Mjamzito; ameandamwa na tumbo, kichwa na anahisi kuna vitu vinatembea njia ya mkojo

Trainee

JF-Expert Member
Sep 22, 2018
2,208
2,808
Habari ndugu zangu...

Soma hii stori ya kumhusu mke wangu halafu naomba ushauri.

Tarehe 28 April 2020 nilimuoa (tukaingia kwenye fungate). Tarehe 4-5 May akasema tumbo linauma nikamnunulia dawa inaitwa amoxicillin (nilishauriwa kutokana na maelezo ya jumla aliyotoa)

Katikati ya May ikazuka hali mpya sasa ya kuhisi anataka kukojoa akienda mkojo hakuna au unatoka kidogo tu na anashinwa kuondoka chooni kwakuwa anakuwa bado anahisi anataka kukojoa; hali hii inamtokea pengine siku nzima akienda chooni anakaa karibu dakika 30 na akitoka hachukui dakika 15 amerudi tena chooni.

Akawa anapata nafuu (anapona) mara vinatimka tena na kichwa basi ikawa ni mwendo wa paracetamol na amoxicillin (hakupimwa). Hali ikawa ndo hiyo lakini kilichonipa wazimu ni hii ya mkojo kwani alisema anahisi kama anatekenywa kuna vitu vitu vinatembea kwenye njia ya mkojo

Tarehe ishirini na kitu May tukapewa ciprofloxacin (bila kupimwa) wakisema itakuwa ni UTI dozi ikaisha siku saba bila yeye kuonesha dalili ya kupona . Mwezi June mwanzoni ndo akapimwa akaonekana ni mjamzito ila ana Malaria basi akapewa quinine vidonge na kuanza clinic mojakwamoja. Akamaliza dozi hali bado kurudi zahanati wakasema atumie tu amoxicillin itatulia nikanunua dawa lakini sikumpa anywe kesho asubuhi nikafunga safari mpaka hospitali.

Ilikuwa tar24 June Kufika kule akamulikwa x-ray na kupimwa tena wakasema ni malaria ila mimba haina shida ina wiki 7 na siku 1. Basi wakaandika amoxillin na quinine ila safari hii sindano sasa siyo vidonge tena. Basi kitu nilichoshukuru ni kwamba walimzungusha zungusha pale nenda huku rudi kule hakuchomwa basi mke wangu akanipigia niende pale nikamsaidie achomwe sindano (maana nilitoka kidogo pale hospitali- utajua mbeleni kwanini nilishukuru walivyomzungusha)

Basi me nilipofika pale sikuwakuta wahusika wote naambiwa wametoka kidogo eti kwa hasira nikamwambia mke twende utendachomewa kule zahanati kijijini kwetu... kufika nikamwambia anywe zilezile aliandikiwa zahanati halafu sindano twende akachomwe na nesi pale pale

Bwana wewe kufika nesi anaangalia chupa zile zime expire siku nyingi tukazitupa anaendelea na amoxicillin lakini hatahivyo tatizo lipo palepale na juzi amejisaidia minyoo miwili mirefu kwenda zahanati wakasema mpaka afike miezi mitatu mimba ndo atakula dawa za minyoo


Msaada tafadhali!
Tanbihi;
Sijabobea kwenye uandishi kwahiyo inawezekana sehemu nyiingine ikawa nimechanganya madesa!... kikubwa tuvumiliane

Sent from my SM-G532F using JamiiForums mobile app
 
Duuh pole sana. Ila upo mkoa gani?

Maana nijuavyo mimi mjamzito siyo mtu wa kupewa madawa dawa.

Ila acha hayo mambo ya madawa dawa tafuta Dr/ specialist mzuri amsaidie mkeo ,mtatoa hiyo mimba msipoangalia.

Madokta mje msaada unaitajika haraka...
 
Duuh pole sana. Ila upo mkoa gani?

