Msaada: Tafsiri ya ndoto yangu - Nimeenda eneo nisilolijua na kukutana na vitisho

Dupe

JF-Expert Member
Jan 21, 2013
1,668
811
Ilikuwa ni usiku wa jana kuamkia leo nilipojikuta naingia kwenye ndoto ambayo mpaka sasa sijapata kujua ikomaanisha nini.

Ndoto Yenyewe:

Tulikuwa watu wawili yaani nimimi na mdogo wangu, mdogo wangu aliniomba nimsindikize mahala fulani ambaki mpaka sasa sipajua palikuwa wapi…!!

Tulifika kwenye hiyo nyumba tukaingia ndani ile nyumba ilikuwa haijaisha kwa kujengwa, yaani mithili ya mtu akiejenga alikuwa kaishindwa so watu wakapangishwa, mdogo wangu alikuwa mbele yangu maana ye ndio alijua wapi tunaenda.

Katika hiyo nyumba ilikuwa ina milango kama nane, yote ilikuwa inaangaliana. Tukapita katikati hadi kwenye mlango wa mwisho wa kushoto wa mkono wetu. Mule kwenye kile chumba hakukuwa na mtu yeyote na mdogo wangu aliingia mpaka ndani na akatoka haraka, mie nikiishia mlangoni pasi kuona ni nini alikiona mule ndani au ndani kulikuwa na nini! Niliona kitanda tu, ambacho kilikuwa na shuka jeupe.

Nilipoona mdogo wangu katoka nami niligeuza paleplale. Wakati tunatoka kabla hatujaimaliza ile nyumba kutoka, yule mwenye chumba ambacho tuliingia akawa anaingia ndani na yeye. Yule mdogo wangu alipomuona alikuwa anacheka na akakimbia huku akiniacha nyuma nikipigwa na butwaa…!!

Yule mama alisimama akaniangalia akaingia chumban kwake na akarudi tena, aliporudi alinikuta mimi nikitoka pale, akanifuata akasimama mbele yangu huku akinitazama kwa hasira…!!

Akachukua mikaa mitatu akanipiga nayo kifuani halafu akanisonya na kuniambia "Ole wenu mukasimulie…!!".

Hapa ndipo nilipochanganyikiwa kabisa mpaka sasa na sijajua nyumba ambayo tuliingia iko wapi na yule mama alienichimba mkwala simjui.

Naomba msaada wa tafsiri wa ndoto hii waungwana..

cc: Mshana Jr
cc: MziziMkavu
 
Kama sio wewe mwenyewe,basi anaweza kuwa mdogo wako ana mambo ya ushirikina na amekuwa akikusumbua akili zako kwa namna mambo yake anavyofanya,sasa ameamua kuja kukuchukua na kukupeleka ukaone kazi afanyayo ili uache kumfatilia
 
Kama sio wewe mwenyewe,basi anaweza kuwa mdogo wako ana mambo ya ushirikina na amekuwa akikusumbua akili zako kwa namna mambo yake anavyofanya,sasa ameamua kuja kukuchukua na kukupeleka ukaone kazi afanyayo ili uache kumfatilia
Mkuu mimi habari za ushirikina sina kabisa wala sijawahi ata kuchanjwa au kwenda kwa mganga kufanya jambo lolote lile na isitoshe huu mkwala tumepigwa wote kwa maana alisema "OLE WENU MUKASIMULIE"
 
Last edited:
Hiyo ndoto kama inakunyima raha likely inakuwa na maana. Maana ukisoma ndoto zote tata walizowahi kuota watu duniani wafalme na wengineo wakakosa raha huwa na maana. My take, jaribu kutafuta wataalamu wa hiyo mambo wakupe maana halisi. Humu bila shaka kuna specialists kwenye hizo area.
 
Hivyo vyumba vinavyotazamana nadhan ni lile danguro la pale temeke kwa wahaya, mdogo wako ana mteja pale, muulize
 
Mkuu usiwe na wasiwasi kwa jinsi ulivyoielezea hiyo nyumba haitakua salama na hii BOMOABOMOA.kwahiyo ishukuru serikali ya JPM kwa kulimaliza tatizo lako.
 
