamalize ikishindikana, chungza pindi mlipoahidiana kuoana au ulipoamua kumuoa mazingira yalikwaje (upendo wa kulazimisha, upendo wa upande mmoja au upendo wa aina gani) usipopata jibu angalia ustarabu mwingine maana matusi kwenye ndoa, kejeli na makwazo huwa yanasababisha mengi na hata ulemavu kitu ambacho hukuwa nacho fikiria mara mbili, kama alikuwa rizki yako atatulia tu kama ulikuwa rizki yake utatulia si vinginevyo ni kuumizana. angalia magonjwa mengi kwa wanandoa ni presha, magonjwa ya moyo, vidonda vya tumbo, kuumizana mkiwa mnagombana... omba yasikufikie ni hatari sana
Nashukuru kwa ushauri...na kuhusu kuoana,,ni idea yake na nimemuoa kwa kweli hatuna shida sana zaidi nilizozitaja hapo juu...kinachoniuma ni kutonishirikisha kwa kitu ambacho ameona sio sawa yeye kukimbilia kwa wazazi maana anajua wana!kubali sana mke wangu
 
Mzee kwanin unaangalia Porn na huku umeoa?
Hapana mie nilitumiwa kwenye group kosa langu ni kuifoward kwa MTU mwengine... Nilikiri kosa ila yeye mpaka wakwe zake kawambia...kua mie naangalia x...sasa hapo ni sawa LIon?
 
Kaa utathmini tatizo lilipo myamalize ikishindikana, chungza pindi mlipoahidiana kuoana au ulipoamua kumuoa mazingira yalikwaje (upendo wa kulazimisha, upendo wa upande mmoja au upendo wa aina gani) usipopata jibu angalia ustarabu mwingine maana matusi kwenye ndoa, kejeli na makwazo huwa yanasababisha mengi na hata ulemavu kitu ambacho hukuwa nacho fikiria mara mbili, kama alikuwa rizki yako atatulia tu kama ulikuwa rizki yake utatulia si vinginevyo ni kuumizana. angalia magonjwa mengi kwa wanandoa ni presha, magonjwa ya moyo, vidonda vya tumbo, kuumizana mkiwa mnagombana... omba yasikufikie ni hatari sana

Well said.
 
Naomba nijue mpaka sasa umechukua hatua gan mana naona uzi una 4hrs ago then nitoe ushauri wngu
 
Aisee jamani naomba mnisaidie ...mie na mke wangu na mtoto wetu mmoja na huyu mke wangu tunapendana na kuahidiana mapenzi ya dhati cha ajabu.. Tunaweza tukawa tupo kwenye furaha mfulilizo...mpaka watu mtaani wanatumaind the way tunavyopendana... Sasa ikitokea tu kukorofishana kidogo wife ye hudai taraka.. Na siku nyengine hua anachukua cm yangu kwa siri halafu huanza kuchati na watu ambao anahisi yeye mie wapenzi wangu yaani akiona SMS hata imeandikwa""sawa wangu""..mitusi atakayopata huyo MTU si yanchi hii
Baya zaidi hua ananichunia sana akinuna atakaa hata siku 3 bila ya mawasiliano mazuri...hivi juzi kakuta nimetumiwa x kwenye group...na Mimi nikaifoward kwa MTU mwengine weeee....hadi wazazi wangu waliju kua naagalia x.. Sasa hii tabia nahisi ka inanichosha...mpaka naandika Uzi huu tayari ashadivert simu yangu...
Nahitaji jinsi ya kuiondoa hiyo divertion pia nahitaji nini cha kufanya ili amani itawale???
Nenda polisi
 
Unakumbuka ya kanumba na lulu lakini? Wanawake co wa kufanya nao mchezo
 
Back
Top Bottom