Maana nijuavyo mimi mjamzito siyo mtu wa kupewa madawa dawa.

Ila acha hayo mambo ya madawa dawa tafuta Dr/ specialist mzuri amsaidie mkeo ,mtatoa hiyo mimba msipoangalia.

Madokta mje msaada unaitajika haraka...
Asante lakini hata hao walionifanya nimpatie dawa hizo niliwatafuta (ni watoa huduma) kwenye hospitali na zahanati zetu nchini sasa kama una suluhisho ni bora kuniambia tu kuliko kusema nikutafute
 
Asante lakini hata hao walionifanya nimpatie dawa hizo niliwatafuta (ni watoa huduma) kwenye hospitali na zahanati zetu nchini sasa kama una suluhisho ni bora kuniambia tu kuliko kusema nikutafute
@THEBADDEST
 
mmmh nayo madawa yote ya nini kwa mkeo?
Hiyo ya kuhisi mkojo Mara nyingi ni Dalili ya UTI na inaweza kuwa inamrudia kwa sababu mnakutana na hamtibiwi wote

mwambie mkeo ajitahidi kunywa maji mpaka Lita 3 per day,
Tikiti nalo linafaa

pia anaweza kutengeneza detox ya Tango,mnanaa na maji ya dafu akanywa Hiyo hali itaondoka kabisa
 
Duuh pole sana. Ila upo mkoa gani?

Maana nijuavyo mimi mjamzito siyo mtu wa kupewa madawa dawa.

Ila acha hayo mambo ya madawa dawa tafuta Dr/ specialist mzuri amsaidie mkeo ,mtatoa hiyo mimba msipoangalia.

Madokta mje msaada unaitajika haraka...
Dawa niliyompa bila ya kupimwa ni ciprofloxacin tu kama umefuatilia maelezo yangu... hizo zingine ni wataalamu wa afya wamemwandikia baada ya kujiridhisha na vipimo walivyomchukua mgonjwa kuzingatia na hali yake.

Tena huyohuyo aliyenishauri nnunue ciprofloxacin tunywe na mke wangu (kabla ya mimba kugundulika) ndiye aliyekuja kumwandikia quinine ya vidonge na ndipo akasema kama angepima mimba mapema asingeshauri mjamZito anywe cipro

Kwahiyo nakubaliana na wewe kwamba madawa sana hayafai kwa mjamzito lakini nakupinga kwa upande mwingine kwakuwa wanaoniandikia kununua hizo dawa ni haohao wahudumu wa hospitalini na zahanati baada ya vipimo (siyo kwamba nilienda kununua tu mwenyewe kienyeji bali hospitalini hakuna ndomana kama uliona nilileta uzi humu)
 
mmmh nayo madawa yote ya nini kwa mkeo?
Hiyo ya kuhisi mkojo Mara nyingi ni Dalili ya UTI na inaweza kuwa inamrudia kwa sababu mnakutana na hamtibiwi wote

mwambie mkeo ajitahidi kunywa maji mpaka Lita 3 per day,
Tikiti nalo linafaa

pia anaweza kutengeneza detox ya Tango,mnanaa na maji ya dafu akanywa Hiyo hali itaondoka kabisa
Asante sana ndugu yangu nitajitahidi aivipate na hivi vitu
 
Dawa niliyompa bila ya kupimwa ni ciprofloxacin tu kama umefuatilia maelezo yangu... hizo zingine ni wataalamu wa afya wamemwandikia baada ya kujiridhisha na vipimo walivyomchukua mgonjwa kuzingatia na hali yake...
Haupo serious mara ukashikwa na hasira ukaenda zahanati ya kijijini kwetu.
Tafuta madaktari wa kuelekea ishu ya mkeo siyo ya kuonea na nesi.
Isitoshe zahanati za vijijini zina matabibu.

Nimekwambia tafuta Dr mzuri/ specialist uliziaulizia huko watu wakusaidie mkoani kwako jinsi ya kuwapata hata kama hospitali ya private.

