Msaada: Tatizo la UTI limeisha lakini bado mkojo unaendelea kuchoma na kuwasha

MURUSI

JF-Expert Member
Jun 25, 2013
4,491
8,721
Habari wakuu.

Nilikuwa na shida ya UTI kwa muda ilinisumbua nikaja nikatumia dawa hasa za mitishamba ikaisha maana za dukani zilidunda zote.

Shida ni kwamba bado mkojo unakuwa unachoma ila nikipima no UTI. Nimeshapima hadi hospitali kubwa inaleta negative.

Je, nini tatizo? Msaada please

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jitahidi kunywa maji mengi,kuhusu dawa za mitishamba siziamini,ungefanya kipimo cha urine culture and sensitivity hospital,then ndo utumie specific drug

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi uume hadi umevimba kiasi kwenye tundu la kichwa cha uume.

Nitumie dawa gani?

ARUSHA KWETU
 
Kuna mtu mmoja alileta thread hapa na kutoa tiba muafaka ya uhonjwa huu. Sodium Bicarbonate ilinitibu kabisa tatizo hilo ambalo lilikuwa sugu sana kwangu. Nilitumia mitishamba na dawa za kizungu bila mafanikio. Tafadhali tumia hiyo Bicarbonate

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivyo ni vidonda kwenye mrija wa uretha endelea kunywa metronidazole

sent from toyota Allex
 
Kuna mtu mmoja alileta thread hapa na kutoa tiba muafaka ya uhonjwa huu. Sodium Bicarbonate ilinitibu kabisa tatizo hilo ambalo lilikuwa sugu sana kwangu. Nilitumia mitishamba na dawa za kizungu bila mafanikio. Tafadhali tumia hiyo Bicarbonate

Sent using Jamii Forums mobile app
Namna ya kutumia pls. Tusije kubwia unga kumbe unakoroga kwenye maji,tusije tumia pakti nzima kumbe unapima vijiko
 
Back
Top Bottom