MWAMUNU
JF-Expert Member
- Dec 17, 2011
- 866
- 526
Heshima kwenu wakubwa zangu, na madogo hamjambo.
Niende moja kwa moja kwenye hoja.
Asubuhi hii saa 12 nimeota ndoto ambayo inaninyima raha sana, .
Katika ndoto hiyo nimeota nimesingiziwa nimeiba box 9 za karatasi nyeupe yaani rim paper na kufungwa miaka miwili jela
Nikiwa jela napata taarifa kwamba jamaa yangu kipenzi (jina namhifadhi)amefariki dunia, nasikitika na kumlilia sana.
Baada ya kumaliza kifungo siku hiyo hiyo naingia mtaani huku ndugu na jamaa wakiendelea kunipa pole, mara jamaa yangu niliyeambiwa amefariki nae anatokea na kunipa pole, namuuliza we si nimeambiwa umekufa ananijibu achana nao wanafiki hao.
Namuuliza umejuaje nimetoka ananijibu fulani(Jina namhifadhi) kakusanya watu anawasimulia watu kwamba uliiba box 9 za karatasi na kwamba walihakikisha hutoki hata kama una uwezo wa kuzilipa.
Ikumbukwe huyo jamaa anayeninenea mabaya huku kwenye maisha ya kawaida ni Mzee wa kanisa na ndie aliesimamia ndoa yangu, japo ilishavunjika, Mwisho wa ndoto yangu.
Wakuu kama kuna wajuzi wa kufafanua ndoto naomba msaada hii ndoto ina maana gani?
Nimeota asubuhi hii na nakumbuka kila kitu yaaani kama movie vile.
Natanguliza shukrani, kama huna la kuchangia pita kimya kimya.
Niende moja kwa moja kwenye hoja.
Asubuhi hii saa 12 nimeota ndoto ambayo inaninyima raha sana, .
Katika ndoto hiyo nimeota nimesingiziwa nimeiba box 9 za karatasi nyeupe yaani rim paper na kufungwa miaka miwili jela
Nikiwa jela napata taarifa kwamba jamaa yangu kipenzi (jina namhifadhi)amefariki dunia, nasikitika na kumlilia sana.
Baada ya kumaliza kifungo siku hiyo hiyo naingia mtaani huku ndugu na jamaa wakiendelea kunipa pole, mara jamaa yangu niliyeambiwa amefariki nae anatokea na kunipa pole, namuuliza we si nimeambiwa umekufa ananijibu achana nao wanafiki hao.
Namuuliza umejuaje nimetoka ananijibu fulani(Jina namhifadhi) kakusanya watu anawasimulia watu kwamba uliiba box 9 za karatasi na kwamba walihakikisha hutoki hata kama una uwezo wa kuzilipa.
Ikumbukwe huyo jamaa anayeninenea mabaya huku kwenye maisha ya kawaida ni Mzee wa kanisa na ndie aliesimamia ndoa yangu, japo ilishavunjika, Mwisho wa ndoto yangu.
Wakuu kama kuna wajuzi wa kufafanua ndoto naomba msaada hii ndoto ina maana gani?
Nimeota asubuhi hii na nakumbuka kila kitu yaaani kama movie vile.
Natanguliza shukrani, kama huna la kuchangia pita kimya kimya.