Ng'ang'ania hivyo hivyo tu hizo nazo unapata hosp shauri yako....
 
Mkuu pole sana mimi hapo nitakusaidia dawa ya asili ya kuondosha minyoo kwa Mke wako tumia hii njia salama kwa afya yake . chukuwa nyanya moja asubuhi isafishe kwa maji kisha kata silesi

kisha chukuwa Pilipili mtama nyeusi nusu kijiko kimoja kidogo achanganye kwa hiyo nyanya. Kisha awe anakula pamoja na hiyo nyanya kila siku asubuhi kabla ya kula kitu atumie hiyo dawa kwa muda wa siku 14 minyoo yote tumboni itakufa.Na kuhusu maradhi sugu ya UTI nitafute kwa wakati wako nipate kumtibia mke wako.
 
Dawa niliyompa bila ya kupimwa ni ciprofloxacin tu kama umefuatilia maelezo yangu... hizo zingine ni wataalamu wa afya wamemwandikia baada ya kujiridhisha na vipimo walivyomchukua mgonjwa kuzingatia na hali yake.

Tena huyohuyo aliyenishauri nnunue ciprofloxacin tunywe na mke wangu (kabla ya mimba kugundulika) ndiye aliyekuja kumwandikia quinine ya vidonge na ndipo akasema kama angepima mimba mapema asingeshauri mjamZito anywe cipro..
Ndugu ciprofloxacin sio dawa inayotakiwa kupewa mjamzito anayeumwa UTI kwa sababu inaingilia ukuaji wa baadhi ya sehemu za mifupa tena kwa mke wako ambaye ndio kwanza bado yupo kwenye 1st trimester sio nzuri kabisa.

Standard guideline ya nchi yetu katika kutibu UTI ni kutumia Amoxicillin lakin tatizo hii amoxicillin inatumika sivyo na hivyo imetengeneza usugu kwa bacteria so inaweza isiwe na matokeo chanya. Kama mke wako amepimwa na akathibitika na UTI, dawa nzuri kwa UTI ni umtafutie either Nitrofurantoin au Nalidixic acid
 
Mkuu pole sana mimi hapo nitakusaidia dawa ya asili ya kuondosha minyoo kwa Mke wako tumia hii njia salama kwa afya yake . chukuwa nyanya moja asubuhi isafishe kwa maji kisha kata silesi...
Safi mkuu kama hii njia yako ya asili itamsaidia kuondoa minyoo itakuw jambo la kheri sana maana mpaka kusubiria miez mi3 ipite ndio apewe dawa za minyoo hao wadudu watakuw wanazid kukua tu na kuzaliana
 
Hapana... ni x-ray

kafanyeni na pelvic ultrasound sababu saa nyingine kutanuka kwa mfuko wa uzazi inakandamiza kibofu cha mkojo sasa kwa case iyo sometimes cervix inasogea mbele inaminya sehem ya chini ya kibofu then anatapa kitu kama urine retention ambapo anaskia kabanwa na mkojo akienda kukojoa hautoki au unatoka kidogo kidogo na bora itoke kidogo kidogo kuliko kutotoka kabisa.

Kwahiyo ukipata retention pressure ndani ya kibofu cha mkojo inaongezeka mkojo unakua unazunguka kuja chini na kuflow juu kidogo kwa kurudia rudia ndo maana anakwambia anaskia vitu vinatembea kweny njia ya mkojo kutokana na stimulation ya nerves zilizo kweny njia ya mkojo ,pia ikiwa ivo ni rahis kwake kupata U T I mara kwa mara.

Kwahiyo, nenda hospital kubwa ufanye vipimo pamoja na iko cha ultrasound ,pia mkeo anaweza kuwa na stricture njia ya mkojo inakua nyembamba sana sehem flan kuliko kawaida na ostruction zingine ambazo wataona kwenye vipimo
 
Back
Top Bottom