Msaada tutani kuhusu "Rythm foundation"

Msaada tutani kuhusu "Rythm foundation"

ludacris86

Member
Joined
Jul 22, 2022
Posts
22
Reaction score
122
Wadau naomba niende moja kwa moja kwenye mada

Kuna mtoto wa mama yangu mkubwa amenipigia simu kuwa amepata nafasi kwenye kampuni tajwa hapo juu ambayo inahusika na kutoa msaada kwa watoto yatima Africa na Asia kwa hiyo amejichanga amepungukiwa na kiasi kidogo ambacho anaomba nimsaidie...nimejaribu kui google ila information nnazopata sizielewi

Kwa maelezo yake anasema ametakiwa kutoa kiasi cha pesa cha tsh 2.3 million kwa ajili ya dhamana ya mafunzo,chakula,umeme na afya...kwa kweli I smell something fishy about this na bahati mbaya ameshatoka kijijini kuja Dar kwa ajili ya hiyo inshu..

Naombeni msaada kwa mtu anaeijua hii kampuni asije akaingizwa chaka mjini hapa
20221123_221633.jpg
 
Duh mjini akili tu,ungemuuliza mshahara sh ngapi?na kwanini iwe africa na asia na sio hapa Tanzania pekee?
 
Hiyo taasisi kama ingekuwa inashughulikia watoto bara la Afrika na Asia ina maana ni kubwa, ipo mabara mawili lazima taarifa zake zingekuwa mtandaoni

Halafu hiyo milioni 2.3 ya kazi gani?
 
Back
Top Bottom