Hiyo ndoto kama inakunyima raha likely inakuwa na maana. Maana ukisoma ndoto zote tata walizowahi kuota watu duniani wafalme na wengineo wakakosa raha huwa na maana. My take, jaribu kutafuta wataalamu wa hiyo mambo wakupe maana halisi. Humu wanaunga unga tu ila kuna specialists kwenye hizo area.
Ahsante sana mkuu ila kuna watu kama @mshanaJr MziziMkavu
 
Kama ni mtu wa dini kaza sana kwenye maombi ina elekea sehemu mnayoishi kuna matatizo ya kutokuelewana either ww na jirani zako na chanzo ni mdogo wako ndo aliesababisha tukirudi kwenye kutupiwa mkaa ina mana mkaa kama kitu cheusi ni kama mikosi ila inavyo elekea ulitupiwa ila haikuweza kukudhuru na huyu aliekutupia anahisi kama umemgundua ndo mana akasema ole wenu mkasimulie ni vyema ukazid kumuomba mungu ila si kila ndoto ina maana nyingne ni mlundikano wa mawazo au bongo movies unazoziangaliaga badae unaziota
 
Kama ni mtu wa dini kaza sana kwenye maombi ina elekea sehemu mnayoishi kuna matatizo ya kutokuelewana either ww na jirani zako na chanzo ni mdogo wako ndo aliesababisha tukirudi kwenye kutupiwa mkaa ina mana mkaa kama kitu cheusi ni kama mikosi ila inavyo elekea ulitupiwa ila haikuweza kukudhuru na huyu aliekutupia anahisi kama umemgundua ndo mana akasema ole wenu mkasimulie ni vyema ukazid kumuomba mungu ila si kila ndoto ina maana nyingne ni mlundikano wa mawazo au bongo movies unazoziangaliaga badae unaziota
Asante mkuu lwa ushauri wako
 
Kipindi cha miaka ya nyuma kuna ndoto moja nilikuwa naota halafu ikawa inajirudia rudia sana. Nikawa naona kawaida.

Ndoto ilikuwa hivi: Nilikuwa naota napita kwenye nyumba moja hivi ambayo maji yalikuwa yanatuama. Kila nikipita kwenye hiyo nyumba nilikuwa naona mtu mzima ana meno yameharibika yupo darani amejikunja. kwa neno lingine kama msukule.

Kipindi hicho kuna nyumba nilikuwa nimepanga na kila wakati mvua ikinyesha maji yalikuwa yanaingia mpaka ndani na kwa muda kama wa wiki moja yanatuama. Kuna siku moja mvua kubwa sana ilinyesha na maji yakaingia kwangu na kwa majirani tuliyopanga wote. katika kutoka nje na kupiga story yule jirani yangu akaniuliza. 'kuna kitu huwa nasikia kinatembea kwenye dari usiku, wewe umeshakisikia?' nikamjibu 'nimeshasikia watakuwa paka' akaniambia ' hapana kaka sio paka sikiliza vizuri. Dah jamaa akawa amenifungua akili yangu. kweli bwana kila nikisikiliza sio paka. Baadaye nilikuja kuhama na ikawa mwisho wa hiyo ndoto.

Muda woooote naota ndoto kumbe ni kunitaarifu kitu. kwa bahati nzuri baadaye nikaja kusoma Bibilia kitabu cha Ayubu 33:14-18

33:14 Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali.

33.15 Katika ndoto, katika maono ya usiku, Usingizi mzito uwajiliapo watu, Katika usingizi kitandani;

33.16 Ndipo huyafunua masikio ya watu, Na kuyatia muhuri mafundisho yao,

33.17 Ili amwondoe mtu katika makusudio yake, Na kumfichia mtu kiburi;

33.18 Yeye huizuia nafsi yake isiende shimoni, Na uhai wake usiangamie kwa upanga.

TAFAKARI:
 
Kipindi cha miaka ya nyuma kuna ndoto moja nilikuwa naota halafu ikawa inajirudia rudia sana. Nikawa naona kawaida.

Ndoto ilikuwa hivi: Nilikuwa naota napita kwenye nyumba moja hivi ambayo maji yalikuwa yanatuama. Kila nikipita kwenye hiyo nyumba nilikuwa naona mtu mzima ana meno yameharibika yupo darani amejikunja. kwa neno lingine kama msukule.

Kipindi hicho kuna nyumba nilikuwa nimepanga na kila wakati mvua ikinyesha maji yalikuwa yanaingia mpaka ndani na kwa muda kama wa wiki moja yanatuama. Kuna siku moja mvua kubwa sana ilinyesha na maji yakaingia kwangu na kwa majirani tuliyopanga wote. katika kutoka nje na kupiga story yule jirani yangu akaniuliza. 'kuna kitu huwa nasikia kinatembea kwenye dari usiku, wewe umeshakisikia?' nikamjibu 'nimeshasikia watakuwa paka' akaniambia ' hapana kaka sio paka sikiliza vizuri. Dah jamaa akawa amenifungua akili yangu. kweli bwana kila nikisikiliza sio paka. Baadaye nilikuja kuhama na ikawa mwisho wa hiyo ndoto.

Muda woooote naota ndoto kumbe ni kunitaarifu kitu. kwa bahati nzuri baadaye nikaja kusoma Bibilia kitabu cha Ayubu 33:14-18

33:14 Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali.

33.15 Katika ndoto, katika maono ya usiku, Usingizi mzito uwajiliapo watu, Katika usingizi kitandani;

33.16 Ndipo huyafunua masikio ya watu, Na kuyatia muhuri mafundisho yao,

33.17 Ili amwondoe mtu katika makusudio yake, Na kumfichia mtu kiburi;

33.18 Yeye huizuia nafsi yake isiende shimoni, Na uhai wake usiangamie kwa upanga.

TAFAKARI:
.mkuu hapa umeniacha njia panda kabisaa
 
#Mshana Jr
#MziziMkavu
Ahsante sana mkuu ila kuna watu kama @mshanaJr MziziMkavu
Kwanza mojawapo ya makundi ya ndoto ni ndoto zinazotokana na kumbukumbu ya yale tuyawazayo tuliyoyaona na kutenda pia
Kundi la pili ndoto maono hizi hubeba taarifa fulani muhimu toka kwa watu tofauti Hasa wafu na wakati mwingine hata Mungu mwenyewe
Kundi la tatu ni ndoto zenye uhalisia hizi mara nyingi huambatana na mambo ya kishirikina
Ndoto yako inaangukia kundi la tatu endelea kufuatilia kwa Karibu kwa wiki nzima Kama itajirudia
 
ndoto ziko na maana nyingi aisee! na kila mtu atakutafsiria kivyake na unaweza kupotea. la msingi muombe Mungu akuepushe na mbaya tuu. note zaburi 140
 
Kwanza mojawapo ya makundi ya ndoto ni ndoto zinazotokana na kumbukumbu ya yale tuyawazayo tuliyoyaona na kutenda pia
Kundi la pili ndoto maono hizi hubeba taarifa fulani muhimu toka kwa watu tofauti Hasa wafu na wakati mwingine hata Mungu mwenyewe
Kundi la tatu ni ndoto zenye uhalisia hizi mara nyingi huambatana na mambo ya kishirikina
Ndoto yako inaangukia kundi la tatu endelea kufuatilia kwa Karibu kwa wiki nzima Kama itajirudia
Ahsante sana mkuu ila kwa kawaida niliwahi ota ndoto ambayo ilijirudia mara 2 tu na hii ilikuwa niya kumbukumbu ambayo pia imeingua kwenye ushirikina ila niliipotezea tu na hii ilikuwa namjua nani anafanya hivo vitu ila mara zote niliota kama anataka kunikamata ila nikawa namkwepa mara zote hii ilikuwa ndoto naota niko kwenye nyumba yake akawa anataka kunishika mie nikawa nainama ananikosa
 
Pole kwa kukuacha njia panda. Mimi sio mtaalam wa ndoto. Ila haya yanawezekana;

1. Kama ndoto itajirudia rudia inawezekana Mungu anakupa onyo.
2. Kama yule mama uliona sura yake na unamfahamu basi muombe Mungu ili akupe ufafanuzi zaidi
3. Muulize mdogo wako kama kuna ndoto ameota hivi karibuni na unganisha dots.....
4. Mara nyingi utakuta mtu hata hajawahi kwenda kwa mganga na wala hapendi kusikia ushirikina. Lakini anatumika kwenye ushirikina kwa njia moja au nyingine. Inawekana ukiwa mdogo ndugu zake mama au baba au hata bibi/babu au hata mashangazi walichomeka mambo kwako.

MY TAKE: kutokujihusisha na ushirikina wala imani zao kama hujafunikwa na damu inenayo mambo mema (damu ya Yesu) ni bure. utatumika na kutumikishwa. Kumbuka dhambi zetu ndo huwa zinafanya tutumikishwe. Hata ukitumia damu ya yesu na bado kuna sehemu wanapata chance ya kuingia kwa sababu ya dhambi unazofanya watakutumia tu. Na dhambi sio kuzini tu hata kukasirikia na kuwa na chuki.
 
Back
Top Bottom